Leo katika Historia: Mambo (facts) ambayo popote huwa hayaelezewi au kumfundisha

MSEZA MKULU

JF-Expert Member
Jul 22, 2011
3,752
5,497
Mambo 12 ambayo ni nadra kuyasikia tunapozungumia Historia

1: Mwaka 536A.D kulitokea vumbi kubwa iliyotanda dunia nzima na kuzuia jua lisionekane duniani kwa mwaka mzima. Hili tukio lilisababisha njaa na magonjwa dunia nzima.
Extreme weather events of 535–536 - Wikipedia, the free encyclopedia

2: Mlipuko Wa volcano mwaka 1883, ulitoa sauti kubwa kuwahi kusikika tangu dunia iumbwe.
Sauti ilisikika zaidi ya km 4800.
1883 eruption of Krakatoa - Wikipedia, the free encyclopedia

3: Miaka ya zamani (ice age) waingereza walikuwa wanakulana na kutumia mafuvu ya wenzao kama vikombe.
More proof ice age Britons had cannibalistic habits | Natural History Museum

4: Ajali ya gari ya kwanza duniani ilitokea mwaka 1891 huko Ohio. hakuna waliokufa bali mwnasayansi aliyekua anatest hilo gari na abilia wake walipata maumivu na michubuko kidogo.
World's First Automobile Accident - Ohio History Central

5: Kusherekea krismass Marekani hadi mwaka 1836 ilikuwa ni kinyume cha sheria, haikuruhusiwa maana Krismass ilihesabika kama sikukuu ya Kipagani isiyohusiana na mambo yoyote ya kidini kama ilkivyokuwa ikinadiwa.
Christmas - Ancient Pagan Holiday Which Was Criminally Illegal Until 1907

6: Zaidi ya wazungu million 1.2 wakiwemo Wanaume, watoto na wakina mama kati ya miaka ya 1530 hadi 1780 walitekwa na kuja kutumikishwa afrika kama watumwa. Wakuwa wanauzwa na waafrika Wa Morocco,tripol, Algeria na matajiri Wa afrika kaskazini. Watumwa hao walitokea uingerza,Hispania,ureno,ufaransa etc na wengine zaidi ya 700 walitokea marekani na kuuzwa eneo hilo.
Barbary slave trade - Wikipedia, the free encyclopedia

7: Mwaka 1212 zaidi ya watoto wadogo 30,000 kutoka ulaya wakiongozwa na mtoto mwenzako ambaye alisema ametokewa na yesu kwenda kuukomboa Jerusalem kwa amani kutoka mikononi kwa waislamu. Walianza safari kuelekea kusini kwa imani kuwa wakivuka Mediterranean bahari itapasuka kama enzi za musa bahari ya shamu ili wapate shortcut kuelekea Jerusalem. Bahari haikupasuka waliishia kutekwa na maharamia na kuuza kama watumwa Tunisia na wengine kufa kwa njaa. Hakuna hata mmoja aliyerudi
The Crusade of the Children: Thousands of Children March to Holy Land but Never Return

8: Kwa miaka 3400 iliyopita wanadamu wamekuwa waliishia kwa amani bila hofu wala vita miaka 268.Hii ni sawa na asilimia nane tu ya muda wote, muda ulibaki ni shida mabalaa, majanga na vita kila kukuchagulia.
'What Every Person Should Know About War'

9:kuzungumzia vita vibaya sana katika dunia hii ya kisasa, ilikuwa ni vita vya TRIPPLE alliance iliyomaliza na kuwaua kabisa asilimia 60 ya wananchi wote Wa Paraguai. Na kuacha uwiiano Wa mwanaume mmoja kwa wanawake wanne.
WaroftheTripleAlliance.com

10: Katika karne ya 16 na 17, wazungu wakiwemo watawala,wafalme,wanasayansi,viongozi au watumishi wakidini\makasisi kwa ugonjwa wowote waliokuwa wakiumwa au kuugua hata kichwa walikuwa wanatumia dawa ambayo mchanganyiko wake ulihusisha mifupa, damu na mafuta ya wanadamu iliyosagwa na kuchanganywa pamoja.
History, Travel, Arts, Science, People, Places | Smithsonian

11: Kuna mamilioni ya watu walio katika utumwa Leo kuliko wakati wowote katika historia ya utumwa duniani. Slavery - Wikipedia, the free encyclopedia

12: Mgomo Wa kwanza Wa wafanyakazi duniani ulifanyika miaka mingi iliyopita BC wakati Wa ujenzi Wa Pyramids huko Egypt. Ikumbukwe kuwa piramidi hazikujengwa na watumwa, huu ilikuwa ni uongo uliosambazwa na jamaa mmoja kutokea ugiriki. Pyramid zilijengwa na watu walioajiriwa na inasemekana zilijengwa na waethiopia sio wamisri na viongozi wao farao.

Ancient Egypt's fantastic and weird history
Today in labor history: First recorded strike in Egypt, maybe ever » peoplesworld
Edited. Samahanini kwa usumbufu Wa TYPO

Ongea au sema chochote
 
Mgomo wa kwanza wa wafanyakazi kuingia kwenye record uliasisiwa na Edward Nedd Ludd (Luddism) wakati wa mapinduzi ya viwanda hiyo namba 12 sina record nao labda utupe proof zaidi
 
Duuh! Asante kwa taarifa Mkuu, ila mda mwingine uandike vizuri maelezo yako maana yamejichanganya sana.
 
Mgomo wa kwanza wa wafanyakazi kuingia kwenye record uliasisiwa na Edward Nedd Ludd (Luddism) wakati wa mapinduzi ya viwanda hiyo namba 12 sina record nao labda utupe proof zaidi
Unawe,za kupitia source. Huo ulikuwa Wa kwanza kwa marekani sio duniani
 
Mkuu,unaweza ukai-edit kidogo maana inaleta shida sana kuisoma kwa mfululizo kwani maneno mengi yamekosewakosewa
 
Namba moja ninamashaka nayo,kwasababu sidhani kama inawezekana vumbi litande juu dunia nzima still uhai ukawepo.Am.just thinking partially...
 
Hizi habari nyingi ni za uongo.

Huyo mtoto aliwezaje kuwashawishi wenzake elfu 30 na aliwakusanyaje?
 
Kumbe waethiopia ndio walijenga pyramids, kila nikitaka kujifunza ya pyramids mapya yanakuja ingawa yameandikwa zamani.

Sijui ukweli ni upi kama na Xmas ilikuwa ni hivyo
 
Mkuu Jua lisionekane ndani ya mwaka mzima dunia nzima? Hivi unaelewa 99% ya energy ktk planet hii inatoka katika jua? sasa tuna survive vipi likiwa halipo
 
Mkuu Jua lisionekane ndani ya mwaka mzima dunia nzima? Hivi unaelewa 99% ya energy ktk planet hii inatoka katika jua? sasa tuna survive vipi likiwa halipo
sehemu kubwa ya dunia ilifunikwa na vumbi kubwa kwa mwaka kulingana na source. pia sio kwamba jua halikuwepo bali lilikingwa na vumbi na kusababisha maazao kufa na magonjwa
 
Back
Top Bottom