Rais Yowel Kaguta Museveni leo anatimiza miaka 23 madarakani baada ya kuipindua serikali ya kijeshi ya Major jenerali Tito Okello Mnamo January 26,1986. Museveni ameonyesha kila dalili ya kwamba hawezi kuachia madaraka ya kuitawala Uganda hivi karibuni kwani ameshaanza kupiga chapuo za kusimama katika uchaguzi ujao kama mgombea wa NRM.
Hali hii ni sawa na wingi jeusi linaloifunika jumuia ya afrika mashariki. Bwana M7 moja ya mambo anayoyawazia ni yeye kuwa rais wa kwanza wa shirikisho la afrika mashariki. Binamu yake Kagame naye anapiga chepuo za kujisimika zaidi na kuifanya Rwanda iwe imaya yake binafsi.
Kwa mtizamo huu wa hawa ndugu wawili ambao kwao utawala wa sheria ni ule unaoashiria kusimama kwa tawala zao. Je Tanzania tutayaweza ya jamaa zetu hawa. Kumbuka tuna amani japo napo siku hizi ishaanza kuingia 'kwikwi', tuna ardhi kubwa tu ( kumbuka nchi zote zilizobaki za jumuia ya A/mashariki zinamatatizo ya ardhi)?
Mwisho leo M7 anashereheka kutimiza hiyo miaka 23, Je watanzania tuna nini cha kujifunza kutokana na yeye pamoja na siasa za afrika mashariki? je shirikisho ndio njia pekee ya kuelekea kwenye kaanani yenye maziwa na asali au ndo kujiweka reahani?
Wakatabahu,
Shadow.
Hali hii ni sawa na wingi jeusi linaloifunika jumuia ya afrika mashariki. Bwana M7 moja ya mambo anayoyawazia ni yeye kuwa rais wa kwanza wa shirikisho la afrika mashariki. Binamu yake Kagame naye anapiga chepuo za kujisimika zaidi na kuifanya Rwanda iwe imaya yake binafsi.
Kwa mtizamo huu wa hawa ndugu wawili ambao kwao utawala wa sheria ni ule unaoashiria kusimama kwa tawala zao. Je Tanzania tutayaweza ya jamaa zetu hawa. Kumbuka tuna amani japo napo siku hizi ishaanza kuingia 'kwikwi', tuna ardhi kubwa tu ( kumbuka nchi zote zilizobaki za jumuia ya A/mashariki zinamatatizo ya ardhi)?
Mwisho leo M7 anashereheka kutimiza hiyo miaka 23, Je watanzania tuna nini cha kujifunza kutokana na yeye pamoja na siasa za afrika mashariki? je shirikisho ndio njia pekee ya kuelekea kwenye kaanani yenye maziwa na asali au ndo kujiweka reahani?
Wakatabahu,
Shadow.