Dijovisonjn
JF-Expert Member
- Nov 14, 2011
- 466
- 125
Ni kweli kabisa alivyosema mh. Mbowe kuwa mbunge mmoja wa CHADEMA ni sawa na wabunge 30 wa CCM.
Hivi ulishawahi kujiuliza ni kwa nini wabunge wa ccm (walio wengi sio wote) ni very weak? hawajui kujielezea, hawajui kujenga hoja? kama hukupata majibu mimi nitakusaidia kukujibu leo, ni kwa sababu chama chao ndio kinashika dola, ni kwa sababu wengi wao walitumia pesa kuupata ubunge na ni kwa sababu wamelizika na mambo yanayofanywa na serikali yao ya CCM!
Na je ulishawahi kujiuliza kuwa ni kwa nini wabunge wa CHADEMA ni wazuri kujielezea, kujenga hoja na kuonekana kwenda sawa sawa na wale wa CCM japokuwa wao ni 48 tu? Na hapa nikusaidie kukupa jibu ni kwa sababu wengi wao ni vijana (wanatafuta umaarufu wa kisiasa), wengi ni wasomi,hawakuingia bungeni kwa pesa na sasa wanajitahidi kumaintain position yao katika jamii na sababu kuu ni kwa sababu chama chao hakijashika dola!
Hivi ulishawahi kujiuliza siku CHADEMA ikishika dola hali itakuwaje bungeni?
mi naona hivi:-
Wabunge 60 wa CHADEMA watakuwa sawa na mbunge 1 wa CCM.
kivipi?
kwanza, wabunge wa CHADEMA watapunguza ukali wao bungeni na kuwa bize kuitetea serikali.
Pili, mawaziri wengi wa CHADEMA watakuwa hawana na uzoefu wa kiutawala wakati wapinzani wao watakuwa na uzoefu mwingi na wakutosha (kumbuka uwaziri kivuli unatofauti kubwa sana na uwaziri kamili)
Tatu, CHADEMA wakiingia madarakani watataka kuongoza tofauti na CCM wanavyoongoza kitu ambacho kukiongea ni rahisi lakini kukitekeleza ukiwa madarakani ni vigumu mno. kwa mfano kama Dr Slaa angeshinda katika uchaguzi wa 2010 angewezaje kutengeneza serikali yake bila kuwachagua wale anaowafahamu na kuamini ndo atakaoweza kufanya nao kazi? naamini hata kama mimi ningekuwa na uwezo gani asingenichagua kwa sababu hanijui na wala sijawahi kufanya naye kazi (kitu ambacho JK amefanya na hata kiongozi yeyote atalazimika kufanya kama JK)
Nne, CHADEMA watataka kutuonesha watanzania kuwa hatujakosea kuwachagua kutuongoza nahisi watakuwa wanafanya maamuzi mengi ya kuturidhisha wananchi kwa 100% kitu ambacho ni hatari kwa uongozi.
Tano, kama ilivyo kwa nchi nyingine za Afrika, CHADEMA na wao hawataongoza bila kuwa na msukumo kutoka nchi za magharibi, kitu ambacho ni hatari kwa viongozi woooote wa Afrika.
HITIMISHO.
UZOEFU WA KISERIKALI WALIONAO VIONGOZI WENGI WA CCM NA UKOSEFU WA UZOEFU WA UONGOZI WA KISERIKALI WALIONAO VIONGOZI WENGI WA CHADEMA UTAWAFANYA WABUNGE 60 WA CHADEMA KUWA SAWA NA MBUNGE MMOJA WA CCM SIKU CHADEMA WAKISHIKA DOLA!
Hivi ulishawahi kujiuliza ni kwa nini wabunge wa ccm (walio wengi sio wote) ni very weak? hawajui kujielezea, hawajui kujenga hoja? kama hukupata majibu mimi nitakusaidia kukujibu leo, ni kwa sababu chama chao ndio kinashika dola, ni kwa sababu wengi wao walitumia pesa kuupata ubunge na ni kwa sababu wamelizika na mambo yanayofanywa na serikali yao ya CCM!
Na je ulishawahi kujiuliza kuwa ni kwa nini wabunge wa CHADEMA ni wazuri kujielezea, kujenga hoja na kuonekana kwenda sawa sawa na wale wa CCM japokuwa wao ni 48 tu? Na hapa nikusaidie kukupa jibu ni kwa sababu wengi wao ni vijana (wanatafuta umaarufu wa kisiasa), wengi ni wasomi,hawakuingia bungeni kwa pesa na sasa wanajitahidi kumaintain position yao katika jamii na sababu kuu ni kwa sababu chama chao hakijashika dola!
Hivi ulishawahi kujiuliza siku CHADEMA ikishika dola hali itakuwaje bungeni?
mi naona hivi:-
Wabunge 60 wa CHADEMA watakuwa sawa na mbunge 1 wa CCM.
kivipi?
kwanza, wabunge wa CHADEMA watapunguza ukali wao bungeni na kuwa bize kuitetea serikali.
Pili, mawaziri wengi wa CHADEMA watakuwa hawana na uzoefu wa kiutawala wakati wapinzani wao watakuwa na uzoefu mwingi na wakutosha (kumbuka uwaziri kivuli unatofauti kubwa sana na uwaziri kamili)
Tatu, CHADEMA wakiingia madarakani watataka kuongoza tofauti na CCM wanavyoongoza kitu ambacho kukiongea ni rahisi lakini kukitekeleza ukiwa madarakani ni vigumu mno. kwa mfano kama Dr Slaa angeshinda katika uchaguzi wa 2010 angewezaje kutengeneza serikali yake bila kuwachagua wale anaowafahamu na kuamini ndo atakaoweza kufanya nao kazi? naamini hata kama mimi ningekuwa na uwezo gani asingenichagua kwa sababu hanijui na wala sijawahi kufanya naye kazi (kitu ambacho JK amefanya na hata kiongozi yeyote atalazimika kufanya kama JK)
Nne, CHADEMA watataka kutuonesha watanzania kuwa hatujakosea kuwachagua kutuongoza nahisi watakuwa wanafanya maamuzi mengi ya kuturidhisha wananchi kwa 100% kitu ambacho ni hatari kwa uongozi.
Tano, kama ilivyo kwa nchi nyingine za Afrika, CHADEMA na wao hawataongoza bila kuwa na msukumo kutoka nchi za magharibi, kitu ambacho ni hatari kwa viongozi woooote wa Afrika.
HITIMISHO.
UZOEFU WA KISERIKALI WALIONAO VIONGOZI WENGI WA CCM NA UKOSEFU WA UZOEFU WA UONGOZI WA KISERIKALI WALIONAO VIONGOZI WENGI WA CHADEMA UTAWAFANYA WABUNGE 60 WA CHADEMA KUWA SAWA NA MBUNGE MMOJA WA CCM SIKU CHADEMA WAKISHIKA DOLA!