Leo nimeona mwenyewe usumbufu wa polisi wa usalama barabarani dhidi ya magari ya mizigo

Gulwa

JF-Expert Member
Jun 16, 2008
9,732
14,741
Nilichukua gari kwenda kupokea mzigo wangu kutoka mkoani pale Mbezi Kibada cha mkaa.

Wakati tunaenda tulipiti njia ya wazo hili na kutokea barabara ya Goba. Njiani nilisimamishwa na maaskari mara tatu, kila mala wakimwambia dereva wanataka kukagua lesseni yake. Kumbe hiyo ni lugha ya kutaka pesa na dereva wangu alikuwa akiambatanisha lesseni na shs 2000.

Polisi baada ya kupokea hela walirudisha leseni tukaendelea na safari. Ilifika mahali nikawajia juu askari na kuwaambia kuwa usumbufu wao unachanguankuua biashara.

Askari mmoja mkurya ana mvi alinitishia ila sikutishika.

Baada ya kupakia mzigo tukapitia njia ile ile. Kuingia tu barabara ya goba tukasimamishwa, baada ya kilometa kama mbili tukawakuta tena askari wawili wa kike wana gari hurrier pembeni nao wakikusanya pesa nk.

Nachotaka kusema ni kuwa usumbufu wanaopata wafanyabishara jijini kutoka kwa askari hawa unachangia kuongeza ugumu wa maisha kwani usafirishaji bidhaa unakuwa juu sana kutokana rushwa ya polisi, na mzigo mwishoni utamuangukia mlaji wa mwisho.

Nimeambiwa kuwa mchezo huu ni rasmi ndani ya Jeshi la Polisi na kila Askari analazimika kupeleka mga kwa wakubwa zake hadi unamfikia mkubwa kabisa.

TAKUKURU wanajua, usalama wa taifa wanajua na Rais analijua. Je, inawezekana kwa kuwa traffic wamegeuka TRA hayo ndiyo malipo yao?
 
bila kutoa hizo buku buku madereva watakufa njaa, asilimia kubwa ya mizigo wanayobeba Ni ya dili wanafanya hivyo ili wasikaguliwe.
Wewe sio dereva wa Lori huwezi jua hizo harakati.
Ndugu, uwe na gari mpya, mzigo halali utasumbuliwa kama kawaida, usipotoa utabambikwa adhabu hadi biashara utaiona chungu.

Wenye gari za abiria mfano hiace ni balaa, barabarani ya kilomita kadhaa wenye gari ya kubeba abiria 14 anatoa 3000 na abiria 18 anatoa 5000 kila kituo, na vituo vinakuwa vingi hatari.

Kama mapato yako kwenda na kurudi ni 100,000 mwenye gari atajikuta anabaki na 40,000 ukitoa mafuta, posho ya dreva zingine watachukua polisi
 
Bila kutoa hizo buku buku madereva watakufa njaa, asilimia kubwa ya mizigo wanayobeba Ni ya dili wanafanya hivyo ili wasikaguliwe.
Wewe sio dereva wa Lori huwezi jua hizo harakati.
Sio mizigo ya dili kwani kazi ya traffic ni kukagua mizigo au magari
 
Hili jambo ni kwa vyombo vya moto vyote, viwe vidogo au vikubwa, na ni nchi nzima.

Kuna siku nilikuwa na ruti za kutosha ikanibidi nichenji noti za elfu kumi mbili, niwe na elfu moja moja tupu, nilianza tripu saa 11 asubuhi na kabla haijafika saa 6 mchana nikawa nimeishiwa japo niliwapa buku kila kituo.

Wana mbinu moja chafu sana, anaomba leseni akague kisha anabaki nayo, anakuchukulia muda akiwa amekupaki pembeni, usipotoa anaendelea kusimamisha magari mengine hadi ulegee.

Kwa kuwa mamlaka zote zinaelewa kinachoendelea, nadhani bora wangeweka kiwango cha kulipa kwa siku kama ni halali, na unapolipa upewe utambulisho wa siku hiyo ili kuonyesha kwenye vituo vingine.

Asante mitano tena na ukomo tunaondoa, sisi ni Tanzania mpya
 
Yaani wasumbufu kama zote.
Mimi baada ya kutowapa pesa wakaandika faini eti tairi mbovu hali zina mwezi.
Nimewaambia silipi mpaka niwaone wakubwa zake ofisini
 
Sasa mbona hamna sehem uliyoombwa rushwa kwenye maelezo yako? Kama kaomba lesen mpe lesen alaf kauka anahaki ya kukagua ila hana haki ya kuomba rushwa.

Kwahiyo hapo kosa ni la Dereva wako alietoa rushwa bila kuombwa
 
kwamba alikutisha ila hukutishika!!!

si ungeamuru kutotoa hizo hela sasa,mambo ya barabarani madereva na traffic ndio wanaelewana,wewe boss ukitaka kuyaingilia utaharibu.
 
Yaani wasumbufu kama zote.
Mimi baada ya kutowapa pesa wakaandika faini eti tairi mbovu hali zina mwezi.
Nimewaambia silipi mpaka niwaone wakubwa zake ofisini
Hasira hasara! Umekaataa kutoa buku mbili,Sasa unaenda kutoa tembo wa tatu!! Sasa hapo imekula kwa nani!?

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Hawa si ndiyo waliopata ile ruksa kubwa ya kukusanya zile za kupigia brashi?

Na bado!
 
Ni maeneo GANI na je. Labda ulinakili namba za gari? Harrier new model/old?
 
Hawa si ndiyo waliopata ile ruksa kubwa ya kukusanya zile za kupigia brashi?

Na bado!
Bora utowe za kubrashia viatu, maana Magari ya wabongo mengi ni Vimeo yakikaguliwa huwezi kosa Makosa kibao! Kwa hiyo Askari wetu wa barabarani wanahuruma sana,we unazani wakiamua kukomaa kuangalia mapungufu ya chombo chako Cha Moto nani atabaki road!?

Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
 
Bila kutoa hizo buku buku madereva watakufa njaa, asilimia kubwa ya mizigo wanayobeba Ni ya dili wanafanya hivyo ili wasikaguliwe.
Wewe sio dereva wa Lori huwezi jua hizo harakati.
Si kweli kua mizigo hiyo ni ya dili huwa ni mizigo halali kabisa.shida ni hao hao wazee maana hiyo ndio ishakua fursa yao
hata gari ikiwa empty bado utasumbuliwa tu
 
Nilichukua gari kwenda kupokea mzigo wangu kutoka mkoani pale Mbezi Kibada cha mkaa.

Wakati tunaenda tulipiti njia ya wazo hili na kutokea barabara ya Goba. Njiani nilisimamishwa na maaskari mara tatu, kila mala wakimwambia dereva wanataka kukagua lesseni yake. Kumbe hiyo ni lugha ya kutaka pesa na dereva wangu alikuwa akiambatanisha lesseni na shs 2000.

Polisi baada ya kupokea hela walirudisha leseni tukaendelea na safari. Ilifika mahali nikawajia juu askari na kuwaambia kuwa usumbufu wao unachanguankuua biashara.

Askari mmoja mkurya ana mvi alinitishia ila sikutishika.

Baada ya kupakia mzigo tukapitia njia ile ile. Kuingia tu barabara ya goba tukasimamishwa, baada ya kilometa kama mbili tukawakuta tena askari wawili wa kike wana gari hurrier pembeni nao wakikusanya pesa nk.

Nachotaka kusema ni kuwa usumbufu wanaopata wafanyabishara jijini kutoka kwa askari hawa unachangia kuongeza ugumu wa maisha kwani usafirishaji bidhaa unakuwa juu sana kutokana rushwa ya polisi, na mzigo mwishoni utamuangukia mlaji wa mwisho.

Nimeambiwa kuwa mchezo huu ni rasmi ndani ya Jeshi la Polisi na kila Askari analazimika kupeleka mga kwa wakubwa zake hadi unamfikia mkubwa kabisa.

TAKUKURU wanajua, usalama wa taifa wanajua na Rais analijua. Je, inawezekana kwa kuwa traffic wamegeuka TRA hayo ndiyo malipo yao?
Rais wa Wanyonge alishawapa kichwa kwa kusema wazi kwamba trafiki kuomba hela ya ku brashi viatu si rushwa.

Yeye ndiye aliyewapa ruhusa.

Sasa ruhusa washapewa na rais, unataka wailazie damu?

Tatizo hili kalilea na kulifuga Magufuli.
 
16 Reactions
Reply
Back
Top Bottom