Leo nimepata jibu kwanini Waethiopia wanakimbia nchi yao

elmagnifico

JF-Expert Member
Jul 7, 2011
8,260
9,698
Kwa taarifa tunazosikia ni kwamba uchumi wa Ethiopia ni kati ya uchumi ambao unakuwa kwa kasi. Wanajenga miundombinu safi, wamezindua train safi ya umeme na mambo kadha wa kadha.

Ila siku zote nilikuwa najiuliza, ni kwanini kila mara waethiopia wanahatarisha maisha yao, wanakubari kubebwa kwenye makontena kupita Tanzania kwenda Afrika ya Kusini na wengine wanafia njiani.

Siyo hao tu kuna wa Ethiopia walichinjwa na ISIS huko Libya wakiwa wanajaribu kufikia bahari ya Mediteranean wapate kuvuka kuingia Italy.
Katika pitapita zangu huko mtandaoni nikajiunga na group la Waethiopia, katika kuchat na mmoja ndipo akaniambia yeye kamaliza degree, ameajiriwa serikalini kama messenger.

Mshahara wake ni kama USD 50 kwa mwezi. Nikashangaa maana kuna muda nimemtajia USD 500, akasema huo ni mshara wake wa miezi kumi. Akaanza kunieleza kuwa serikali inajenga miundombinu, ikitaka aminisha dunia kuwa uchumi unakuwa lakini maisha ya raia wa kawaida ni magumu sana sana.
Anadai kupata kazi ni vigumu labda uwe una pesa ya kuhonga au unamjua mtu mkubwa serikalini.

Akaniambia yeye ana degree ila ni messenger ila boss wake pale kazini ana diploma. Akaniambia ya kwamba watu wengi hawana chakula hawajui watakula nini, ila watawala wanajilipa mishara mikubwa na wanaishi maisha ya kifahari.
Uhuru wa kuongea hakuna ukileta kelele kukuua hawaoni hatari.

Anadai kukiwa na mikutano ya kimataifa, omba omba na watu wanaonyesha umasikini wanaondolewa wote addis ababa mpaka mkutano utakapoisha huwezi kuona masikini na omba omba. Nimekaa nikatafakari nikaona maendeleo na maisha bura siyo train wala fly overs tu, inabidi vyote viende sambamba na kuboresha kipato cha mwananchi wa kawaida.
 
Elimu kwa maboss na wafanyakazi wa chini yao hilo jambo ni la kawaida sana tena ni duniaani kote.

Tatizo, ni kwenye upendeleo , una sifa anapewa mtu asiye na sifa.

"Who knows who to get an opportunity" hapo ndiyo shida hasa pale jamii au watu wa familia moja wakipewa madaraka tangia taasisi au ofisi inaanzishwa hadi kifo ofisi haina mtu tofauti na jamii hiyo.
 
Nchi za magharibi zlifuata mtindo huu zamani. Ni mapinduzi ya Ufaransa ndiyo yaliamsha watu. Viongozi walianza kuiangalia social benefits kama kishawishi kwa wapiga kura.

Kila kiongozi alikuja na manifesto ya elimu, afya, makazi, ajira na pesa za kujikimu kwa wasio na kazi.

Raia wanapopata mahitaji muhimu hawana muda wa kuilalamikia serikali. Mipango makubwa ya maendeleo inapata nafasi.
 
Nchi za magharibi zlifuata mtindi huu zamani. Ni mapinduzi ya Ufaransa ndiyo yaliamsha watu. Viongozi walianza kuiangaliaw social benefit kama kishawishi kwa wapiga kura.

Kila kiongozi alikuja na manifesto ya elimu, afya, makazi, ajira na pesa za kujiku kwa wasio na kazi.

Raia wanaopata mahitaji muhimu hawana muda wa kuilalamikia serikali. Mipingo makubwa ya maendeleo inapata nafasi.
Well said mkuu, yani kwa aliyoniambia nimeona afadhali hata ya hapa tz.
Usiku anafanya kazi ya u bartender ili walau aweze kuongeza kipato chake kwenye $50 anazopata.
Kumiliki gari ethiopia ni kazi kodi zao ziko juu sana zaidi ya Tanzania.
 
Hata Tanzania tunaelekea huko huko, ajira za kumulika kwa tochi, chakula kitakuwa haba si mda mrefu maana kilimo si kipaumbele cha serikali hii,. Katiba mbovu imempa mtu mmoja mamlaka ya kufikir kwa niaba ya raia zaid ya million 45.
 
Well said mkuu, yani kwa aliyoniambia nimeona afadhali hata ya hapa tz.
Usiku anafanya kazi ya u bartender ili walau aweze kuongeza kipato chake kwenye $50 anazopata.
Kumiliki gari ethiopia ni kazi kodi zao ziko juu sana zaidi ya Tanzania.
Ninakumbuka Ufaranza miaka hiyo wnanchi walilalamika hakuna chakula, viongozi kwa dharau waliwaambia wakatengeneze keki wale. Mtu asiye na mkate unamtajia keki.

Walipimduliwa
 
Kuna aina mbili ya maendeleo; maendeleo ya watu na maendeleo ya vitu. Bahati mbaya sana wakazi wa dunia hii wanajua maendeleo ni yale tu ya vitu. Hata sisi binafsi tunawaza hivyo. Utasikia mtu anamsifu mtu fulani "fulani bwana ameendelea sana, ana magari kumi na nyumba tano". Huyo mtu katika ulimwengu wa leo anaonekana ni bora kuliko yule anayewasomesha ndugu zake kule kijijini. Falsafa hizo za kuwaendeleza watu wameondoka nazo akina Mwalimu Nyerere.
 
Well said mkuu, yani kwa aliyoniambia nimeona afadhali hata ya hapa tz.
Usiku anafanya kazi ya u bartender ili walau aweze kuongeza kipato chake kwenye $50 anazopata.
Kumiliki gari ethiopia ni kazi kodi zao ziko juu sana zaidi ya Tanzania.
Kodi kwenye magari ni hatari,ni kitu anasa sana kwao
 
Nchi za magharibi zlifuata mtindo huu zamani. Ni mapinduzi ya Ufaransa ndiyo yaliamsha watu. Viongozi walianza kuiangaliaw social benefits kama kishawishi kwa wapiga kura.

Kila kiongozi alikuja na manifesto ya elimu, afya, makazi, ajira na pesa za kujiku kwa wasio na kazi.

Raia wanaopata mahitaji muhimu hawana muda wa kuilalamikia serikali. Mipingo makubwa ya maendeleo inapata nafasi.
Ni kweli kabisa nchi nyingi za ulaya zimepitia mambo mabaya zaidi, kama kunyanyaswa wanawake, ajira/vibarua vigumu ujira mdogo, child labour ambayo haielezeki, wakati huo watawala wafalme na familia zao,au koo zao wanatukuzwa kama miungu, ILa baada ya miaaka mingi ya kupaza sauti na harakati za kupinga uonevu na unyanyasaji wa watawala leo hii nchi nyingi za ulaya Kuwa kiongozi wa kisiasa ni kujitolea zaidi maana hakuna maslahi makubwa kuliko wajiliwa wengine wa serikali, pia hata wala huwi mtu wa kuogopwa sana

ila sisi badala ya kujifunya mema tunataka tupitia huko walipopita wao, wanasiasa wetu wajiona wao ndio first class citizen hapa nchini, wanalipana mishahara na maposho makubwa hata maprof, mainjinia, ma dr hawaoni ndani, ndio maaana watalamu wote tz wanataka kuwa wanasiasa kupata easy money maaana wanasiasa hamna kitu wanafanya pale dodoma mjengoni, zaidi ya kupiga umbea tu......

Nchi yetu wanasiasa (wabunge,mawaziri, wateule wa raisi dc,rc,ma ceo uchwara maana tasisi zetu ziko hoi kwa rushwa na ineffeciency. Makatibu wakuu, mabalozi na nk) mishahara yao pamoja na posho nizaidi ya 50% ya wage bill yote ya watumishi wa umma (yaaani hela zetu za kodi zinawahudumia hawa tu kwa kiasi kikubwa)
 
14 Reactions
Reply
Back
Top Bottom