Lema na Nassary Walitikisa Bunge kipindi cha Maswali kwa Waziri Mkuu..

Jembe langu lema mungu yuko nawewe usiogope mtangulize yeye utaya shinda yote yupo akutiae nguvu rais wa arusha soma zaburi 121 mstari wa 1 mpaka wa 2 mungu yko kazini
 
Hakuna walichotikisa mbona, hilo swali wameambiwa waandike kwa maandishi sio wanabwabwaja tu kama wameshapiga gongo zao asubui.
..lazima tukukaushe tu mtimbichi,hii ngoma inaitwa force kingi,pm kawekwa mtu kati mpaka kachemka,chezeya cdm weye...!!
 
Dhana za siasa za kijinga zilizopitwa na wakati!
Mnatafuta mbinu mbaya mpaka mnauwa Watu ili mkidhohofishe Chama Fulani! Haipendezi ata siku moja!
Watumikieni wananchi Kwa haki mtapendwa!

Kumwaga damu walianza zamani sana ili kukiokoa chama, unamkumbuka Korimba na Kombe?
 
Ni sawa na nyie Yule jamaa yenu aliekua anatembea na Yule muathirika Wa tindikali kuuaminisha umma Kua ni matendo ya upinzani!

Siasa za kijinga kabisa!

Kilewo ndio anatuhumiwa kuhusika na lile tukio na tayari keshapanda kizimbani na kesi inaendelea kuunguruma.
 
Kilewo ndio anatuhumiwa kuhusika na lile tukio na tayari keshapanda kizimbani na kesi inaendelea kuunguruma.


Jiulize! Ni kesi Ngapi ambazo mmewafungulia wapinza ziwe za kubambika Au za kweli mlizozishinda? Ata ya Huyo Kilewo mtashindwa!

Au niambie ni Kiongozi gani Au mbuge gani Wa upinzani mliwahi kumshinda mahakani? Hii inaonesha kesi nyingi si halali na Ndo maana hamshindi!
 
Hiivi LiverpoolFC, Arushaone, sweetlady, Passion Lady, Preta mmepona nyie huko na hilo bomu maana ni kali sana
Swala la Mabomu ya Soweto na Olasit laibuka tena bungeni, baada ya Kijana aliyebambikizwa kesi na kuteswa akilazimishwa kumtaja Lema kuwa ndo aliyemtuma kulipua mabomu hayo! Kijana yupo Bungeni tayari kumwaga ushahidi wake. Waziri mkuu amekosa majibu asema wampelekee katika maandishi.

Baada ya mbunge wa Arusha mjini Godbless Lema kukoswakoswa na bomu la Soweto yeye na Mwenyekiti wa chadema Freeman Mbowe na kuua Watoto wadogo (3) na kiongozi wa chadema (1) na kuacha makumi bila viungo kama miguu, mikono. Sasa jeshi la polisi kwa kushirikiana na Mwigulu Nchemba liko kwenye harakati za kumubambikia Mhe. Lema kuwa yeye ndiyo aliyetuma mtu kwenda kulipua bomu kwenye kanisa la Olasti (St. Joseph Moyo safi) bahati mbaya sana kwa CCM na jeshi lake na bahati mzuri Kwa mhe. Lema na Chadema ni kuwa kijana huyo aligoma kabisa kusema/kutenda dhambi hiyo ya kusema uongo licha ya kwamba aliwahi kugombana na Mhe. Lema na akawaambia nina ugomvi na Lema lakini siwezi kumsingizia kitu kama hicho kijana huyo aliminywa sehemu za siri na kutishwa lakini alisimamia msimamo wake huo na akawaambia wakati wa mlipuko huo kijana(Nico) alikuwa gerezani kwa kesi nyingine.. Ndipo jeshi la polisi kwa aibu wakamwachia kijana huyo kwasasa yuko bungeni na alikuwa tayari kutoa maelezo hayo...

Lakini Waziri mkuu alimtaka Nasari akaandike maelezo ili ampelekee, kasimama Godbless Lema kukazia swali hilo Makinda akamwambia hairuhusiwi kurudia swali Lema akasema ana masikitiko makubwa kuwa yeye baada ya kukoswakoswa sasa anaandaliwa kesi ya kulazimishwa kuwa yeye alituma watu kuja kulipua bomu kanisani na baadae kwenye mkutano wa chadema soweto.
 
Last edited by a moderator:
Jiulize! Ni kesi Ngapi ambazo mmewafungulia wapinza ziwe za kubambika Au za kweli mlizozishinda? Ata ya Huyo Kilewo mtashindwa!

Au niambie ni Kiongozi gani Au mbuge gani Wa upinzani mliwahi kumshinda mahakani? Hii inaonesha kesi nyingi si halali na Ndo maana hamshindi!

Kama mna historia ya kushinda kesi hivyo. Mbona ya bomu la soweto haipelekwi mahakamani ilhali ushahidi wa "DVD" upo?
 
Kinachosikitisha ni serikali kutomkamata Mwigulu Nchemba mpaka sasa, Sasa sijui tuna serikali au kikundi cha wasanii tu! Serikali ya CCM haina tofauti na makaburu wa Afrika kusini,
 
Hakuna walichotikisa mbona, hilo swali wameambiwa waandike kwa maandishi sio wanabwabwaja tu kama wameshapiga gongo zao asubui.

Hakuna utaratibu wa kuandika. utaratibu ni wa maswali ya papo kwa papo, kama waziri mkuu anataka maswali ya kuandikwa basi aache kuuza sura siku za alhamisi. Kama hana majibu akayaandike lakini siyo swali liandikwe kwa sababu swali lilishaulizwa na linaeleweka.
 
Hakuna walichotikisa mbona, hilo swali wameambiwa waandike kwa maandishi sio wanabwabwaja tu kama wameshapiga gongo zao asubui.

wewe bila shaka unapapaswa na mwigulu unatetea hata ujinga, wacha waanuliwe mnaua watu mnaleta blaa blaa hapa
 
Akili ndogo kuiongoza akili kubwa ndio ivyo tena na wewe umechangia eti he he he he :bange:
..lazima tukukaushe tu mtimbichi,hii ngoma inaitwa force kingi,pm kawekwa mtu kati mpaka kachemka,chezeya cdm weye...!!
 
Uliona povu jingi alilotoa Mwigulu kabla ya sakata hilo bungeni alipotafuta pa kujishikiza kumshinikiza Mbowe, bado utelezi unaendelea atakuja angukia pua soon.
Hebu kwanza tujikumbushe kauli ya serikali ambayo ilitolewa na waziri Lukuvi, baada ya bomu hilo kulipuka, kuwa ni mipango ya Chadema, kwa kuwa walijua kuwa hawana nafasi ya kushinda kata yoyote kati ya hizo nne zilizokuwa zikigombewa za madiwani.

Uchaguzi ulipofanyika CCM walilala 4 kwa bila!!

Sasa kutokana na kauli ya Lukuvi kuwa chama lilicholipua bomu hilo, ilikuwa ni mkakati wao wa kutaka kuvuruga uchaguzi huo, baada ya kuona hawana nafasi hata kidogo ya kushinda uchaguzi huo, kwa matokeo hayo yaliyotokea ya CCM kupoteza kata zote hizo 4, ni ushahidi usio na mashaka yoyote kuwa wao ndiyo wahusika wakuu wa tukio hilo la bomu.

Fact namba 2 ni kuwa kwa jinsi poliCCM inavyotenda kazi zao, wakiwa katika coalition na magamba, kama kweli viongozi wa Chadema wangekuwa wamehusika na ulipuaji wa bomu hilo, sasa hivi wangekuwa wanaozea jela.

Kwa maana hiyo, taarifa hii mpya iliyotolewa bungeni na mbunge Nassari na Lema, inaweza kuwa na ukweli wa asilimia 100, kwa kuwa tokea mwanzo, jeshi la polisi na serikali yake, vilionyesha wazi wazi, lengo lao la kutaka kupotosha ukweli wa tukio hilo, hadi pale Chadema waliposema kuwa wanao mkanda wa video, unaoonyesha kuwa jeshi la polisi, ndiyo wahusika wakuu, wa ulipuaji wa bomu hilo!

Kutokana na hali hiyo, ushauri wangu wa bure kwa kijana huyo ambaye ameenda Dodoma bungeni kwa lengo la kutaka kueleza ukweli wa suala hilo, ni vyema akaamua kubadilisha uamuzi wake na akatafuta hifadhi, kwenye ubalozi wa Marekani, kwani kwa hiyo dhamira yake ya kutaka kueleza yale aliyofanyiwa akiwa kwenye mahabusu za polisi, za kushinikizwa ambambikie na kumtaje Lema kuwa ndiye aliyemtuma kufanya unyama huo, kwa kitendo chake cha kukataa mashinikizo, ni wazi kijana huyo maisha yake yatakuwa hatarini sana kwa sasa, kama hatafanya uamuzi wa haraka wa kuomba hifadhi kwenye balozi za nje.
 
Mwigullu hawezi kuchomoka kwenye hili! Kama poli-ccm wangekuwa makini walitakiwa wawe wamesha mkamata yeye na Nape kwa kauli zao za kuashiria mauwaji siku moja kabla ya mauwaji yenyewe.

Mtu yotote makini ataunganisha nukta na kuona ushiriki wa ccm kwenye kulipua bomu. Kwani hata wakisema wana kana kuwa hawaja lipua halafu tukalinganisha ripoti ya serikali iliyofichwa juu ya mauwaji ya Januari 5 wataweza kurukia wapi wakati ripoti imesema kabisa kuwa polisi walihusika na walidhamiria kuuwa?!!

Vipi kauli ile ya Dr Slaa mara baada ya uchaguzi mkuu kwamba nchi hii haiwezi kutawalika? tukiunganisha dots nam matukio mengi ya fujo kwenye mikutano ya siasa hususan ile ya CDM kuna mahusiano yoyote ? au hapo dots haziunganiki?
 
Back
Top Bottom