Leo naomba nimtetee mheshimiwa raisi wangu ndugu J M Kikwete

Naomba nielezee kwa vipengele ulivyochambua
  • Ni kweli Kenya imejengwa sana na wakoloni na rwanda ni nchi ndogo lakini kwa miaka hamsini ya utawala wa ccm yalitakiwa yawepo mabadiliko,kwanza uchache wa watu katika nchi sio sababu ya kuwa tajiri kumbuka china ina watu karibu bilioni moja na inaendelea kwa kwasi,burundi nayo ni nchi ndogo lakini bado maskini wa kutupa,TATIZO LA KIKWETE HANA VISION HAJUI HAFANYE NINI NDIO MAANA ANAKUWA MZIGO KWETU WA TZ,hao kwenye na rwanda hawana rasilimali tulizonazo sisi ,achana na madini yanayohitaji technolojia kuchibwa hata watu pia ni rasilimali serikali imeshindwa kutumia kuongeza pato la nnchi,kikwete hajui anachofanya NDIO MAANA ALIULIZWA KWA NINI NCHI YAKO MASIKINI AKAJIBU SIJUI,
  • KUHUSU KUTEUA RAFIKI ZAKE,ameteua rafiki zake sio kwa kuwa ana waamini na anajua watatimiza malengo HAPANA KAFANYA HIVYO KULIPA FADHILA YA WALIYOMFANYIA KUMSAIDIA KUINGIA IKULU,KWA HIYO WAMEPEWA VYEO KAMA MSHAHARA WAJILIPE KILE WALICHOPOTEZA KWA SABABU YAKE NDIO MAANA PESA NYINGI YA SERIKALI IMEPOTEA mambo ya richmond na epa.
  • pia kikwete hawezi kuwachukulia hatua kwa sababu naye ni mmoja wapo ya mambo machafu yanayofanyika namnukuu lowasa akisema katika kikao cha nec ya ccm "WATU WANANISHAMBULIA KWA KUNIITA FISADI LAKINI UNAKUMBUKA WAKATI HII KAMPUNI YA RICHMOND INAINGIA NILITAKA KUIKATAA ULIVYOWASILIANA NA WEWE UKASEMA UMEPATA TAARIFA KWA MAKATIBU WAKUU KUWA HAINA TATIZO IENDELEE NA KAZI" kwa hali kama hiyo kikwete akichelewa kufanya maamuzi utasema anapima faida na hasara?
  • Rais kusafiri ,watu sio kwamba wanataka rais asisafiri tatizo ni safari za mara kwa mara na rais huwa anasafiri na msafara kiasi kwamba yanatumika mabilioni ya fedha,kuna mengine ambayo unakuta hata angeenda waziri ingetosha ambaye garama zake za usafiri ni chache kulingana na rais,ni kweli technolojia yetu ndogo lakini kuna mawaziri wengi wanaweza kuliwakilisha taifa,HATUTEGEMEI RAIS AENDE MAREKANI ALAFU AKAPIGE PICHA NA 50CENT au kwenda kuomba kikampuni fulani cha IT kije kiwekeze TZ wakati ni vitu vizuri lakini hata balozi angevifanya achana na wakurugenzi,makatibu wakuu au mawaziri

sijaongelea idadi ya watu (population) bali nliongelea eneo la kijografia (territory) ya nchi husika.
Yote Kikwete anayofanya yupo sahihi (sio makosa) katiba ina mruhusu, je unadhan kuna ulazima kwenye katiba mpya tuweke ni safar zipi raisi anatakiwa kusafir kwa mwaka na nyingine awaachie mawaziri?
Na je unadhan kuwa raisi anaweza kuteua wasaidizi wake bila kuwalipa wadhila wale jamaa zake wa karibu? Kama unaamin ni kivipi? Na vp anaweza kukacha kulipa fadhila?
Na unadhan tatizo ni JK au ni mfumo wetu wa kiuongozi?
 
Kama huyu mtoa maada ni msomi wa hiyo taaluma na unashindwa kutafsiri mambo, kweli leo ndo nimethibitisha kuwa ni kweli Elimu yetu imeshuka!

Napata utata sana kama kweli huyu anachukua Degree, bado siamini kabisa!
 
Nimejaribu kurudia kusoma mara2 kuelewa mwandishi alidhamiria nn, nimegundua mtoa thread mwanzoni mwa uzi alitanabaisha kuwa yuko tayari kumtetea rais wake. Na kwa msingi huo jamaa akajipanga kulinda maslahi ya JK...

Natofautina nae kudai kwamba Rwanda imepiga hatua eti kwa sababu ya eneo dogo kijografia hii si kweli, Rwanda iko hivyo ilivyo kutokana usimamizi mzuri wa rasilimali unaoambatana uwajibikaji usioruhusu ufisadi.. Tanzania ni kubwa lakini ukubwa wake isiwe kigezo cha kupiga hatua kimaendeleo, kwa sababu kila eneo lina wasimamizi wa shughuli za maendeleo lakini pia walinzi wa rasilimali,,kwa ustawi wa taifa.

Vp kama kanda ya ziwa ingekuwa nchi unadhan ingekuwa maskini kama ilivyo sasa?
Vp kama Pwani nayo ingekuwa nchi?
Tanzania mikoa inagawana umaskini na utajiri wake, pili ni vigumu kwa central government kucontrol the whole state, wasimamizi wa local government si sawa na wa central government, maendeleo ya nchi kiujumla unategemea usimamizi na umakini wa central government na sio local government.
 
sijaongelea idadi ya watu (population) bali nliongelea eneo la kijografia (territory) ya nchi husika.
Yote Kikwete anayofanya yupo sahihi (sio makosa) katiba ina mruhusu, je unadhan kuna ulazima kwenye katiba mpya tuweke ni safar zipi raisi anatakiwa kusafir kwa mwaka na nyingine awaachie mawaziri?
Na je unadhan kuwa raisi anaweza kuteua wasaidizi wake bila kuwalipa wadhila wale jamaa zake wa karibu? Kama unaamin ni kivipi? Na vp anaweza kukacha kulipa fadhila?
Na unadhan tatizo ni JK au ni mfumo wetu wa kiuongozi?
Nashukuru kwa kueleza JINSI KATIBA YETU ILIVO MBOVU,sikatai rais asisafiri,anatakiwa asafiri lakini kwa vitu kweli vinamuhitaji rais kama kuhuzuria mikutano ya jumuiya za madola,UN na mambo ambayo kweli mkuu wa nchi hizi warsha zinazofanyika ugaibuni za mambo ya nishati,kilimo ,tabia nchi awaachie mawaziri,wakurugenzi na makatibu wa kuu,hata vifursa vya biashara vidogo vidogo ni aibu raisi kwenda marekani eti ili apige picha na 50cent au rihhana,sio vibaya kupiga nao picha lakini mkuu wa nchi hiyo spare time umetoa wapi?
 
Wewe kama unajiita msomi wa Political Science, ni bora uende kijijini ukachunge kuku. Kwa kuwa tuna uhuru wa kutoa maoni, basi unahaki ya kufanya hivyo. Nasikitika kuwa kwa makusudi na ama kwa sababu fulani unajifanya kumtazama Kikwete kwa jicho la makengeza. Uchaguzi wa mwaka 2005, Kikwete alipata 81% ya kura zote zilizopigwa. Uchaguzi Mkuu wa mwaka juzi kapata 62% baada ya kudaiwa kuchakachua. Je, kushuka huko kwa kura kunaonyesha nini kama si imani ya wananchi dhidi yake kushuka? Kwa nini? majibu ni mengi, rushwa, ufisadi, kubebana na kutochukua hatua sahihi kwa muda sahihi. Hizo ziara zake nje ya nchi zinaligharimu taifa mabilioni mangapi ukilinganisha na matokeo ya ziara hizo?<br><br>Mikataba mingapi ambayo haina maslahi kwa taifa bali maslahi binafsi ya watu wachache? kuleta hao unaowaita wanateknolojia kubwa na kufunga nao mikataba inayowanufaisha wao binafsi na wale wanaosaini nao mkataba kwa niaba yetu kuna faida gani?<br><br>Kumpa mtu nafasi ya uongozi wakati alikusaidia kufika hapo ulipo badala ya kufuata sifa za mtu kwa nafasi husika kunalipeleka wapi taifa kama si kuliangamiza kabisa? Mtu aliyekusaidia kufikia malengo yako unaweza kuwa na ubavu wa kumkoromea akiteleza? Hajioni kuwa na yeye anaubia katika nafasi uliyo nayo?. Nchi yetu si masikini na wala si changa. Mnaojiita wasomi na mna mawazo ya aina hii, basi taifa hili liko uchi. Nchi inakila aina ya raslimali, utasemaje ni maskini? viongozi tulio nao akiwemo huyo unayemtetea wamejaa ubabaishaji, usanii, ubinafsi, si makini, si wazalendo wala waadirifu. wanawaza mambo yao, nyumba zao ndogo na marafiki zao. Hakuna anayewaza juu ya watanzania wa leo na kesho ndiyo maana mauzauza ni mengi. Unayejaribu kumtetea ameshashindwa, na wewe mtetezi wake ushindwe na ulegee.
 
Jamani huyu msomi "uchwara" kama anavyojipambanua mwacheni akae na mindset mbovu hadi atakapong'amua! Huwezi ukawa na akili timamu ukapoteza muda kuandika hii mada! It's the problem of having poor vision and lack reasoning! Naungana na waliosema kuwa "elimu unayosoma haitakusaidia kama haya ni mawazo yako, badili fani please".
 
Ingekuwa bora kama ungemuacha rais akijitetea mwenyewe au wale wanaolipwa kufanya kazi hiyo. Kimsingi rais wetu anahitaji msaada wa ushauri nasaha hasa kuhusiana na waliomzunguka wakimshauri vibaya.
 
Kwanza kabisa naomba niseme kama wewe unadhani utachangia hizi hoja zangu kwa matusi ni bora ukasoma tu na kupotezea, natamani kuona wale wote watakao changia hapa wachangie kwa lengo la kujenga na sio kujionesha bora zaidi ya wengine. Nikiwa kama mtanzania wa kawaida nisiyeamini katika chama chochote kile cha siasa katika hii dunia lakin mfuatiliaji mzuri wa masuala ya siasa za dunia (nadhan ni kwa vile nasoma POLITICAL SCIENCE AND PUBLIC ADMINISTRATION (BA PSPA)) nimeguswa kidogo leo walau kumtetea raisi Kikwete japo mi sio msaidizi wake wala sio mfuasi wake ila kama mtanzania nliye chini ya utawala wake naamini nina haki 100% kumtetea raisi wangu kwa nguvu zangu zote.
Katika mitandao mbalimbali na hata hapa JF raisi Kikwete amekuwa akipewa lawama kibao mfano juu ya ufisadi, umaskini wa mtanzania, kushuka kwa uchumi, kuwa mzito wa kutoa maamuzi n.k naamini hizi lawama zote JK anazifahamu ila aidha kwa kuzipuuzia, au kwa kuwaacha watu waongee tu watakavyo coz kuna uhuru wa kuongea am eamua kukaa kimya. Binafsi naomba nitoe ufafanuzi kidogo wa baadhi ya lawama kwa mh. raisi.

1) Tanzania tupo nyuma kimaendeleo tukijilinganisha na jirani zetu. Hii ni kweli sisi tupo nyuma kimaendeleo ukitulinganisha na nchi kama Kenya na Rwanda, lakin hii sio kwa sababu ya JK, kihistoria Kenya ilikuwa kolononi la kilowezi yaani ni kwamba wazungu walikaa/kuishi Kenya na kujenga miundombinu na huduma za kijamii mfano hospitali, shule n.k, pia walianzisha mashamba makubwa pia kwa kuwa Muingereza ndiye aliyekuwa mtawala wa nchi nyingi za Afrika mashariki, aliifanya Kenya kama makao makuu yake, kwa sababu hii Muingereza aliweza kuijenga Kenya zaidi kuliko koloni lolote lile ndani ya Afrika Mashariki ndo maana leo Kenya ipo juu zaidi ya nchi zote za Afrika Mashariki.
Kwa upande wa Rwanda, naamini wote mnatambua kuwa Rwanda kijografia ni nchi ndogo sana kwa kuilinganisha na Tanzania kitu ambacho kinawasaidia wanyarwanda kusimamia shughuli za kimaendeleo na mali asili zao kikamilifu zaidi.

2) Kuwateua rafiki zake kuwa wasaidizi wake wakuu katika uongozi wake. wengi wanaamini kuwa kosa kubwa alilofanya JK ni kuwateua rafiki zake kuwa wasaidizi wake kitu ambacho kinamsababisha kushindwa kuwachukulia hatua za kinidhamu pindi wanapofanya makosa, Binafsi naamini kuwa JK hakufanya kosa kuwateua rafiki zake kwa sababu kiongozi yeyote yule huteua wasaidizi ambao kwa 100% anaamini kuwa watamsaidia katika uongozi wake, hakuna raisi anayeteua watu asioamini kama watamsaidia kutimiza lengo lake, naamin hata siku mimi nikiwa raisi siwezi kukuteua wewe nisiyekufaamu wala kuamini kama kweli utanisaidia katika uongozi wangu. Kuhusu kutokuwachukulia hatua hawa wasaidizi wake naielezea hapa kwa chini.

3) Kuchelewa kufanya maamuzi au kushindwa kabisa kufanya maamuzi. Inasemekana kuwa na huu ni udhaifu wa JK, kwanza naomba niseme kuwa mtu kuwa raisi ni tofauti na mtu kuwa baba au mwenyekiti wa taasisi fulani, sifa kubwa ya mfanya maamuzi ni kupima faida na hasara za maauzi atakayofanya katika jamii husika na kama maauzi hayo yana faida kubwa kwa jamii yambidi ayafanye na kama hayana faida kubwa kwa jamii sio lazima/haitakiwi kuyafanya hayo maamuzi. Hapa naomba niwakumbushe tu kuwa JK ni raisi na mwenyekiti wa CCM ivyo basi katika maamuzi yake ni lazima yawe na faida kote kote kwa CCM na kwa serikali, maamuzi yeyote kwa serikali yasiyo na faida kwa chama hayatakiwi, hii sio kwa CCM tu bali hata wewe chama chako kikiingia madarakani kitafanya hivi, na kwa sababu hii ndio maana anashindwa kuwachukulia hatuna wasaidizi wake wa karibu haswa haswa mawaziri kwa lengo la kukilinda chama kisisambaratike.

4) Kusafiri nchi za nje na kuomba misaada. Naamini hata kama Obama ndo angekuwa raisi wetu naye angekuwa anasafiri kama JK anavyosafiri, watanzania wenzangu, japokuwa tuna rasilimali nyingi sana hapa kwetu tatizo ni kwamba hatuwezi kuzitumia hizo rasilimali sisi wenyewe, mbali na kuzitumia hata namna ya kuzivuna hatujui kwa sababu teknolojia yetu ni ya chini saaaana, hivyo ili walau tufaidi kidogo hizi rasilimali zetu tutahitaji kuwaomba wenye ujuzi na teknolojia yao waje watunyonye kidogo, hali hii haisababishwi na JK bali ni kwa sababu ya mfumo tulioachiwa na wakoloni (ukoloni mamboleo)

kwa udogo na uchache ndo hayo tu kwa leo.

mi mapita tuuu
 
Back
Top Bottom