Lembeli ashtaki magazeti

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,175
25,446
Mbunge wa Kahama,mkoani Shinyanga,James Lembeli amewashtaki wamiliki wa magazeti matatu pamoja na Wahariri wake kwa madai ya kukashifiwa. Kashfa husika ni kuhusu yeye na Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu kudaiwa kupanga kuhamisha uendeshaji wa Mbuga ya Wanyama ya Katavi kutoka TANAPA na kuikabidhi kwa Kampuni ya kigeni ya APN.

Nyaraka za kimahakama zinaonyesha kuwa Lembeli amefungua kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,Dar es Salaam. Nyaraka husika zinawataja wadaiwa kuwa ni pamoja ya magazeti ya Fahamu, Raia Tanzania na Jamhuri.Pia,Wahariri wa magazeti hayo matatu ni Wadaiwa. Kama hiyo haitoshi, Manyerere Jackton (Jamhuri), Kundaeli Kwamaya(Fahamu) na Joseph Petro nao ni Wadaiwa katika kesi hiyo.

Katika kesi hiyo,Lembeli anataka kuombwa radhi na kulipwa fidia kwa madai ya kudhalilishwa na kuvunjiwa hadhi yake.Kesi husika bado haijapangiwa Hakimu wa kuisikiliza.

Chanzo: ----- la tarehe 22-28/5/2014, ukurasa wa 3
 
Last edited by a moderator:
Nilimuonya Manyerere Jackton aache kuchafua watu kwa tuhuma za uongo.Ngoja atakuja hapa kujitetea na kujisafisha kwa style atakayoona inafaa
 
Last edited by a moderator:
Hayo magezeti ni ya ukawa ameliacha pia lile la toilet pepa Tanzania daima
 
Nilimuonya Manyerere Jackton aache kuchafua watu kwa tuhuma za uongo.Ngoja atakuja hapa kujitetea na kujisafisha kwa style atakayoona inafaa

ben saanane wewe ni mchumia tumbo tu unashnda chadema unakula kwa membe dtail zako zpo ata chadema wameshakushtukia huna ubavu au gaut za kumshauri mwandshi makn kama manyerere nan hajui kua ishu ya kuuza katavi national park kwa kampun ambayo nyalandu na lembeli na yalandu ni board of directors mpango ulkua umefchwa akauibua manyerere akna nyalandu na lembeli wakafeli? wewe uzalendo wako upo wapi si bora ya kna zto kulko wewe njaa mbaya sana...membe+Nyalandu=Lembeli wote hao walkua wachumia tumbo kwa mengi hawawezi kutengana nyalandu na lembeli....now days lembeli kawa fsadi kahongwa pesa na nyalandu na wenye vtalu..lembeli anasafr kwenda maonyesho ya utalii I.e Germany anashnda hotelini wiki mbili bila kaz fsadi mkubwa...alafu leo ben saanane unamtetea lembeli acha ufsad na njaa ben
 
Last edited by a moderator:
ben saanane wewe ni mchumia tumbo tu unashnda chadema unakula kwa membe dtail zako zpo ata chadema wameshakushtukia huna ubavu au gaut za kumshauri mwandshi makn kama manyerere nan hajui kua ishu ya kuuza katavi national park kwa kampun ambayo nyalandu na lembeli na yalandu ni board of directors mpango ulkua umefchwa akauibua manyerere akna nyalandu na lembeli wakafeli? wewe uzalendo wako upo wapi si bora ya kna zto kulko wewe njaa mbaya sana...membe+Nyalandu=Lembeli wote hao walkua wachumia tumbo kwa mengi hawawezi kutengana nyalandu na lembeli....now days lembeli kawa fsadi kahongwa pesa na nyalandu na wenye vtalu..lembeli anasafr kwenda maonyesho ya utalii I.e Germany anashnda hotelini wiki mbili bila kaz fsadi mkubwa...alafu leo ben saanane unamtetea lembeli acha ufsad na njaa ben

Leta ushahidi hapa maana na mimi naweza kusema umetumwa na yule Mwenyekiti njaa wa CCM wa Huko Shinyanga.Mbona hao wote uliowataja kwa kutoa povu ndio wazalendo?

Hatutaki waandishi wanatumikia Mafisadi na kuchafua watu kwa uongo.

Kuna waandishi wa Habari ambao nawaheshimu sana lakini ukifikia hatua ya kuandika mambo ya uongo hadharani inatia shaka
 
Mbunge wa Kahama,mkoani Shinyanga,James Lembeli amewashtaki wamiliki wa magazeti matatu pamoja na Wahariri wake kwa madai ya kukashifiwa. Kashfa husika ni kuhusu yeye na Waziri wa Maliasili na Utalii,Lazaro Nyalandu kudaiwa kupanga kuhamisha uendeshaji wa Mbuga ya Wanyama ya Katavi kutoka TANAPA na kuikabidhi kwa Kampuni ya kigeni ya APN.

Nyaraka za kimahakama zinaonyesha kuwa Lembeli amefungua kesi hiyo katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu,Dar es Salaam. Nyaraka husika zinawataja wadaiwa kuwa ni pamoja ya magazeti ya Fahamu, Raia Tanzania na Jamhuri.Pia,Wahariri wa magazeti hayo matatu ni Wadaiwa. Kama hiyo haitoshi, Manyerere Jackton (Jamhuri), Kundaeli Kwamaya(Fahamu) na Joseph Petro nao ni Wadaiwa katika kesi hiyo.

Katika kesi hiyo,Lembeli anataka kuombwa radhi na kulipwa fidia kwa madai ya kudhalilishwa na kuvunjiwa hadhi yake.Kesi husika bado haijapangiwa Hakimu wa kuisikiliza.

Chanzo: ----- la tarehe 22-28/5/2014, ukurasa wa 3
Mtoa mada hebu waulize mods mbona jina la chanzo cha habari yako wamekifuta? Hivi kuna tatizo gani kutaja chanzo hicho wakati kipo kihalali na kinapatikana kwenye meza za magazeti. Kuna tatizo hapa JF ambalo mimi silielewi ambapo baadhi ya magazeti hata ukiyataja tu katika habari yako au uchangiaji wako hayaandikwi majina yake. Mojawapo lianaanza na M na kuishia na O (Ambalo ndilo nadhani ndio chanzo cha uzi wako hata mimi kuliandika lote nimeacha kwasababu nitakuwa napoteza nguvu na muda bure) na jingine nadhani ni mama yake na hilo nililotaja herufi zake linaanza na MW na kuishia na SI. Hili limefungiwa kwa muda usiojulikana lakini nalo sababu ya lenyewe kutoandikwa JF siijui labda wamepewa maagizo maalumu na serikali wasiyataje. Watueleimishe kwanini wanafanya hivyo!
 
Ben saanane mchumia tumbo weye, huna lolote, chadema watakutema siku si nyingi. Nyalandu hana lolote, ana kashifa za kuhujumu uchumi wa tanzania wa kuuza mbuga na vitalu, nyalandu ni gaidi namba moja kwenye hii nchi, ameuza vitalu vyote na wanyama wanauliwa na kuwindwa kwa idhini yake
 
Mtoa mada hebu waulize mods mbona jina la chanzo cha habari yako wamekifuta? Hivi kuna tatizo gani kutaja chanzo hicho wakati kipo kihalali na kinapatikana kwenye meza za magazeti. Kuna tatizo hapa JF ambalo mimi silielewi ambapo baadhi ya magazeti hata ukiyataja tu katika habari yako au uchangiaji wako hayaandikwi majina yake. Mojawapo lianaanza na M na kuishia na O (Ambalo ndilo nadhani ndio chanzo cha uzi wako hata mimi kuliandika lote nimeacha kwasababu nitakuwa napoteza nguvu na muda bure) na jingine nadhani ni mama yake na hilo nililotaja herufi zake linaanza na MW na kuishia na SI. Hili limefungiwa kwa muda usiojulikana lakini nalo sababu ya lenyewe kutoandikwa JF siijui labda wamepewa maagizo maalumu na serikali wasiyataje. Watueleimishe kwanini wanafanya hivyo!

Hata mimi nikiandika m..wio inakataa,-----
 
habari zinazoandikwa na manyerere huwa zimefanyiwa uchunguzi wa kina
 
Hata mimi nikiandika m..wio inakataa,-----
Mbona lipo kihalali na linapatikana mitaani kwanini JF wanalinyanyapaa? Kuna neno ambalo ni la kiswahili sanifu na sio tusi ambalo aliambiwa yule mkubwa fulani aliyemrisha vyombo vya dola kupiga raia ukiliandika linakataa. Neno lenyewe ni Mpmbvu ambapo likiandikwa kwa usahihi linakataa wakati ni neno sanifu na sio tusi. Nafikiri kuna tatizo la uelewa na ushabidiki wa kisiasa kwa wahusika miongoni mwa mods. Kuna maneno mengine mazito zaidi ya hayo yanaandikwa humu lakini huwa hayaondolewi sijui kwanini wayaondoe majina ya magazeti na hilo neno aliloambiwa mkubwa yule mjinga. Maneno kama Mhuni, mjinga, mpmbvu, mwendawazimu, zuzu, mlevi, nk alikuwa anyatumia sana baba wa taifa kuelezea tabia mbali mbali za viongozi wasiokuwa na sifa za uongozi thabiti. Mods: Wake up!
 
Hakuna mwana ccm msafi hata mmoja... Niliwahi kumuamini Samuel 6, lakin ghafla nimechefukwa naye sitaki hata kumwona... Gazeti la kuchomoza jua halinaga huruma na dhambi...
 
Ben Saa 8 ameacha kazi ya kumlea Juniour Slaa , naona anatafuta kazi ya uyaya kwa faraja kota ( Mke wa nyalandu) haka kajamaa ni kandumila kuwili balaa.
 

Attachments

  • APN.JPG
    APN.JPG
    310.7 KB · Views: 128
Salaam kwa mnafiki Ben Sanane

Kuna mnafiki zaidi yako..Leta ushahidi wa yale Madai yako kuhusu Mkakati wa Ben Saanane na Tundu Lissu ndani ya CHADEMA. kwenye uongozi wa chama kwanza.Miezi sita inakaribia kupita lakini Upo kimya tangu nikwambie uweke ushahidi hapa
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom