Lengo la Serikali kutoa Ruzuku kwenye Mafuta Lilikuwa ni nini, kuwafaidisha wafanyabiashara au kupunguza gharama Kwa wananchi?

3 Angels message

JF-Expert Member
Aug 3, 2017
4,890
13,626
Serikali kupitia kwa waziri wake wa Nishati Mh Makamba ilitoa taarifa kwa umma kuwa kutokana na uhaba wa mafuta ambao ulipelekea nishati hiyo kupanda bei ilitarajia kutoa ruzuku ya bilioni 100 ili kupunguza athari ambazo zilitokana na kupanda kwa bei ya mafuta kama bei za usafiri, bei za bidhaa nk

Taarifa ya waziri ilikuwa wazi kuwa ruzuku hiyo ingelikuwa kwa kipindi cha mwezi mmoja ambao ni wa 6 pekee na kweli mwanzoni mwa mwezi huu ahadi hiyo ilitimia

Jambo ambalo ndiyo hoja ya uzi huu ni nini athari za ruzuku hiyo ambayo serikali imetoa ili hali mambo yako vilevile wakati wa bei ilivyopanda? Bei zilizotangazwa za nauli na Latra mbona bado zipo vilevile hata baada ya kutolewa kwa ruzuku? Bei za bidhaa nazo mbona zimebaki vilevile pia? Lengo la serikali lilikuwa kupunguza makali kwa wafanyabiashara peke yao tu na siyo kwa wananchi?

Au wafanyabiashara wameamua kuigomea serikali kutoshusha bei, au mamlaka husika zimeamua kuwa upande wa wafanyabiashara, waziri husika haoni pia?

Maana hata kwa akili ya kawaida tulitarajia kupungua hata kwa sh 10 tu lkn mpk leo tunaenda katikati ya mwezi hatusikii cha Latra kupunguza bei wala yeyote mambo yako vilevile shida iko wapi?
 
Miliki chombo cha moto ndio utajua kama mafuta yamepanda bei au yamepungua. Na punguzo hilo ni hizo fedha ambazo wapinzani wanasema ni kidogo,ziongezwe.
 
Miliki chombo cha moto ndio utajua kama mafuta yamepanda bei au yamepungua. Na punguzo hilo ni hizo fedha ambazo wapinzani wanasema ni kidogo,ziongezwe.
Kwani mpk nimiliki mkuu kutoka 3200 mpk 2970, 2994 si naona kuna kupungua
 
Serikali kupitia kwa waziri wake wa Nishati Mh Makamba ilitoa taarifa kwa umma kuwa kutokana na uhaba wa mafuta ambao ulipelekea nishati hiyo kupanda bei ilitarajia kutoa ruzuku ya bilioni 100 ili kupunguza athari ambazo zilitokana na kupanda kwa bei ya mafuta kama bei za usafiri, bei za bidhaa nk

Taarifa ya waziri ilikuwa wazi kuwa ruzuku hiyo ingelikuwa kwa kipindi cha mwezi mmoja ambao ni wa 6 pekee na kweli mwanzoni mwa mwezi huu ahadi hiyo ilitimia

Jambo ambalo ndiyo hoja ya uzi huu ni nini athari za ruzuku hiyo ambayo serikali imetoa ili hali mambo yako vilevile wakati wa bei ilivyopanda? Bei zilizotangazwa za nauli na Latra mbona bado zipo vilevile hata baada ya kutolewa kwa ruzuku? Bei za bidhaa nazo mbona zimebaki vilevile pia? Lengo la serikali lilikuwa kupunguza makali kwa wafanyabiashara peke yao tu na siyo kwa wananchi?

Au wafanyabiashara wameamua kuigomea serikali kutoshusha bei, au mamlaka husika zimeamua kuwa upande wa wafanyabiashara, waziri husika haoni pia?

Maana hata kwa akili ya kawaida tulitarajia kupungua hata kwa sh 10 tu lkn mpk leo tunaenda katikati ya mwezi hatusikii cha Latra kupunguza bei wala yeyote mambo yako vilevile shida iko wapi?
Wafanya maamuzi hawakuwa na uwezo wa kuwaza mpaka kufikia huko. Uwezo wao uliishia kwenye ..."tutashusha bei ya mafuta tar 1 june ". Kiukweli unapokuwa kiongozi unatakiwa uwe na uwezo wa juu kutatua changamoto tofauti na uwezo wa watu wengi. Tumepigwa
 
Wafanya maamuzi hawakuwa na uwezo wa kuwaza mpaka kufikia huko. Uwezo wao uliishia kwenye ..."tutashusha bei ya mafuta tar 1 june ". Kiukweli unapokuwa kiongozi unatakiwa uwe na uwezo wa juu kutatua changamoto tofauti na uwezo wa watu wengi. Tumepigwa
Kweli mkuu, maana baada ya tamko kule bungeni ilitakiwa mipango iwe imeshapangwa tayari ili ruzuku inapoingia basi tuone athari zake japo kidogo lkn wapi nauli zimebaki vilevile bidhaa nyingine ndiyo zinazidi kupanda tu sasa hivi
 
Hizi bei zitakuwa zinatimika DSM labda.

Mkoa ilikuwa 3400 na ruzuku imepunguza 120,kwa hiyo mabadiliko ya bei hayana impact yoyote kwa mlaji wa mwisho.

Ni siasa tu kama kawaida.
Yes mkuu ni bei za Dsm, kwa kweli ni siasa hakuna unafuu wowote ambao mwananchi ameupata
 
Kama nilimsikia vyema tena jana waziri alisema wataongeza tena 100b hizi za kwanza hatujaona unafuu hizi nyingine tena kuna watu wananufaika hapa
 
Kuna mambo yanantiririsha machozi, yani na hili pia serikali inahitaji rocket science kuling'amua?

Ipo wazi jamani mafuta yameshuka nauli ishuke...

Mibunge yetu nayo ipo tu inasifu na kuabudu so sad...
 
Serikali kupitia kwa waziri wake wa Nishati Mh Makamba ilitoa taarifa kwa umma kuwa kutokana na uhaba wa mafuta ambao ulipelekea nishati hiyo kupanda bei ilitarajia kutoa ruzuku ya bilioni 100 ili kupunguza athari ambazo zilitokana na kupanda kwa bei ya mafuta kama bei za usafiri, bei za bidhaa nk

Taarifa ya waziri ilikuwa wazi kuwa ruzuku hiyo ingelikuwa kwa kipindi cha mwezi mmoja ambao ni wa 6 pekee na kweli mwanzoni mwa mwezi huu ahadi hiyo ilitimia

Jambo ambalo ndiyo hoja ya uzi huu ni nini athari za ruzuku hiyo ambayo serikali imetoa ili hali mambo yako vilevile wakati wa bei ilivyopanda? Bei zilizotangazwa za nauli na Latra mbona bado zipo vilevile hata baada ya kutolewa kwa ruzuku? Bei za bidhaa nazo mbona zimebaki vilevile pia? Lengo la serikali lilikuwa kupunguza makali kwa wafanyabiashara peke yao tu na siyo kwa wananchi?

Au wafanyabiashara wameamua kuigomea serikali kutoshusha bei, au mamlaka husika zimeamua kuwa upande wa wafanyabiashara, waziri husika haoni pia?

Maana hata kwa akili ya kawaida tulitarajia kupungua hata kwa sh 10 tu lkn mpk leo tunaenda katikati ya mwezi hatusikii cha Latra kupunguza bei wala yeyote mambo yako vilevile shida iko wapi?

Lengo ni kupiga pesa maana ni rahis kudhibiti na kushusha bei na ni endelevu kwa kupunguza kodi lakini ni ngumu kuidhiti ruzuku na ku menten bei kwa muda mrefu kwasababu ruzuku inaingia kwenye mifuko ya watu halafu wao watajua namna ya kuila eidha wale sana mpaka kuvimbiwa au wale kidogo kutokana na urefu wa kamba
 
Nadhani watawala wanafanya haya makusudi wakijua wananchi siyo wafuatiliaji wala hawajali. Lakini katika hili tumepigwa waziwazi
 
Serikali kupitia kwa waziri wake wa Nishati Mh Makamba ilitoa taarifa kwa umma kuwa kutokana na uhaba wa mafuta ambao ulipelekea nishati hiyo kupanda bei ilitarajia kutoa ruzuku ya bilioni 100 ili kupunguza athari ambazo zilitokana na kupanda kwa bei ya mafuta kama bei za usafiri, bei za bidhaa nk

Taarifa ya waziri ilikuwa wazi kuwa ruzuku hiyo ingelikuwa kwa kipindi cha mwezi mmoja ambao ni wa 6 pekee na kweli mwanzoni mwa mwezi huu ahadi hiyo ilitimia

Jambo ambalo ndiyo hoja ya uzi huu ni nini athari za ruzuku hiyo ambayo serikali imetoa ili hali mambo yako vilevile wakati wa bei ilivyopanda? Bei zilizotangazwa za nauli na Latra mbona bado zipo vilevile hata baada ya kutolewa kwa ruzuku? Bei za bidhaa nazo mbona zimebaki vilevile pia? Lengo la serikali lilikuwa kupunguza makali kwa wafanyabiashara peke yao tu na siyo kwa wananchi?

Au wafanyabiashara wameamua kuigomea serikali kutoshusha bei, au mamlaka husika zimeamua kuwa upande wa wafanyabiashara, waziri husika haoni pia?

Maana hata kwa akili ya kawaida tulitarajia kupungua hata kwa sh 10 tu lkn mpk leo tunaenda katikati ya mwezi hatusikii cha Latra kupunguza bei wala yeyote mambo yako vilevile shida iko wapi?
Hawa watu wanaotuongoza Ni wa pwani so hawana maumivu na mafuta kupanda. Wao yanachukuliwa hapo hapo bandarini. Kumbuka hawana machungu na huku bara.
 
Na watu wa usafiri wa umma nao wamejitoa ufahamu as if nothing has happened
Mkuu wao hawawezi kushusha bila maelezo kutoka Latra kipindi kile bei zimepanda za mafuta walivumilia kwa bei ya awali mpk Latra walivyopandisha tulitegemea baada ya ruzuku ya serikali Latra waact fast ktk kutoa bei mpya kulingana na ruzuku ila mpk leo mwezi unaelekea mwisho hakuna mabadiliko ruzuku imeenda na unafuu hatujauona
 
Back
Top Bottom