Leo nimemkumbuka mwanamuziki Kikumbi Mwanza Mpango, King Kikii, aliposema "Tushike ya kwetu, tusiwape muda karagosi", karagosi ni nani?

Tushike ya kwetu...yapi?kutatua changamoto zetu,kujenga nchi,tujenge mshikamano na umoja wetu watanzania na tuwe wazalendo hakika kuitetea nchi yetu dhidi ya kikundi fulani(MAKARAGOSI),chenye kujali maslahi yao(kubaki madarakani), bila kujali mahangaiko ya watanzania.Karagosi anatumia kila njia chafu kubaki madarakani kujinufaisha.

Je basi,KARAGOSI ni nani?...................
 
Mtunzi wa wimbo huo wala hakua na maana unayoitaka mkuu.

Na kama una lengo la kumbeza au kumtweza au kumkejeli mgombea fulani, basi unapoteza muda wako.

Kila mtu kwa nafasi yake anatambua anataka nini katika uchuguzi huu, kwa jasho na damu, kura zitakwenda kuamua hatma ya nchi kwa mara ya kwanza. Kinyume na hapo ..............
Kapige kura kwa JPM wewe acha ujinga na Karagosi wenu,aliye badirisha nchi kwa kiwango cha 85% tunamuachaje then tumpe mwenye kuonyesha uchu wa madaraka,yaani issue kwake siyo wananchi ni Ikulu,tena katoka kwenye makubaliano na whites huko nje,we unajua kakubaiana nao nini?mtu gani kuongea kwake muda wote ni mahasira tu dhidi ya wengine,hapa alitakiwa kunadi sera imara za kutufanyia sisi kama wananchi,lakini yeye kutwa kucha ni hasira dhidi ya JPM,hatuna shida na hasira zake sisi,sisi tuna shida na mambo mengi ambayo huyo huyo anaye mkasirikia tunamuona anatutendea

Hebu piteni hivi mtupishe bana

Angalizo-: Mimi sina chama chochote maana najua wale ni watu wanapambania maisha yao tu,wapate kazi walee koo zao isipokua mimi pia najua uhalisia wa nani anaweza kuliko mwingine
 
Huyo Muandishi njaa tangu hii siku alishika adabu yake akaamua kua mlamba viatu
Mtunzi wa wimbo huo wala hakua na maana unayoitaka mkuu.

Na kama una lengo la kumbeza au kumtweza au kumkejeli mgombea fulani, basi unapoteza muda wako.

Kila mtu kwa nafasi yake anatambua anataka nini katika uchuguzi huu, kwa jasho na damu, kura zitakwenda kuamua hatma ya nchi kwa mara ya kwanza. Kinyume na hapo ..............
 
KIKARAGOSI ni wewe Pascal Mayalla na VIKARAGOSI wenzio wengi tu. Na ushahidi wa wewe kuwa KIKARAGOSI huu hapa.
Elections 2015 - If you can't beat them, join them! He is the worst dictator. Let's pray for him!

https://www.jamiiforums.com/threads...-ni-zamu-ya-media-ina-suffer.1518514/Wanabodi,
leo nikiwa natoka mahali kwa kutumia public transport, ukapigwa wimbo wa King Kikii, kitambaa cheupe, hivyo from no where, nimetokea kumkumbuka mwanamuziki mkongwe huyu, jina kamili ni Kikumbi Mwanza Mpango, aka King Kikii, kumbe pia alikuwa na vibwagizo fulani vya kisiasa vya kiaina.

Kwenye wimbo huo, kuna versi aliimba
"Bongo ina mambo mengi mama eeh
Kila kukuchapo kuna mambo mapya,
Tuyazingatie ya kwetu,
Wala tusiwape muda Karagosi".

Karibu msikilize


Verse hiyo imenifikirisha sana, haswa kwenye muktadha wa uchaguzi mkuu wetu kwa upande wa urais.

Japo kikaragosi kwa kizungu ni cartoon, caricature, marionette, jee hapa kwenye neno Karagosi, King Kikii alimaanisha nini?.
Nani ni Karagosi au karagosi ni nani?.

Paskali
 
Hivi viji kumbukumbu hivi vya kuwakumbuka watu, vinasaidia sana, hebu angalia baada ya kumbukumbu hii, nini kimefuatia

Mhesh Kassimu Majaliwa amemtembea nguli huyo wa muziki Nchini almaarufu Mzee wa Kitambaa Cheupe Nyumbani kwake leo.
Duh, nilimkumbuka King Kikii na wimbo wake wa kitambaa cheupe hivi karibuni
Get Well Soon King Kikii
P
 
Back
Top Bottom