Dijovisonjn
JF-Expert Member
- Nov 14, 2011
- 466
- 125
Kwanza kabisa naomba niseme kama wewe unadhani utachangia hizi hoja zangu kwa matusi ni bora ukasoma tu na kupotezea, natamani kuona wale wote watakao changia hapa wachangie kwa lengo la kujenga na sio kujionesha bora zaidi ya wengine. Nikiwa kama mtanzania wa kawaida nisiyeamini katika chama chochote kile cha siasa katika hii dunia lakin mfuatiliaji mzuri wa masuala ya siasa za dunia (nadhan ni kwa vile nasoma POLITICAL SCIENCE AND PUBLIC ADMINISTRATION (BA PSPA)) nimeguswa kidogo leo walau kumtetea raisi Kikwete japo mi sio msaidizi wake wala sio mfuasi wake ila kama mtanzania nliye chini ya utawala wake naamini nina haki 100% kumtetea raisi wangu kwa nguvu zangu zote.
Katika mitandao mbalimbali na hata hapa JF raisi Kikwete amekuwa akipewa lawama kibao mfano juu ya ufisadi, umaskini wa mtanzania, kushuka kwa uchumi, kuwa mzito wa kutoa maamuzi n.k naamini hizi lawama zote JK anazifahamu ila aidha kwa kuzipuuzia, au kwa kuwaacha watu waongee tu watakavyo coz kuna uhuru wa kuongea am eamua kukaa kimya. Binafsi naomba nitoe ufafanuzi kidogo wa baadhi ya lawama kwa mh. raisi.
1) Tanzania tupo nyuma kimaendeleo tukijilinganisha na jirani zetu. Hii ni kweli sisi tupo nyuma kimaendeleo ukitulinganisha na nchi kama Kenya na Rwanda, lakin hii sio kwa sababu ya JK, kihistoria Kenya ilikuwa kolononi la kilowezi yaani ni kwamba wazungu walikaa/kuishi Kenya na kujenga miundombinu na huduma za kijamii mfano hospitali, shule n.k, pia walianzisha mashamba makubwa pia kwa kuwa Muingereza ndiye aliyekuwa mtawala wa nchi nyingi za Afrika mashariki, aliifanya Kenya kama makao makuu yake, kwa sababu hii Muingereza aliweza kuijenga Kenya zaidi kuliko koloni lolote lile ndani ya Afrika Mashariki ndo maana leo Kenya ipo juu zaidi ya nchi zote za Afrika Mashariki.
Kwa upande wa Rwanda, naamini wote mnatambua kuwa Rwanda kijografia ni nchi ndogo sana kwa kuilinganisha na Tanzania kitu ambacho kinawasaidia wanyarwanda kusimamia shughuli za kimaendeleo na mali asili zao kikamilifu zaidi.
2) Kuwateua rafiki zake kuwa wasaidizi wake wakuu katika uongozi wake. wengi wanaamini kuwa kosa kubwa alilofanya JK ni kuwateua rafiki zake kuwa wasaidizi wake kitu ambacho kinamsababisha kushindwa kuwachukulia hatua za kinidhamu pindi wanapofanya makosa, Binafsi naamini kuwa JK hakufanya kosa kuwateua rafiki zake kwa sababu kiongozi yeyote yule huteua wasaidizi ambao kwa 100% anaamini kuwa watamsaidia katika uongozi wake, hakuna raisi anayeteua watu asioamini kama watamsaidia kutimiza lengo lake, naamin hata siku mimi nikiwa raisi siwezi kukuteua wewe nisiyekufaamu wala kuamini kama kweli utanisaidia katika uongozi wangu. Kuhusu kutokuwachukulia hatua hawa wasaidizi wake naielezea hapa kwa chini.
3) Kuchelewa kufanya maamuzi au kushindwa kabisa kufanya maamuzi. Inasemekana kuwa na huu ni udhaifu wa JK, kwanza naomba niseme kuwa mtu kuwa raisi ni tofauti na mtu kuwa baba au mwenyekiti wa taasisi fulani, sifa kubwa ya mfanya maamuzi ni kupima faida na hasara za maauzi atakayofanya katika jamii husika na kama maauzi hayo yana faida kubwa kwa jamii yambidi ayafanye na kama hayana faida kubwa kwa jamii sio lazima/haitakiwi kuyafanya hayo maamuzi. Hapa naomba niwakumbushe tu kuwa JK ni raisi na mwenyekiti wa CCM ivyo basi katika maamuzi yake ni lazima yawe na faida kote kote kwa CCM na kwa serikali, maamuzi yeyote kwa serikali yasiyo na faida kwa chama hayatakiwi, hii sio kwa CCM tu bali hata wewe chama chako kikiingia madarakani kitafanya hivi, na kwa sababu hii ndio maana anashindwa kuwachukulia hatuna wasaidizi wake wa karibu haswa haswa mawaziri kwa lengo la kukilinda chama kisisambaratike.
4) Kusafiri nchi za nje na kuomba misaada. Naamini hata kama Obama ndo angekuwa raisi wetu naye angekuwa anasafiri kama JK anavyosafiri, watanzania wenzangu, japokuwa tuna rasilimali nyingi sana hapa kwetu tatizo ni kwamba hatuwezi kuzitumia hizo rasilimali sisi wenyewe, mbali na kuzitumia hata namna ya kuzivuna hatujui kwa sababu teknolojia yetu ni ya chini saaaana, hivyo ili walau tufaidi kidogo hizi rasilimali zetu tutahitaji kuwaomba wenye ujuzi na teknolojia yao waje watunyonye kidogo, hali hii haisababishwi na JK bali ni kwa sababu ya mfumo tulioachiwa na wakoloni (ukoloni mamboleo)
kwa udogo na uchache ndo hayo tu kwa leo.
Katika mitandao mbalimbali na hata hapa JF raisi Kikwete amekuwa akipewa lawama kibao mfano juu ya ufisadi, umaskini wa mtanzania, kushuka kwa uchumi, kuwa mzito wa kutoa maamuzi n.k naamini hizi lawama zote JK anazifahamu ila aidha kwa kuzipuuzia, au kwa kuwaacha watu waongee tu watakavyo coz kuna uhuru wa kuongea am eamua kukaa kimya. Binafsi naomba nitoe ufafanuzi kidogo wa baadhi ya lawama kwa mh. raisi.
1) Tanzania tupo nyuma kimaendeleo tukijilinganisha na jirani zetu. Hii ni kweli sisi tupo nyuma kimaendeleo ukitulinganisha na nchi kama Kenya na Rwanda, lakin hii sio kwa sababu ya JK, kihistoria Kenya ilikuwa kolononi la kilowezi yaani ni kwamba wazungu walikaa/kuishi Kenya na kujenga miundombinu na huduma za kijamii mfano hospitali, shule n.k, pia walianzisha mashamba makubwa pia kwa kuwa Muingereza ndiye aliyekuwa mtawala wa nchi nyingi za Afrika mashariki, aliifanya Kenya kama makao makuu yake, kwa sababu hii Muingereza aliweza kuijenga Kenya zaidi kuliko koloni lolote lile ndani ya Afrika Mashariki ndo maana leo Kenya ipo juu zaidi ya nchi zote za Afrika Mashariki.
Kwa upande wa Rwanda, naamini wote mnatambua kuwa Rwanda kijografia ni nchi ndogo sana kwa kuilinganisha na Tanzania kitu ambacho kinawasaidia wanyarwanda kusimamia shughuli za kimaendeleo na mali asili zao kikamilifu zaidi.
2) Kuwateua rafiki zake kuwa wasaidizi wake wakuu katika uongozi wake. wengi wanaamini kuwa kosa kubwa alilofanya JK ni kuwateua rafiki zake kuwa wasaidizi wake kitu ambacho kinamsababisha kushindwa kuwachukulia hatua za kinidhamu pindi wanapofanya makosa, Binafsi naamini kuwa JK hakufanya kosa kuwateua rafiki zake kwa sababu kiongozi yeyote yule huteua wasaidizi ambao kwa 100% anaamini kuwa watamsaidia katika uongozi wake, hakuna raisi anayeteua watu asioamini kama watamsaidia kutimiza lengo lake, naamin hata siku mimi nikiwa raisi siwezi kukuteua wewe nisiyekufaamu wala kuamini kama kweli utanisaidia katika uongozi wangu. Kuhusu kutokuwachukulia hatua hawa wasaidizi wake naielezea hapa kwa chini.
3) Kuchelewa kufanya maamuzi au kushindwa kabisa kufanya maamuzi. Inasemekana kuwa na huu ni udhaifu wa JK, kwanza naomba niseme kuwa mtu kuwa raisi ni tofauti na mtu kuwa baba au mwenyekiti wa taasisi fulani, sifa kubwa ya mfanya maamuzi ni kupima faida na hasara za maauzi atakayofanya katika jamii husika na kama maauzi hayo yana faida kubwa kwa jamii yambidi ayafanye na kama hayana faida kubwa kwa jamii sio lazima/haitakiwi kuyafanya hayo maamuzi. Hapa naomba niwakumbushe tu kuwa JK ni raisi na mwenyekiti wa CCM ivyo basi katika maamuzi yake ni lazima yawe na faida kote kote kwa CCM na kwa serikali, maamuzi yeyote kwa serikali yasiyo na faida kwa chama hayatakiwi, hii sio kwa CCM tu bali hata wewe chama chako kikiingia madarakani kitafanya hivi, na kwa sababu hii ndio maana anashindwa kuwachukulia hatuna wasaidizi wake wa karibu haswa haswa mawaziri kwa lengo la kukilinda chama kisisambaratike.
4) Kusafiri nchi za nje na kuomba misaada. Naamini hata kama Obama ndo angekuwa raisi wetu naye angekuwa anasafiri kama JK anavyosafiri, watanzania wenzangu, japokuwa tuna rasilimali nyingi sana hapa kwetu tatizo ni kwamba hatuwezi kuzitumia hizo rasilimali sisi wenyewe, mbali na kuzitumia hata namna ya kuzivuna hatujui kwa sababu teknolojia yetu ni ya chini saaaana, hivyo ili walau tufaidi kidogo hizi rasilimali zetu tutahitaji kuwaomba wenye ujuzi na teknolojia yao waje watunyonye kidogo, hali hii haisababishwi na JK bali ni kwa sababu ya mfumo tulioachiwa na wakoloni (ukoloni mamboleo)
kwa udogo na uchache ndo hayo tu kwa leo.