Leo Bungeni..Simbachawene Ashabikia Hoja ya Wabunge Kuongezewa Mafao

reformer

JF-Expert Member
Jul 22, 2011
387
101
Leo bungeni kuna mbungemmoja toka Zanzibar sifahamu kama ni wa CCM au CUF..Bada ya kumaliza kuchangiabajeti ya wizara ya Afrika Mashariki akamalizia kwa kusema...anaungana na Shibudakwamba wabunge waongezewe posho na mishahara sababu kiasi wanachopata sasa nikidogo sana. Akaongeza kuwa wana matatizo sana majimboni kwao hivo wanahitajimafao zaidi yawasaidie kutatua matatizo ya majimboni kwao. Wabunge wa CCMwakampigia makofi.

Cha kushangaza, Simbachawene aliyekuwa anaendesha kikao hicho akamsifia kwakuchangia hoja vizuri...akisema nimependa ulivochangia vizuri hasa hiyo hojayako ya mwisho, akimaanisha hoja ya kupandishiwa mishahara na posho kwawabunge.

Baada ya huyombunge kumaliza kuchangia, akafuatia Zito, naye alipomaliza kuchangia hoja yamsingi akaamua kujibu swala la mafao ya wabunge liloanzashwa na huyo Mzanzibar.Akasema anashangaa kuona kuna baadhi ya wabunge ambao bado wanataka waongezwemafao wakati watanzania wengi wako katika hali ngumu ya maisha, na pia serikaliinasema haina pesa hadi imelazimika kukopa ili kuweza kufanikisha mpango wadharula wa umeme. “Iweje leo sisi tunaka tuongezwe mishahara na posho?..ebutuonyeshe kama sisi ni viongozi, tuwaonyeshe wananchi kwamba nasi tunajali matatizona kero zao. Alimalizia Zitto, pamoja na kuzomewa na Wabunge wengi waCCM.

Simbachawene, hakucomemnt kitu kuhusu issue ya posho bada yaZitto kumaliza kuongea. Lakini nakumbuka siku kadhaa zilizopita wakati hoja yaposho imepamba moto, Simbachawene alikuwa akihojiwa TBC kuhusu suala la posho,akasema anakubaliana nalo ila approach waliotumia CHADEMA haikuwa nzuri. Akaongeza,serikali imelisikia na itaangalia utaratibu mzuri wa kerekabisha posho hizo kwawatumishi wa uma ikiwemo wabunge. But you could see from his eyes, that he didn’tmean what he was saying and today I proved that bada ya kussaport point kuwa mafaoya wabunge yaongezwe, na kujifanya hajamsikia zito kuhusu wabunge kujalimatatizo ya wananchi.

Rai yangu kwa Simbachawene, CCM na serikali yake, pamoja nawanasiasa wengine ambao ni waongo, wanafiki na hawamaanishi kile wasemacho nikwamba..watanzania wa siku hizi tunafatilia mnachokisema, tunawaangiliamsemapo, na tunakumbuka msemacho. So unapoongea kitu hakikisha unamaanisha naunatoa kile kilicho moyoni mwako, kuliko kuongea kitu ambacho kinapinagana nadhamira yako. Koz uongo huwa haufichwi milele iko siku watu watajua ukweli tu..kama leo tulivojua kwamba ww na wabunge wengi wa CCM mkobungeni si kwa ajili ya kushughulikia kero za wananchi bali kwa maslahibinafsi..And we will keep on seeing your true colors.
 
na wakipitisha hy hoja yao ya kijinga kuongezeana mishahara na posho wakati cc twafa na njaa,umeme, mafuta kwakwel porini kutaendeka
 
Hawa watu(ccm) tunaowaita wawakilishi wetu,hawako kwa maslahi yetu hata kidogo.Hivi hizo posho,mafao na masurufu yote wanayojimegea kazi yake ni kutatua matatizo ya wapiga kura wao majimboni?If yes,huko bungeni hizo bajeti wanazojadili na kupitisha ni za nini hasa ikiwa hazilengi kutatua shida za wapiga kura wao?Kwa nini wasiweke mkazo kwenye kuisimamia serikali kutimiza wajibu wake kwa wananchi?NI DHAHIRI KUWA HATUNA WAWAKILISHI BUNGENI...KILICHOSALIA TUJIWAKILISHE WENYEWE SASA!
 
Leo bungeni kuna mbungemmoja toka Zanzibar sifahamu kama ni wa CCM au CUF..Bada ya kumaliza kuchangiabajeti ya wizara ya Afrika Mashariki akamalizia kwa kusema...anaungana na Shibudakwamba wabunge waongezewe posho na mishahara sababu kiasi wanachopata sasa nikidogo sana. Akaongeza kuwa wana matatizo sana majimboni kwao hivo wanahitajimafao zaidi yawasaidie kutatua matatizo ya majimboni kwao. Wabunge wa CCMwakampigia makofi.

Cha kushangaza, Simbachawene aliyekuwa anaendesha kikao hicho akamsifia kwakuchangia hoja vizuri...akisema nimependa ulivochangia vizuri hasa hiyo hojayako ya mwisho, akimaanisha hoja ya kupandishiwa mishahara na posho kwawabunge.

Baada ya huyombunge kumaliza kuchangia, akafuatia Zito, naye alipomaliza kuchangia hoja yamsingi akaamua kujibu swala la mafao ya wabunge liloanzashwa na huyo Mzanzibar.Akasema anashangaa kuona kuna baadhi ya wabunge ambao bado wanataka waongezwemafao wakati watanzania wengi wako katika hali ngumu ya maisha, na pia serikaliinasema haina pesa hadi imelazimika kukopa ili kuweza kufanikisha mpango wadharula wa umeme. "Iweje leo sisi tunaka tuongezwe mishahara na posho?..ebutuonyeshe kama sisi ni viongozi, tuwaonyeshe wananchi kwamba nasi tunajali matatizona kero zao. Alimalizia Zitto, pamoja na kuzomewa na Wabunge wengi waCCM.

Simbachawene, hakucomemnt kitu kuhusu issue ya posho bada yaZitto kumaliza kuongea. Lakini nakumbuka siku kadhaa zilizopita wakati hoja yaposho imepamba moto, Simbachawene alikuwa akihojiwa TBC kuhusu suala la posho,akasema anakubaliana nalo ila approach waliotumia CHADEMA haikuwa nzuri. Akaongeza,serikali imelisikia na itaangalia utaratibu mzuri wa kerekabisha posho hizo kwawatumishi wa uma ikiwemo wabunge. But you could see from his eyes, that he didn'tmean what he was saying and today I proved that bada ya kussaport point kuwa mafaoya wabunge yaongezwe, na kujifanya hajamsikia zito kuhusu wabunge kujalimatatizo ya wananchi.

Rai yangu kwa Simbachawene, CCM na serikali yake, pamoja nawanasiasa wengine ambao ni waongo, wanafiki na hawamaanishi kile wasemacho nikwamba..watanzania wa siku hizi tunafatilia mnachokisema, tunawaangiliamsemapo, na tunakumbuka msemacho. So unapoongea kitu hakikisha unamaanisha naunatoa kile kilicho moyoni mwako, kuliko kuongea kitu ambacho kinapinagana nadhamira yako. Koz uongo huwa haufichwi milele iko siku watu watajua ukweli tu..kama leo tulivojua kwamba ww na wabunge wengi wa CCM mkobungeni si kwa ajili ya kushughulikia kero za wananchi bali kwa maslahibinafsi..And we will keep on seeing your true colors.

Kumbe ni huyu Simbachawene...nadhani ni sawa alichosema kulingana na uwezo wake wa kusoma majira na nyakati...
 
Jamani hawa wabunge wetu wanatujali kweli? Umeme hakuna lakini wanadai posho, maji hakuna wanadai posho,mafuta,sukari,madawa,mishahara midogo,na hali ngumu ya maisha,bado wanadai posho 2.pamba bei ndogo,mahindi bei ndogo,usafiri wa treni,meli,hakuna alafu wanadai posho,wamefanya nini?2waulize..
 
Wapitishe sasa hizo posho zao na mishahara huku mitaan8i hakutakalika tutawaanzishia hadi waikimbie nji
 
Wabunge wengi, wanajali maslahi binafsi kuliko ya wananchi wanaowaongoza. Ebu fikiria kuna mtumishi wa umma analipwa 15o,000 kwa mwezi, wewe Simbachawene unalipwa 7,500,000 kwa mwezi.

Bado unalalamika uongezewe, na bado kila siku mnapokea bahasha ili mpitishe bajeti feki, jamani muogopeni mungu.
Huyu mtumishi mdogo unategemea ataishi vipi kama sio kumkamua rushwa mwananchi wa kawaida atakaetaka huduma kutoka kwa huyu mtumishi wa umma?

Sidhani kama kuna mbunge ambae hana shughuli mbadala ya kumpatia kipato zaidi ya ubunge, na kama wapo hawazidi 30. Ebu tujiulize mtu kama Mohamed Dewji, Shabiby, Abood, Nchambi na wengine wengi, bado wanataka kuwakamua wapiga kura wao? Kwanza sidhani kama waliingia pale kwa ajili ya siasa?

Naona kuna haja ya sisi kuwahoji kama atatokea mbunge hana kazi nyingine zaidi ya ubunge tuwaorodheshe, wapewe shughuli mbadala ya kuwaongezea kipato chao kama ni lazima kufanya hivyo. kama wao wanaubiri ujasiliamali kwa nini wasianze wao.
 
Hivi hawa wabunge wanaoshangilia posho wana akili timamu kweli hawa?? Yaani wanaacha kutekeleza vitu vya msingi na badala yake wanadai posho, kwa kipi cha maana walichokifanya ikiwa watu wanakufa kwa njaa, dawa hospitalini hazipo, shule hazina walimu achilia mbali huduma kifisi fisi zilizopo na vyuo vyetu ndo kwanza vimejaa matatizo kila kukicha!! Umeme, mafuta na maji ni kero zinazoimbwa kila siku kama wimbo wa taifa alafu leo hii bila aibu limtu linadai kudhulumu kodi ya mwananchi wa kipato cha chini! Mafisadi wakubwa nyie, kila leo mnahubiri habari za ujasiriamali na kilimo kwanza mbona nyie hamuanzi?? Mnajenga mabar na mahotel makubwa kila kukicha tena kwa hela ya mtanzania akiwemo mama mjamzito aliyeenda kujifungua kwa mkokoteni umbali wa maili mia, hivi hamridhiki?? Bakhresa leo hii amekejeli jasho la mkulima, anagushi nyanya, vitunguu mpaka dafu na anauza tu, hivi mnategemea nini kwa huyu mkulima wa haya mazao?? Haya soko la mama ntilie nalo kaliteka anauza mpaka chapati na maandazi, jamani hivi hamyaoni haya??? Nyinyi ni viongozi gani ambao mmejaa mapengo hadi kwenye ubongo wenu?? Sasa ongezeni hiyo posho ili mzidi kunenepa vizuri na mtalaaniwa mpaka na vizazi vyenu vyote mkiongozwa na huyo mjomba wenu JK!!
 
Ee Baba Mungu tusaidie..
Serikali hatuna...
Mahakama hatuna...
Bunge nalo almost hatuna....
Mungu Ibariki Tanzania!
 
Nchi hii inahitaji overhauling. hakuna Serikali, Hakuna wabunge(Isipokuwa wapinzani), hakuna mahakama(wenyewe mmesikia ya hakimu mkazi Arusha). Nchi inaendeshwa kimjini mjini na wanaoindesha wote wanatumia masaburi. Bila nguvu ya umma hatutabadirika.
 
Huyu huyu simbachawene ndo alisema watu waliokufa nadhani nyamongo si kitu!
So siwezi mshangaa ni wa apa apa!
 
Kwa kweli inasikitisha mtu mzima kuongopa hadharani kuwa wanawasaidia wananchi majimboni mwao. Nakumbuka bunge la mwaka jana wabunge hao hao walikuwa wakiwaponda wananchi kuwa wanasumbua sana hadi spika Sita akasistizia ya kwamba mbunge kazi yake sio kugawa pesa kwa wananchi. Sasa leo wanaanziawapi kuwagawia na wananchi wote. Pia kumbuka mbunge hawezi kuleta maendeleo kwa kuwapa pesa wananchi bali kuwajengea miundombinu itakayowawezesha wao wenyewe kuwasiliana kwa urahisi! Nimekaa morogoro miaka sita sasa sijapataona hata siku moja mbunge kawapingisha mstari wananchi wasiojiweza kuwapa hata kilo moja ya unga ama sukuri.
 
Wengi wa wabunge hawajui nini kimewapeleka bungeni wengi wao wamekwenda kutafuta fedha siwezi kuwalaumu hawa nalaumu mfumo wa ccm kuchaguana kwa kigezo cha fedha , kujuana na... Ndio maana kuna wakina maji marefu , komba , idi azan ,shabibu etc wewe unategemea wataonge point za ukweli
 
Back
Top Bottom