Leo Rais kasema wamelipa madeni ya pension, mbona wastaafu ATCL bado hawajalipwa?

kisingi

JF-Expert Member
Apr 9, 2014
516
377
Serikali inajinasibu kulipa madeni yote ya wastaafu kiasi cha shilingi trillion 1.3. Leo hii katika mkutano wa walimu Dodoma raisi Magufuli amerudia kuwa wamekwisha lipa. Mbona viongozi wa PPF wanasema hawajapokea pesa ya madai ya wastaafu wa ATCL.

Wanasema walichopokea ni malipo ya madeni wao waliikopesha serikali. Hali hii inawasikitisha wastaafu ATCL kwani hawaelewi nani mkweli katika ya raisi na viongozi wa PPF.

Ama waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano amepeleka pesaxhizo mahala pengine na anabaki kuahidi kulipa tu. Hii danadana kwa wastaafu wa ATCL inhitaji ufumbuzi kwani ni haki yao kisheria na wamekatwa toka mishahara yao wakati wakiwa kazini.

Serikali iwe ya watendaji wa kweli na wazi kuwa SSRA haina uwezo wa kusimamia mifuko kwani suala la wastaafu ATCL wanalifahamu na hakuna hatua madhubuti walizo chukua hata baadaya mahakama kuamuru kukamata mali za ATCL ili kuwalipa wastaafu hawa haki zao.

Ofisi ya katibu mkuu kiongozi analijua suala hili lakini maagizo yake nae yamepuuzwa. Tunaomba serikali ilipe hawa wastaafu ATCL na sio kufanya siasa na kutoa ahadi hewa.
 
Hebu wizara Ujenzi ijibu suala hili maana raisi hawezi kulidanganya taifa. Tatizo ni wasaidizi wake hasa mawaziri
 
Bado siamini kuwa raisi kasema uwongo bali waziri wa Ujenzi, Uchukuzi, na Mawasiliano, Makame Mbarawa ndio muongo. Nasikia aliahidi kwa maandishi kulipa mwezi wa nane na baadaye akasema December na mwezi ndio unayoyoma. Kama hakulipa mwezi huu nitakubaliana nanyi kuwa mkulu ni muongo na hutumia mawaziri kutekeleza uwongo wake.
 
Serikali inajinasibu kulipa madeni yote ya wastaafu kiasi cha shilingi trillion 1.3. Leo hii katika mkutano wa walimu Dodoma raisi Magufuli amerudia kuwa wamekwisha lipa. Mbona viongozi wa PPF wanasema hawajapokea pesa ya madai ya wastaafu wa ATCL.

Wanasema walichopokea ni malipo ya madeni wao waliikopesha serikali. Hali hii inawasikitisha wastaafu ATCL kwani hawaelewi nani mkweli katika ya raisi na viongozi wa PPF.

Ama waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano amepeleka pesaxhizo mahala pengine na anabaki kuahidi kulipa tu. Hii danadana kwa wastaafu wa ATCL inhitaji ufumbuzi kwani ni haki yao kisheria na wamekatwa toka mishahara yao wakati wakiwa kazini.

Serikali iwe ya watendaji wa kweli na wazi kuwa SSRA haina uwezo wa kusimamia mifuko kwani suala la wastaafu ATCL wanalifahamu na hakuna hatua madhubuti walizo chukua hata baadaya mahakama kuamuru kukamata mali za ATCL ili kuwalipa wastaafu hawa haki zao.

Ofisi ya katibu mkuu kiongozi analijua suala hili lakini maagizo yake nae yamepuuzwa. Tunaomba serikali ilipe hawa wastaafu ATCL na sio kufanya siasa na kutoa ahadi hewa.
Imeshatoka hiyo wapambane na hali zao.
 
Kama waziri kasema uwongo kwa ushahidi wa maaandishi nashauri wasipo lipwa wastaafu hawa wa ATCL waende mahakamani kumshitaki waziri na waende CLOUDS TV wakamshushue msemaji mkuu wa serikali aliyedanganya taifa kupitia kupindi cha CLOUDS 360;kuwa serikali imelipa madeni ya wastaafu wote wakiwemo wa ATCL kitu ambacho hakija fanyika.
 
Serikali inajinasibu kulipa madeni yote ya wastaafu kiasi cha shilingi trillion 1.3. Leo hii katika mkutano wa walimu Dodoma raisi Magufuli amerudia kuwa wamekwisha lipa. Mbona viongozi wa PPF wanasema hawajapokea pesa ya madai ya wastaafu wa ATCL.

Wanasema walichopokea ni malipo ya madeni wao waliikopesha serikali. Hali hii inawasikitisha wastaafu ATCL kwani hawaelewi nani mkweli katika ya raisi na viongozi wa PPF.

Ama waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano amepeleka pesaxhizo mahala pengine na anabaki kuahidi kulipa tu. Hii danadana kwa wastaafu wa ATCL inhitaji ufumbuzi kwani ni haki yao kisheria na wamekatwa toka mishahara yao wakati wakiwa kazini.

Serikali iwe ya watendaji wa kweli na wazi kuwa SSRA haina uwezo wa kusimamia mifuko kwani suala la wastaafu ATCL wanalifahamu na hakuna hatua madhubuti walizo chukua hata baadaya mahakama kuamuru kukamata mali za ATCL ili kuwalipa wastaafu hawa haki zao.

Ofisi ya katibu mkuu kiongozi analijua suala hili lakini maagizo yake nae yamepuuzwa. Tunaomba serikali ilipe hawa wastaafu ATCL na sio kufanya siasa na kutoa ahadi hewa.

Kiongozi unachofanya ni kutafuta kitu ambacho hakipo.
Jana JPM amesema serikali imelipa Deni ambalo serikali ilikopa kutoka mifuko ya hifadhi ya jamii kwa ajili ya uwekezaji na huo ndio UKWELI,je ulitaka viongozi wa PPF wakujibu nini?
 
Bila shaka hizo takwimu za ulipaji madeni amepewa na NBS, wazee wa kupika data
 
Kama kawaida yenu ninyi PPF kazi yenu kupindisha hotuba ya raisi na maelezo aliyotoa msemaji mkuu wa serikali katika kipindi cha CLOUDS 360. Je mbona mnakiuka sheria na kanuni za SSRA zinazo wataka kuwalipa wastaafu haki zao zote na ninyi kushughuluka na mwajiri ambae ni ATCL katika suala hili. Hata pale kesi mliyofungua mahakamani na kupewa amri ya kukamata mali za ATCL na kuziuza hamkufanya. Huu ni udhaifu mwingine wa utendaji kazi wa baadhi ya watumishi wa PPF wachumia matumbo kwa kukandamiza na kumeza haki za wastaafu. Kama hujui sheria na kanuni za SSRA kuhusu mifuko ya jamii na utekelezaji wake kaa kumya maana unaonyesha ni mmoja wa wanao sababisha mifuko hiyo kuonekana kuwa ni utitiri na inastahili kufutwa.
 
Kulipa madeni ya pensheni kama ulivyoweka kichwa cha habari na kulipa wastaafu ni vitu viwili tofauti. Umeeleza hiyo mifuko imelipwa walichoikopa serikali. Sasa unachanganywa na nini?
 
Back
Top Bottom