Lengo la Rais Magufuli kuzuia makinikia ni ili Smelter inunuliwe hapa nchini. Prof. Muhongo alifukuzwa uwaziri kwa kushindwa kununua Smelter

G Sam

JF-Expert Member
Apr 20, 2013
11,555
35,880
Nikukumbushe tu Rais Magufuli mwaka 2017 wakati unapokea taarifa ya Prof. Mruma lalamiko lako kubwa sana na hata watanzania wakakuamini (Isipokuwa mimi) ni kuhusu kuchenjulia makinikia nje ya nchi.

Nakumbuka sana ulimlaumu sana Prof. Muhongo ukafikia hatua yakumwambia kuwa Prof. mwenzake yaani Mruma amem prove wrong kwa ripoti aliyowasilisha. Hatimaye Prof. Muhongo ukamtengua uwaziri huku Simbachawene aliyekuwa TAMISEMI akajiuzulu eti kulinda heshima yake kwakuwa alikuwa msaidizi wa Muhongo enzi ya Kikwete.

Nakumbuka sana ulimlaumu sana Prof. Muhongo kwa kile ulichodai eti amekaa kwenye hiyo wizara kwa muda mrefu bila kushauri serikali inunue Smelter na hivyo ukamuona hafai anashirikiana na mabeberu. Kikubwa ulitueleza pia kuwa kuna madini mengine yanaibiwa yakienda huko kuchenjuliwa hayawepewi thamani hivyo kinachothaminiwa ni gold pekee.

Kama kawaida yetu mawakala wa mabeberu tukaja na threads zetu humu tukielezea ugumu wa Smelter unayotaka iwepo hapa nchini. Kwakuwa wakati Prof. Mruma anawasilisha ile ripoti yake ilifikia hatua akawa anatokwa na machozi basi sisi mawakala tulipopolewa mawe kweli kweli. Hakuna mzalendo ambaye angetuelewa wakati ule.

Leo miaka miwili imepita, umesaini makubaliano ya hovyo hovyo kuwahi kutokea, ACACIA wamepata mgao wao bila kwenda mahakamani. Barrick anapeleka makinikia nje kuyachenjua kiulaini kabisa na mambo yanaendelea vyema huku Barrick akipiga bao la nguvu.

Sisi tunakuuliza kuwa, lengo lako hasa lilikuwa ni lipi? Au ulikuwa tu hulipendi jina ACACIA? Lilikukosea nini?

NB. Watanzania subirini hayo makubaliano yaje kuwekwa wazi ila kimsingi muliowaona kuwa wana akili hawajafanya kitu zaidi ya kupoteza muda na kuingia hasara.
 
Prof Muhongo aliteuliwa ili afukuzwe.

Lengo la kuteuliwa kwake lilikuwa ni kuwaficha Homeboy Medard Kalemani ( alietulizwa kwa muda kama NW ) na Dotto Biteko.

Dotto Biteko na Medard Kalemani ( Huyu Kaachiwa Jimbo na Jiwe ) kama wangeliteuliwa directly kwenye MADINI watu wangepiga kelele sana.
 
Mkuu kaisikilize kwa umakini speech ya Mark Bristol, Mzaliwa wa africa ya kusini mwenye asili ya uyahudi, kasema yeye ni mwafrica halisi tena mzulu, alimaanisha kuwa africa tunapaswa kuwa wamoja yanapokuja maslahi ya africa. isingelikuwa kukomaa kwa magufuli Mark asingekuwa ceo wa barrick, na Mark asingekomaa na Geleta tusingepata huyu mtoto twiga minerals, na huu ndio ushirikiano wa kikanda akasema, either we win together or we loose together na hii ndio africa mpya chini ya magufuli. Umeelewa?
 
Mkuu kaisikilize kwa umakini speech ya Mark Bristol, Mzaliwa wa africa ya kusini mwenye asili ya uyahudi, kasema yeye ni mwafrica halisi tena mzulu, alimaanisha kuwa africa tunapaswa kuwa wamoja yanapokuja maslahi ya africa. isingelikuwa kukomaa kwa magufuli Mark asingekuwa ceo wa barrick, na Mark asingekomaa na Geleta tusingepata huyu mtoto twiga minerals, na huu ndio ushirikiano wa kikanda akasema, either we win together or we loose together na hii ndio africa mpya chini ya magufuli. Umeelewa?
Kwahiyo Mark kwa kusema vile umemwamini kweli kabisa? Yani mtu aaminiwe kuongoza Barrick Afrika kisha aje kuangalia maslahi ya watanzania? Kiukweli wana CCM wengi sana huwa tunafeli hapa! Kuamini kuwa kiongozi wa serikali au mtu akiongelea upande wetu kwa uchungu na kujipiga piga kifua basi huyo na baba wa kweli. Tujifunze kutoka nje ya miili yetu ya asili ili tujue mengi zaidi.

Yani kweli kwa ulichoandika nimekudharau kabisa! Kwamba kwakuwa jamaa alijiita mwafrika basi kwako amemaliza kila kitu? Shame!
 
Magufuli ana matatizo makubwa mawili

1. Anadhani yeye ni mjuzi wa kilakitu
2. Anataka kuambiwa kile kinachoendana na mawazo yake tu, vinginevyo wewe mshauri utaitwa hauna 'uzalendo'

Juu ya hayo, kuna tatizo moja dogo,
Anawaamini sana TISS utadhani ni malaika, wakimpelekea viripoti vya siri basi yeye anaona kila kilichomo humo ni 'fact' kumbe wakati mwingine ni madudu matupu.
muhuri wa SIRI hauifanyi taarifa kuwa iliyosheheni facts.

Matokeo yake ni washauri wake wenye uelewa mkubwa wa baadhi ya mambo wanaamua kukaa kimya au kushauri vile anavyopenda mshauriwa.

Lissu aliita ripoti ya akina prof Mruma kuwa ni 'professional rubish' watu wakanuna kwelikweli, alikua sahihi kwa 100%
 
Mkuu kaisikilize kwa umakini speech ya Mark Bristol, Mzaliwa wa africa ya kusini mwenye asili ya uyahudi, kasema yeye ni mwafrica halisi tena mzulu, alimaanisha kuwa africa tunapaswa kuwa wamoja yanapokuja maslahi ya africa. isingelikuwa kukomaa kwa magufuli Mark asingekuwa ceo wa barrick, na Mark asingekomaa na Geleta tusingepata huyu mtoto twiga minerals, na huu ndio ushirikiano wa kikanda akasema, either we win together or we loose together na hii ndio africa mpya chini ya magufuli. Umeelewa?
Huyu mpuuzi G Sam hawezi kukuelewa ! Ni kuwaacha waandike pumba zao
 
Magufuli ana matatizo makubwa mawili

1. Anadhani yeye ni mjuzi wa kilakitu
2. Anataka kuambiwa kile kinachoendana na mawazo yake tu, vinginevyo wewe mshauri utaitwa hauna 'uzalendo'
3. Anawaamini sana TISS utadhani ni malaika, wakimletea viripoti vya siri basi yeye anaona kila kilichomo humo ni 'fact' kumbe wakati mwingine ni madudu matupu.

Matokeo yake ni washauri wake wenye uelewa mkubwa wa baadhi ya mambo wanaamua kukaa kimya au kushauri vile anavyopenda mshauriwa.

Lissu aliita ripoti ya akina prof Mruma kuwa ni 'professional rubish' watu wakanuna kwelikweli, alikua sahihi kwa 100%
Na mwaka huku kuna mtu anaenda kufanya politiko mastabeshen
 
!
Mkuu kaisikilize kwa umakini speech ya Mark Bristol, Mzaliwa wa africa ya kusini mwenye asili ya uyahudi, kasema yeye ni mwafrica halisi tena mzulu, alimaanisha kuwa africa tunapaswa kuwa wamoja yanapokuja maslahi ya africa. isingelikuwa kukomaa kwa magufuli Mark asingekuwa ceo wa barrick, na Mark asingekomaa na Geleta tusingepata huyu mtoto twiga minerals, na huu ndio ushirikiano wa kikanda akasema, either we win together or we loose together na hii ndio africa mpya chini ya magufuli. Umeelewa?
Hamna kitu kinaitwa win together kwa mapebari...hiyo ni siasa tu kuonyesha tuko pamoja ila tutaendelea kupigwa tuu.
 
Prof Muhongo aliteuliwa ili afukuzwe.

Lengo la kuteuliwa kwake lilikuwa ni kuwaficha Homeboy Medard Kalemani ( alietulizwa kwa muda kama NW ) na Dotto Biteko.

Dotto Biteko na Medard Kalemani ( Huyu Kaachiwa Jimbo na Jiwe ) kama wangeliteuliwa directly kwenye MADINI watu wangepiga kelele sana.
Na huu uliosema ndo sababu kuu ya kumuondoa Muhongo,tuna Raisi mpuuzi sana
 
Nikukumbushe tu Rais Magufuli mwaka 2017 wakati unapokea taarifa ya Prof. Mruma lalamiko lako kubwa sana na hata watanzania wakakuamini (Isipokuwa mimi) ni kuhusu kuchenjulia makinikia nje ya nchi.

Nakumbuka sana ulimlaumu sana Prof. Muhongo ukafikia hatua yakumwambia kuwa Prof. mwenzake yaani Mruma amem prove wrong kwa ripoti aliyowasilisha. Hatimaye Prof. Muhongo ukamtengua uwaziri huku Simbachawene aliyekuwa TAMISEMI akajiuzulu eti kulinda heshima yake kwakuwa alikuwa msaidizi wa Muhongo enzi ya Kikwete.

Nakumbuka sana ulimlaumu sana Prof. Muhongo kwa kile ulichodai eti amekaa kwenye hiyo wizara kwa muda mrefu bila kushauri serikali inunue Smelter na hivyo ukamuona hafai anashirikiana na mabeberu. Kikubwa ulitueleza pia kuwa kuna madini mengine yanaibiwa yakienda huko kuchenjuliwa hayawepewi thamani hivyo kinachothaminiwa ni gold pekee.

Kama kawaida yetu mawakala wa mabeberu tukaja na threads zetu humu tukielezea ugumu wa Smelter unayotaka iwepo hapa nchini. Kwakuwa wakati Prof. Mruma anawasilisha ile ripoti yake ilifikia hatua akawa anatokwa na machozi basi sisi mawakala tulipopolewa mawe kweli kweli. Hakuna mzalendo ambaye angetuelewa wakati ule.

Leo miaka miwili imepita, umesaini makubaliano ya hovyo hovyo kuwahi kutokea, ACACIA wamepata mgao wao bila kwenda mahakamani. Barrick anapeleka makinikia nje kuyachenjua kiulaini kabisa na mambo yanaendelea vyema huku Barrick akipiga bao la nguvu.

Sisi tunakuuliza kuwa, lengo lako hasa lilikuwa ni lipi? Au ulikuwa tu hulipendi jina ACACIA? Lilikukosea nini?

NB. Watanzania subirini hayo makubaliano yaje kuwekwa wazi ila kimsingi muliowaona kuwa wana akili hawajafanya kitu zaidi ya kupoteza muda na kuingia hasara.
Haya tumekusikia!
 
!
Hamna kitu kinaitwa win together kwa mapebari...hiyo ni siasa tu kuonyesha tuko pamoja ila tutaendelea kupigwa tuu.
Hawa jamaa wa CCM wakishaona Magufuli kakubali kitu basi ni Mungu kapitisha. Yani myahudi akusainie documents halafu akupongeze na wewe ucheke? Muda utaongea tena kama jinsi ambavyo umeongea!
 
Back
Top Bottom