Leo nafanya maombi maalumu kumuombea Rais Magufuli. Naomba mjumuike nami.

Keynez

JF-Expert Member
Feb 12, 2007
2,397
3,884
Tafadhali jumuikeni nami kuanzia saa 2:00 hadi 2:30 usiku huu wa leo kwa ajili ya kumuombea Rais Magufuli.

Maandiko yanasema wanapokusanyika wawili au zaidi Mungu atayapokea maombi hayo. Umbali siyo tatizo, kwenye mambo ya kiroho hakuna umbali.

Tumuombee afya njema, hekima, huruma, maarifa, roho ya kiasi na kuepuka hasira.

Najua wengi tuna maoni HASI kuhusu Rais Magufuli na serikali yake ila inabidi tukumbuke wote tuko kwenye boti moja. Ikizama tunazama wote na najua wengi wetu hata kuogelea hatujui.

Kuna njia halali za kumshinikiza Rais na serikali yake. Kwa mfano bado naamini maandamano ni njia sahihi na ambayo ingeweza kutumika ila kila Afande Mroto akitoa vitisho watu wanapoteana. Hilo siyo la kumlaumu Rais Magufuli ni woga wetu sisi wenyewe.

Kutumia njia za hila, blackmail na zingine za kiuhalifu ili Rais atimize matakwa ya kundi fulani siyo njia sahihi. Rais ana madaraka makubwa sana, anaweza kuamua kulianzisha hapa na hakuna atakayeweza kumzuia. Tuwe makini sana.

Nimekumbuka Mfalme Sauli alikuwa anamsakama Daudi kwa muda mrefu ili amuue ila Daudi pamoja na kwamba tayari alikuwa ameshapakwa mafuta na Nabii Samuel ya kuwa mfalme lakini hata alipopata nafasi mara kadhaa ya kummaliza Sauli kwa mikono yake mwenyewe hakufanya hivyo. Alimuachia hilo jukumu Mwenyezi Mungu mwenyewe.

Kumbuka ni kuanzia saa 2:00 hadi 2:30 usiku huu wa leo. Tafadhali usizembee na mtaarifu mwenzio.
 
Unaacha kuombea familia yako na ukoo wako, unakaa kumeombea JpM yuko zake huko hata hakufahamu, Na hata ukiomba hatajua. Ukichunguza utagundua ukoo wako unamatatizo na changamoto nyingi za kimaisha, Badala ya kutenga mda wa kutatua unafany amambo yaaaaaàbu
Tafadhali jumuikeni nami kuanzia saa 2:00 hadi 2:30 usiku huu wa leo kwa ajili ya kumuombea Rais Magufuli.

Maandiko yanasema wanapokusanyika wawili au zaidi Mungu atayapokea maombi hayo. Umbali siyo tatizo, kwenye mambo ya kiroho hakuna umbali.

Tumuombee afya njema, hekima, huruma, maarifa, roho ya kiasi na kuepuka hasira.

Najua wengi tuna maoni HASI kuhusu Rais Magufuli na serikali yake ila inabidi tukumbuke wote tuko kwenye boti moja. Ikizama tunazama wote na najua wengi wetu hata kuogelea hatujui.

Kuna njia halali za kumshinikiza Rais na serikali yake. Kwa mfano bado naamini maandamano ni njia sahihi na ambayo ingeweza kutumika ila kila Afande Mroto akitoa vitisho watu wanapoteana. Hilo siyo la kumlaumu Rais Magufuli ni woga wetu sisi wenyewe.

Kutumia njia za hila, blackmail na zingine za kiuhalifu ili Rais atimize matakwa ya kundi fulani siyo njia sahihi. Rais ana madaraka makubwa sana, anaweza kuamua kulianzisha hapa na hakuna atakayeweza kumzuia. Tuwe makini sana.

Nimekumbuka Mfalme Sauli alikuwa anamsakama Daudi kwa muda mrefu ili amuue ila Daudi pamoja na kwamba tayari alikuwa ameshapakwa mafuta na Nabii Samuel ya kuwa mfalme lakini hata alipopata nafasi mara kadhaa ya kummaliza Sauli kwa mikono yake mwenyewe hakufanya hivyo. Alimuachia hilo jukumu Mwenyezi Mungu mwenyewe.

Kumbuka ni kuanzia saa 2:00 hadi 2:30 usiku huu wa leo. Tafadhali usizembee na mtaarifu mwenzio.
 
Unaweza kukuta mama yako mzazi ni mgonjwa au wadogo zako shule ngumu.

Unaacha kuwaombea hao unamuombea mwenye ulinzi wake + uhakika wa kula yeye na vizazi vyake + uhakika wa kutibiwa bure hadi anakufa..

Inabidi uchunguzwe afya ya akili yako
 
Bila kujali itikadi, misimamo wala imani zetu baada ya lisaa limoja kutoka sasa acha lolote unalofanya tujumuike katika maombi haya.

Nikipata mtu mwingine mmoja tu atakayejumuika nami quota itakuwa imetimia ingawa ningependa wote tuishinde hasira na tulainishe mioyo yetu, hii ni kwa ajili yetu sote.

Usawa huu kuanza kubeba magodoro na kuanza kuutafuta mpaka siyo kabisa. Kwanza haitasaidia lolote sana sana kuumizana tu.
 
Bila kujali itikadi, misimamo wala imani zetu baada ya lisaa limoja kutoka sasa acha lolote unalofanya tujumuike katika maombi haya.

Nikipata mtu mwingine mmoja tu atakayejumuika nami quota itakuwa imetimia ingawa ningependa wote tuishinde hasira na tulainishe mioyo yetu, hii ni kwa ajili yetu sote.
Umepata mmoja ni mimi. Naungana nawe kumuombea ila mimi nitamuombea kwa jina la Yesu sijui mwenzangu ni bohola au maana sijui unaomba kwa jina gani.
 
namuomba Mungu amfunge shetani kwa minyororo ili asitutie majaribuni.

nakuapia kwa jinsi alivyoyavuruga mambo ni rahisi sana shetani kunishawishi nimvurumishie hata kohozi.
 
Tafuta njia uuanganishwe na wafungwa wa Butimba chini ya yule Askofu wao. Wako vizuri maombi yao yamejibiwa papo kwa papo. Yale mapepo yanayo mpinga Rais yamejiinua na kujianika hadharani kwa kazi za mikono na vinywa vyao.
 
Sasa mbona unaniacha peke yangu wakati umesema unatafuta wa kuungana na wewe?

Nadhani haukuelewa dhamira yangu. Nikichokusudia kusema ni kuwa ikifika muda huo popote ulipo chukua muda kumuombea Rais Magufuli. Utakapokuwa unafanya hivyo na mimi na wengine pia tutakuwa tunafanya hivyo. Ndiyo kujumuika kwenyewe huko.
 
Nadhani haukuelewa dhamira yangu. Nikichokusudia kusema ni kuwa ikifika muda huo popote ulipo chukua muda kumuombea Rais Magufuli. Utakapokuwa unafanya hivyo na mimi na wengine pia tutakuwa tunafanya hivyo. Ndiyo kujumuika kwenyewe huko.
Ameen
 
Nami nipo nawe katika maombi, JPM amevunja "miiko" ambayo akuna aliyewahi kuthubutu kuigusa, ukisikia watu wanasema "AMEWATELEKEZA WALIOMFIKISHA HAPA" maana yake "kundi la wateule, wanaofaidi mema ya nchi kwa njia halali na haramu, maslahi yao yameguswa"....TUNAFUNGA NA KUOMBA KWA AJILI YA MZALENDO WA KWELI, JOHN JOSEPH POMBE MAGUFULI.
 
Tafadhali jumuikeni nami kuanzia saa 2:00 hadi 2:30 usiku huu wa leo kwa ajili ya kumuombea Rais Magufuli.

Maandiko yanasema wanapokusanyika wawili au zaidi Mungu atayapokea maombi hayo. Umbali siyo tatizo, kwenye mambo ya kiroho hakuna umbali.

Tumuombee afya njema, hekima, huruma, maarifa, roho ya kiasi na kuepuka hasira.

Najua wengi tuna maoni HASI kuhusu Rais Magufuli na serikali yake ila inabidi tukumbuke wote tuko kwenye boti moja. Ikizama tunazama wote na najua wengi wetu hata kuogelea hatujui.

Kuna njia halali za kumshinikiza Rais na serikali yake. Kwa mfano bado naamini maandamano ni njia sahihi na ambayo ingeweza kutumika ila kila Afande Mroto akitoa vitisho watu wanapoteana. Hilo siyo la kumlaumu Rais Magufuli ni woga wetu sisi wenyewe.

Kutumia njia za hila, blackmail na zingine za kiuhalifu ili Rais atimize matakwa ya kundi fulani siyo njia sahihi. Rais ana madaraka makubwa sana, anaweza kuamua kulianzisha hapa na hakuna atakayeweza kumzuia. Tuwe makini sana.

Nimekumbuka Mfalme Sauli alikuwa anamsakama Daudi kwa muda mrefu ili amuue ila Daudi pamoja na kwamba tayari alikuwa ameshapakwa mafuta na Nabii Samuel ya kuwa mfalme lakini hata alipopata nafasi mara kadhaa ya kummaliza Sauli kwa mikono yake mwenyewe hakufanya hivyo. Alimuachia hilo jukumu Mwenyezi Mungu mwenyewe.

Kumbuka ni kuanzia saa 2:00 hadi 2:30 usiku huu wa leo. Tafadhali usizembee na mtaarifu mwenzio.
" Usilitaje bure jina la la bwana Mungu wako "
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom