Petro E. Mselewa
JF-Expert Member
- Dec 27, 2012
- 10,175
- 25,446
Mbunge wa Kahama,mkoani Shinyanga,James Lembeli amewashtaki wamiliki wa magazeti matatu pamoja na Wahariri wake kwa madai ya kukashifiwa. Kashfa husika ni kuhusu yeye na Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu kudaiwa kupanga kuhamisha uendeshaji wa Mbuga ya Wanyama ya Katavi kutoka TANAPA na kuikabidhi kwa Kampuni ya kigeni ya APN.
Nyaraka za kimahakama zinaonyesha kuwa Lembeli amefungua kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,Dar es Salaam. Nyaraka husika zinawataja wadaiwa kuwa ni pamoja ya magazeti ya Fahamu, Raia Tanzania na Jamhuri.Pia,Wahariri wa magazeti hayo matatu ni Wadaiwa. Kama hiyo haitoshi, Manyerere Jackton (Jamhuri), Kundaeli Kwamaya(Fahamu) na Joseph Petro nao ni Wadaiwa katika kesi hiyo.
Katika kesi hiyo,Lembeli anataka kuombwa radhi na kulipwa fidia kwa madai ya kudhalilishwa na kuvunjiwa hadhi yake.Kesi husika bado haijapangiwa Hakimu wa kuisikiliza.
Chanzo: ----- la tarehe 22-28/5/2014, ukurasa wa 3
Nyaraka za kimahakama zinaonyesha kuwa Lembeli amefungua kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,Dar es Salaam. Nyaraka husika zinawataja wadaiwa kuwa ni pamoja ya magazeti ya Fahamu, Raia Tanzania na Jamhuri.Pia,Wahariri wa magazeti hayo matatu ni Wadaiwa. Kama hiyo haitoshi, Manyerere Jackton (Jamhuri), Kundaeli Kwamaya(Fahamu) na Joseph Petro nao ni Wadaiwa katika kesi hiyo.
Katika kesi hiyo,Lembeli anataka kuombwa radhi na kulipwa fidia kwa madai ya kudhalilishwa na kuvunjiwa hadhi yake.Kesi husika bado haijapangiwa Hakimu wa kuisikiliza.
Chanzo: ----- la tarehe 22-28/5/2014, ukurasa wa 3
Last edited by a moderator: