Leo Major: Shujaa wa aina yake

zitto junior

JF-Expert Member
Oct 7, 2013
19,039
28,688
Habari za jioni wana JF,

Natumaini wote wazima humu, na moja kwa moja niende kwenye mada.

1297486572115_ORIGINAL.jpg

UTANGULIZI

Leo major alikuwa mwanajeshi wa Canada ambaye aliyepigana vita mbili kubwa na kuibuka shujaa wa aina yake yaani Vita Kuu ya Pili ya Dunia (1940s) na Vita vya Korea (1950s). Leo alizaliwa mnamo january,1921 huko Bedford Massachusets, USA na baadae wakahamia nchini Canada ambako ndio ulikuwa uraia wa wazazi wake. Inaelezwa kuwa Leo tokea utotoni hakuwa na uhusiano mzuri na baba yake hivyo ikapelekea aishi mbali naye (kwa shangazi yake) na kwakuwa alijua baba yake alimdharau sababu hakuwa na "jipya" hivyo hakuwa na mchango wowote kwenye familia ikampelekea leo kuamua kujiunga na jeshi la Canada mwaka 1940 ili aweze kuthibitisha kwa baba yake kuwa yeye ni "hazina" kwenye taifa na familia na sio "mzigo" kama walivyofikiri.

VITA KUU YA DUNIA YA PILI

Akiwa jeshini Leo alipangwa kushiriki vita kuu ya pili ya dunia na alikuwa mmoja ya wanajeshi ambao walihusika kwenye operation D-Day kule Normandy ambapo majeshi ya Marekani,Canada na washirika yalivamia ulaya ili kuikomboa kutoka mikono ya Ujerumani chini ya Hitler. Inaelezwa kwamba akiwa Normandy aliweza kuteka kifaru cha Wajerumani akiwa peke yake huku akipambana na maadui takribani 10 kwenye kifaru, kitendo hiki kiliwawezesha kunasa mawasiliano muhimu na taarifa za kiintelijensia zingine ambazo ziliwasaidia kufichua maficho ya wajerumani na kurahisisha uvamizi wao huko Ufaransa. Siku chache baadae Leo major alikumbana na kikosi cha wanajeshi wa Kijerumani na Major alifanikiwa kupambana nao kishujaa akiwa peke yake hadi kufanikiwa kuwaua wanne lakini kwa bahati mbaya mwanajeshi mmoja wa kijerumani alimrushia bomu ambalo lilimlipukia Major na kumjeruhi sana ikiwemo kumtoa jicho la kushoto.

Baada ya kuwa ameng'olewa jicho alitakiwa kuondolewa kwenye uwanja wa vita na kurudishwa nyumbani lakini katika kitendo cha kishujaa na kizalendo bwana Major aligoma kurudi nyuma na inaelezwa kwamba baada ya mabishano ya muda mrefu alidai haitaji macho mawili ili aweze kutumia bunduki kumlenga adui kwenye sniper gun yake maana ikumbukwe jamaa alikuwa ni mdunguaji (sniper) hivyo aliona jicho moja linatosha kulenga shabaha na mwishowe akakubaliwa kuendelea kuwepo uwanja wa vita huko Ufaransa.

USHUJAA UHOLANZI

Jeshi la washirika (Allied ) lilipofika nchini uholanzi Leo Major alipewa kazi ya kwenda kutafuta taarifa za kiintelijensia kuhusu ngome za adui kwenye mji wa Schledt ila major hakuishia kwenye ujasusi tu bali alidhamiria kuyateketeza majeshi ya ujerumani akiwa peke yake!! Alisogea mpaka kwenye kambi ya kijerumani na kuanza kudungua mwanajeshi mmoja baada ya mwingine huku akibadilisha nafasi anapowalengea kiasi ikaonekana kama ni jeshi limevamia na sio mtu mmoja.

Wakati jeshi la Ujerumani likipanick alifanikiwa kumuwinda commander wa kikosi kile hapo kambini na kumteka ambapo alimpa sharti kuwa akubali surrender lasi hivyo ''vikosi'' vilivyozunguka kambi yake vitammaliza bila kujua "timbwili" lote hapo kambini lilisababishwa na mtu mmoja tu. Hivyo walisurrender kwa ujumla wao wanajeshi 93 wa Kijerumani na hata aliporudi kambini viongozi wake walipigwa na butwaa maana alitumwa kuleta taarifa za adui ila yeye sio tu alirudi na taarifa bali na maadui wenyewe. Kitendo hiki kilichukuliwa cha kishujaa sana hivyo alipewa medali ya juu ya ushujaa ''Distinguished conduct medal'' kwa sababu ya tukio hili.

distinguished_conduct_medal_-_victoria.jpg

USHUJAA #2

February 1943 wakiwa Uholanzi bado Leo major alikuwa anasaidiana na mwenzake kupakia miili ya wanajeshi waliofariki kwenye vita na mara baada ya kupakia miili hii wakawasha gari na kuondoka lakini ghafla ukatokea mlipuko wa bomu lililokanyagwa na gari yao hivyo likawajeruhi vibaya sana na aliponea ''chupuchupu'' kifo kwa mara nyingine.

Aliporudishwa kambini kwa ajili ya vipimo akaambiwa amevunjika mgongo mara 3, mbavu mara 4 na visigino vyote viwili hivyo akaambiwa kwa mara nyingine kuwa ushiriki wake kwenye vita umeishia hapo hivyo atarudishwa canada. Ila kabla hilo halijafanyika Major alifanikiwa kutoroka hapo kambini na kwenda mji wa Nijmegen ambako aliishi kwenye moja ya familia za Uholanzi na kupewa huduma za hapa na pale hata baada ya mwezi licha ya maumivu aliokuwa nayo hakukata tamaa na alirudi upya jeshini baada ya mwezi ingawa sijaona vyanzo vinavyoeleza aliwezaje kuruhusiwa kurudi jeshini akiwa na majeraha wala alikwepaje adhabu ya kutoroka jeshini.
 
images (48).jpg
USHUJAA #3
Mmamo April,1943 majeshi ya washirika yalipanga kuteka mji wa Zwolle, Uholanzi. Ilitolewa tangazo na commander wa kikosi chao kuwa wajitolee kwenda kukusanya taarifa za adui na ngome zake ili jeshi zima likivamia basi wawe na taarifa za uhakika kuhusu adui. Wengi kwa kujua nguvu ya jeshi la ujerumani waliogopa ila Leo Major na mwenzie mmoja bwana Willy Arseneault walikubali kujitolea. Usiku walipokwenda kupeleleza bwana willy alionekana na wanajeshi wa kijerumani hivyo alidunguliwa na risasi za adui na kufariku hapo hapo.

Tukio hili lilimuumiza sana Leo Major na licha ya kukimbia sababu alikuwa ameonekana aliamua kuvamia "kijiwe" hicho cha adui na kufanikiwa kuua wawili huku wengine wakikimbia na gari. Hakuishia hapo alisonga mbele na kuteka gari ya kijeshi la ujerumani hivyo aliweza kupenya hadi ndani ya mji wa Zwolle ambapo alifanikiwa kuingia kwenye bar ambayo ina askari mwenye cheo wa Ujerumani, ambapo alimpiga mkwara kuwa jeshi la washirika limeshazingira mji na litashambulia muda wowote hivyo akamuachua yule kamanda aende kuwataarifu wenzake. Alipotoka humo alienda kutega mabomu kwenye maeneo tofauti (sio makazi ya watu) na yalipoanza kulipuka moja baada ya nyingine wanajeshi wajerumani walifikiri ndio majeshi ya washirika yamevamia hivyo wakaanza kupanick sababu hawakuwa wameona majeshi yakija mji huo ila bado wanasikia milipuko so walipigwa na butwaa.

Alichokifanya Leo major ni kubadilisha maeneo ya mashambulizi yaani anadungua mwanajeshi mmoja mtaa huu alafu anahamia mtaa wa pili na kushoot .mwingine hii ikajenga picha kuwa majeshi ya washirika yameshajipenyeza kwenye ngome na ukiongezea na ili milipuko basi wajerumani wakajua hawana chao hivyo askari zaidi ya 800 wakautekeleza mji ili wakajipange upya. Hivyo Leo Major kwa mara nyingine badala ya kurudi na taarifa za kiintelijensia kuhusu ADUI yeye alirudi na taarifa kuwa HAKUNA ADUI katika mji wa Zwolle. Kwa ushujaa huu alipewa kwa mara nyingine medali ya juu ya heshima jeshini ya DCM maana aliokoa mji mzima dhidi ya umwagaji damu kama jeshi la washirika lingevamia mji huo. Kitendo hiki cha kishujaa kilisababisha jina la mtaa huko uholanzi lipewe kwa heshima yake kama mkombozi wao.

leo_majorlaan.jpg

USHUJAA VITA YA KOREA

Leo Major baada ya vita ya pili ya dunia hakuishia hapo bali alishiriki na vita ya korea iliyotokea mwaka 1950 ambapo korea kusini ilivamiwa na vikosi vya kikomunisti kutokea upande wa kaskazini wa korea hivyo marekani na washirika wake wakiwa chini ya bendera ya UN walivamia korea ili kuzuia wakomunisti. Leo Major hakuwa nyuma kwenye vitendo vyake vya kishujaa tena hasa katika Battle ya Maryang san ambapo ilikuwa ni mission ya kuteka mlima ambao ulikuwa muhimu sana kwani ulikuwa unaona mzunguko wa mile 14. November 22,1951 jeshi la China lilivamia likiwa na kikosi cha wanajeshi 40,000 na kufanikiwa kuwafurumusha vikosi vya Wamarekani kutoka kilima hicho. Na siku kadhaa baadae jeshi la marekani lilifanya shambulizi kuukomboa mlima huo ili walikutana na kipigo kikali hivyo mission ikaishia hapo. Kwa kuona haya kamandi ya brigade yake ikaamua kumteua Leo Major na vijana wake kama 20 ambao ni wadunguaji/snipers waweze kupata upenyo na kuvuruga ngome ya adui.

Leo Major na vijana wake waliweza kutambaa na kujipenyeza kwenye ngoma ya adui hadi juu ya kilima. Walipofika juu wakaanza kudungua wanajeshi wa kichina mmoja baada ya mwingine hii ilitengeneza panick kwenye kambi ya wachina maana walijiuliza kivipi shambulizi litokee katikati ya ngome yao ilihali adui yupo chini ya mlima? Aliweza kupambana na vikosi hivyo vya wachina usiku kucha huku akiwasaidia majeshi yaliokuwa chini kupata urahisi wa kushambuli ngome hiyo na mwisho wa siku kuwezesha Leo major na kikosi chake kuweza kuteka kilima hicho na kuletea ushindi vikosi vya washirika dhidi ya jeshi la china. Na kwa ushujaa huu alitunukiwa medali ya juu ya heshima ya kijeshi kwa mara nyingine tena sababu ya ushujaa wake.

images (38).jpg

HITIMISHO

Kupitia mtu huyu tunaweza jifunza kutokukata tamaa kwenye maisha maana licha ya changamoto za kupata ulemavu wa jicho na baadae kuvunjika mgongo ila bado aliweza endelea na vita hadi kushinda medali hizo. Pia story kama hizi najua watanzania tunazo mfano ya yule askari wa Tanzania kule Darfur ambaye alipambana na "brigade" ya waasi na kuwapunguza hadi risasi yake ya mwisho ndipo akauawa ila shida nyingi zinafanywa siri ila ni wakati na sisi tuanze kuwatambua mashujaa kama hawa ili hata watoto wa vizazi hivi wajengewe moyo wa kujitoa kwa ajili ya nchi yao licha ya changamoto zingine.

Naomba kuwasilisha.
 
Mkuu napata vitu adimu na vitu vilivyotukuka kupitia maandiko yako. Hii ndio JamiiForums ninayoijua mimi.
 
Ana moyo sana, hawa ndo wanaojenga Nchi ambayo huliwa na wasio mashujaa.
Ni sawa na waliopigana vita ya Idd Amin walipambana asivuke border asije pora rasilimali zetu ila baadae wakaja viongozi mafisadi wakaachia rasilimali zetu zifujwe dah inauma sana laiti wangefufuka wangehuzunika sana.
 
Yuko vizuri sana huyu jamaa. Kwa mikwara yake namfananisha na yule mlevi aliyeteka majambazi watatu wenye silaha na kuwapeleka kituo cha police huku akiwamulikia njia kwa torch na walevi wengine wakiwa wamebeba bunduki za majambazi.
 
Huwa natamani sana kujua kuhusu wanajeshi wetu wamefanyamengi sana lakini kwasababu zisizoelezeka tumefichwa taarifa nyingi sana za mashujaa wetu tumebakia kupewa story zao kiumbea tu
Sijui kwanini watawala wanapenda kufanya siri hizi mambo si unaona hata yule bodyguard wa nyerere alipoandaa kitabu naona ikabidi kipelekwe Kitengo ili "kihaririwe" sasa kwa staili hii sidhani kama stori za mashujaa wetu zitawahi tunzwa katika uhalisia wake.
 
Yuko vizuri Sana huyu jamaa kwa mikwara yake namfananisha na yule mlevi aliyeteka majambazi watatu wenye silaha na kuwapeleka kituo cha police huku akiwamulikia njia kwa torch na walevi wengine wakiwa wamebeba bunduki za majambazi
Hahahaha kumbe hata bongo tuna leo major?? Embu tupe kidogo mkuu kivp mlevi ateke jambazi??
 
Sijui kwanini watawala wanapenda kufanya siri hizi mambo si unaona hata yule bodyguard wa nyerere alipoandaa kitabu naona ikabidi kipelekwe Kitengo ili "kihaririwe" sasa kwa staili hii sidhani kama stori za mashujaa wetu zitawahi tunzwa katika uhalisia wake.
Hizi kelele zetu na udadisi wetu usihishie hapa tuwashinikize hawa wazee wanaojiona wenye hati milmiki ya hii nchi mpka kieleweke naamini ipo siku ukweli wote utakuwa wazi.
 
View attachment 864420
USHUJAA #3
Mmamo April,1943 majeshi ya washirika yalipanga kuteka mji wa Zwolle,uholanzi. Ilitolewa tangazo na commander wa kikosi chao kuwa wajitolee kwenda kukusanya taarifa za adui na ngome zake ili jeshi zima likivamia basi wawe na taarifa za uhakika kuhusu adui. Wengi kwa kujua nguvu ya jeshi la ujerumani waliogopa ila leo major na mwenzie mmoja bwana willy arseneault walikubali kujitolea. Usiku walipokwenda kupeleleza bwana willy alionekana na wanajeshi wa kijerumani hivyo alidunguliwa na risasi za adui na kufariku hapo hapo. Tukio hili lilimuumiza sana leo major na licha ya kukimbia sababu alikuwa ameonekana aliamua kuvamia "kijiwe" hicho cha adui na kufanikiwa kuua wawili huku wengine wakikimbia na gari. Hakuishia hapo alisonga mbele na kuteka gari ya kijeshi la ujerumani hivyo aliweza kupenya hadi ndani ya mji wa zwolle ambapo alifanikiwa kuingia kwenye bar ambayo ina askari mwenye cheo wa ujerumani, ambapo alimpiga mkwara kuwa jeshi la washirika limeshazingira mji na litashambulia muda wowote hivyo akamuachua yule kamanda aende kuwataarifu wenzake. Alipotoka humo alienda kutega mabomu kwenye maeneo tofauti (sio makazi ya watu) na yalipoanza kulipuka moja baada ya nyingine wanajeshi wajerumani walifikiri ndio majeshi ya washirika yamevamia hivyo wakaanza kupanick sababu hawakuwa wameona majeshi yakija mji huo ila bado wanasikia milipuko so walipigwa na butwaa. Alichokifanya Leo major ni kubadilisha maeneo ya mashambulizi yaani anadungua mwanajeshi mmoja mtaa huu alafu anahamia mtaa wa pili na kushoot .mwingine hii ikajenga picha kuwa majeshi ya washirika yameshajipenyeza kwenye ngome na ukiongezea na ili milipuko basi wajerumani wakajua hawana chao hivyo askari zaidi ya 800 wakautekeleza mji ili wakajipange upya. Hivyo leo major kwa mara nyingine badala ya kurudi na taarifa za kiintelijensia kuhusu ADUI yeye alirudi na taarifa kuwa HAKUNA ADUI katika mji wa Zwolle. Kwa ushujaa huu alipewa kwa mara nyingine medali ya juu ya heshima jeshini ya DCM maana aliokoa mji mzima dhidi ya umwagaji damu kama jeshi la washirika lingevamia mji huo. Kitendo hiki cha kishujaa kilisababisha jina la mtaa huko uholanzi lipewe kwa heshima yake kama mkombozi wao.
View attachment 864422

USHUJAA VITA YA KOREA
Leo major baada ya vita ya pili ya dunia hakuishia hapo bali alishiriki na vita ya korea iliyotokea mwaka 1950 ambapo korea kusini ilivamiwa na vikosi vya kikomunisti kutokea upande wa kaskazini wa korea hivyo marekani na washirika wake wakiwa chini ya bendera ya UN walivamia korea ili kuzuia wakomunisti. Leo major hakuwa nyuma kwenye vitendo vyake vya kishujaa tena hasa katika Battle ya Maryang san ambapo ilikuwa ni mission ya kuteka mlima ambao ulikuwa muhimu sana kwani ulikuwa unaona mzunguko wa mile 14. November 22,1951 jeshi la China lilivamia likiwa na kikosi cha wanajeshi 40,000 na kufanikiwa kuwafurumusha vikosi vya wamarekani kutoka kilima hicho. Na siku kadhaa baadae jeshi la marekani lilifanya shambulizi kuukomboa mlima huo ili walikutana na kipigo kikali hivyo mission ikaishia hapo. Kwa kuona haya kamandi ya brigade yake ikaamua kumteua Leo major na vijana wake kama 20 ambao ni wadunguaji/snipers waweze kupata upenyo na kuvuruga ngome ya adui. Leo major na vijana wake waliweza kutambaa na kujipenyeza kwenye ngoma ya adui hadi juu ya kilima. Walipofika juu wakaanza kudungua wanajeshi wa kichina mmoja baada ya mwingine hii ilitengeneza panick kwenye kambi ya wachina maana walijiuliza kivipi shambulizi litokee katikati ya ngome yao ilihali adui yupo chini ya mlima? Aliweza kupambana na vikosi hivyo vya wachina usiku kucha huku akiwasaidia majeshi yaliokuwa chini kupata urahisi wa kushambuli ngome hiyo na mwisho wa siku kuwezesha Leo major na kikosi chake kuweza kuteka kilima hicho na kuletea ushindi vikosi vya washirika dhidi ya jeshi la china. Na kwa ushujaa huu alitunukiwa medali ya juu ya heshima ya kijeshi kwa mara nyingine tena sababu ya ushujaa wake.
View attachment 864423

HITIMISHO
Kupitia mtu huyu tunaweza jifunza kutokukata tamaa kwenye maisha maana licha ya changamoto za kupata ulemavu wa jicho na baadae kuvunjika mgongo ila bado aliweza endelea na vita hadi kushinda medali hizo. Pia story kama hizi najua watanzania tunazo mfano ya yule askari wa Tanzania kule Darfur ambaye alipambana na "brigade" ya waasi na kuwapunguza hadi risasi yake ya mwisho ndipo akauawa ila shida nyingi zinafanywa siri ila ni wakati na sisi tuanze kuwatambua mashujaa kama hawa ili hata watoto wa vizazi hivi wajengewe moyo wa kujitoa kwa ajili ya nchi yao licha ya changamoto zingine.

Naomba kuwasilisha.
Mkuu hii story ya huyo mwanajeshi wa Tanzania ntaipatia wapi tafadhal!?
 
Mkuu hii story ya huyo mwanajeshi wa Tanzania ntaipatia wapi tafadhal!?
Nilisimuliwa tu na mjeshi mmoja huko mara ambaye aliwahi pelekwa Darfur kulinda amani. Hata ikiandikwa haitoruhusiwa kuchapishwa!! nakumbuka hata tukio la wanajeshi wa Tanzania kuuawa kule msituni na waasi wa ADF-NALU kuna polisi mmoja alikuwa anachambua hali halisi iliotokea kule duh ghafla kuna mwana-TISS akaingia kupiga biti kwenye group kuhusu jamaa kuendelea kusimulia hilo tukio. Tokea hapo nikajua nchi yetu inasafari ndefu sana katika kuandika kumbukumbu za mashujaa wetu vitani.
 
Nilisimuliwa tu na mjeshi mmoja huko mara ambaye aliwahi pelekwa Darfur kulinda amani.... Hata ikiandikwa haitoruhusiwa kuchapishwa!! nakumbuka hata tukio la wanajeshi wa Tanzania kuuawa kule msituni na waasi wa ADF-NALU kuna polisi mmoja alikuwa anachambua hali halisi iliotokea kule duh ghafla kuna mwana-TISS akaingia kupiga biti kwenye group kuhusu jamaa kuendelea kusimulia hilo tukio. Tokea hapo nikajua nchi yetu inasafari ndefu sana katika kuandika kumbukumbu za mashujaa wetu vitani.
Daaah kazi ya jeshi inachangamoto zake aseee yan unawapigania watu ambao hawajielewi na hawatambui mchango wako!
 
Back
Top Bottom