zinc
JF-Expert Member
- May 24, 2013
- 1,392
- 1,066
Ndugu wana JF,
Katika kongamano la BAVICHA tulijadili miaka 52 ya uhuru pale eneo la Landmark hotel, Kamanda Lema alitoa hotuba yake fupi na yenye ujasiri na ya kuvutia sana.
Alitusihi na kutuhasa sana vijana wa leo kutokuwa na uwoga, Kamanda Lema alitueleza kwamba hata kama ni mtoto wake anamwosia kabla hajaondoka duniani hawezi kumueleza mtoto wake asome sana, bali atamueleza kwamba "HAKUNA DHAMBI MBAYA NA KUBWA DUNIANI KAMA WOGA".
Vijana wengi tulifurahi sana kwani kuna wasomi wengi ambao wamefanya mambo mabaya na ya kufedhehesha katika taifa, pia akatoa angalizo kuhusu Red brigade na Chadema vijana kwamba ni wakati wa kumlinda katibu mkuu wetu wa Chadema ambaye ni Dr Slaa, alihitimisha kwa kusema huu ubabe wa kijinga tunaofanyiwa na magamba tumechoshwa nao, sasa hatuwezi kuuvumilia kwa kuwa hata sisi (Chadema) tunaweza ubabe kwani "UBABE SIO DHAMBI INATEGEMEA UBABE HUO UNAUFANYIA WAPI".
Hapa ndipo napozidi kumkubali Kamanda Lema.
Katika kongamano la BAVICHA tulijadili miaka 52 ya uhuru pale eneo la Landmark hotel, Kamanda Lema alitoa hotuba yake fupi na yenye ujasiri na ya kuvutia sana.
Alitusihi na kutuhasa sana vijana wa leo kutokuwa na uwoga, Kamanda Lema alitueleza kwamba hata kama ni mtoto wake anamwosia kabla hajaondoka duniani hawezi kumueleza mtoto wake asome sana, bali atamueleza kwamba "HAKUNA DHAMBI MBAYA NA KUBWA DUNIANI KAMA WOGA".
Vijana wengi tulifurahi sana kwani kuna wasomi wengi ambao wamefanya mambo mabaya na ya kufedhehesha katika taifa, pia akatoa angalizo kuhusu Red brigade na Chadema vijana kwamba ni wakati wa kumlinda katibu mkuu wetu wa Chadema ambaye ni Dr Slaa, alihitimisha kwa kusema huu ubabe wa kijinga tunaofanyiwa na magamba tumechoshwa nao, sasa hatuwezi kuuvumilia kwa kuwa hata sisi (Chadema) tunaweza ubabe kwani "UBABE SIO DHAMBI INATEGEMEA UBABE HUO UNAUFANYIA WAPI".
Hapa ndipo napozidi kumkubali Kamanda Lema.