Kilasi Mkuu
JF-Expert Member
- Nov 25, 2013
- 2,325
- 719
Katika hali ambayo ujio wa Lembeli umezidi kufichua madudu ya CCM,tuna elezwa Mafisadi wa CCM walitaka kumhonga Lembeli afiche uhalifu huo.
Hayo tume ya sikia katika taarifa ya habari ya ITV wakiwa Bunda wakijitambulisha.
Kimsingi huyu mzee alikuwa anaonekana hata akiwa huko huko CCM kuwa hayuko radhi kukubaliana na mambo yao.
Hayo tume ya sikia katika taarifa ya habari ya ITV wakiwa Bunda wakijitambulisha.
Kimsingi huyu mzee alikuwa anaonekana hata akiwa huko huko CCM kuwa hayuko radhi kukubaliana na mambo yao.
Katika wanasiasa ambao nimekuwa nikiwakubali na kuwaheshimu yupo lembeli, bulaya, filikunjombe, kangi lugola na wengineo.
Ambao pamoja na kuwa wapo CCM wamekuwa mstari wa mbele kujitenga na masuala yanayohusu ufisadi mara zote.
Na pamoja na kujitenga kwa kutojihusisha lakini wamekuwa ni wakemeaji wakubwa wa ufisadi ndani ya bunge. Kati ya hao nilimuengua kangi lugola ambaye kwenye escrow alidiriki hata kuvaa 'ninja' ili aiite 'spedi spedi' bila haya. Jambo lililokuja kunishangaza alipopita mitaani kifua mbele kumnadi lowassa.
Na kusahau kuwa naye ni mmoja watu waliosemwa kujihusisha na masuala ambayo amekuwa akiyapinga. Nilipoona hivi huyu nikamdelete kabisa kwenye orotha yangu ya majembe. Sasa kabla sijakaa sawa nikasikia kuwa lembeli na bulaya wamehama.
Sikushtuka ni uamuzi wa kidemokrasia lililonishangaza ni kumsikia lembeli akisema kuwa alikataa 50 milioni ya hongo akiwa CCM kwenye kufichua moja ya maovu katika operesheni tokomeza.
Swali ni je, ameamua kusema kwasababu ametoka? Je, aliogopa kusema kabla hajatoka? Je, siku akitoka chadema atasema mangapi ya ndani ya chama?