Waziri2025
Senior Member
- Sep 2, 2019
- 148
- 379
Akiongea na Vyombo Vya Habari katika Ofisi za jiji la Arusha wakati akiwasilisha malalamiko yake kwa Mkurugenzi msaidizi wa uchaguzi dkt John Pima ,Mgombea Ubunge wa jimbo la Arusha Mjini chadema,Godbless Lema amedai kushtukia mpango uliosukwa wa kuongeza majina hewa ili kukipa ushindi Chama cha mapinduzi.
Akiongea kwa uchungu huku akilengwalengwa na machozi ,Lema amesema awali wapiga kura kwenye daftari la kudumu jimbo la Arusha mjini walikuwa zaidi ya laki 240 lakini Jana wameshangaa kuona kwenye daftari hilo kuna wapiga kura zaidi ya laki 370 ikiwa ni ongezeko la wapiga kura hewa zaidi ya 100 .
Lema amesema baada ya kumuuliza dkt. Pima ameshindwa kutoa ufafanuzi badala yake aliwatuliza viongozi wa chadema na kuwataka wafike Ofisini kwake ili atoe ufafanuzi.
Hata hivyo Lema amesema Chama chake kimejipanga kuandika barua ya malalamiko kwa Mkurugenzi wa uchaguzi NEC ,dkt Wilson Mahera kupeleka kilio chao
Amesema ameshutushwa pia na hatua ya Mgombea wa ccm,Mrisho Gambo kwenda kuomba kura kwa wanafunzi wa sekondari ambao alidai ndio wametayatishwa kupiga kura siku ya uchaguzi jambo ambalo aliwaonya Wazazi wao kutowaachia watoto wao waliochini ya miaka 18 kushiriki mchezo huo mchafu wakati hawakujiandikisha kuwa wapiga kura.
Halikadhalika amesema kuwa ameshangaa katika Ofisi ya Mkurugenzi kumkuta mkuu wa wilaya ya Arusha Kenan Kihongosi na DSO wakichambua fomu za mawakala jambo ambalo mkuu wa wilaya hahusiki kabisa na suala la uchaguzi na kudai kuwa kuna mpango wa maksudi wa kuhujumu mawakala wao.
Hata hivyo waandishi wa Habari waliofurika katika Ofisi za jiji la Arusha kutaka kupata ufafanuzi wa tuhuma hizo kwa dkt Pima msimamizi msaidizi wa uchaguzi, alikataa kutolea ufafanuzi jambo hilo huku akiahidi kuita wanahabari kwa muda wake.
"Nitawaita wakati mwingime nitaonga na nyingi si jambo hili tu nitawaeleza na mengine yanayohusi uchaguzi" alisema huku akiingia Ofisini kwake.
Akiongea kwa uchungu huku akilengwalengwa na machozi ,Lema amesema awali wapiga kura kwenye daftari la kudumu jimbo la Arusha mjini walikuwa zaidi ya laki 240 lakini Jana wameshangaa kuona kwenye daftari hilo kuna wapiga kura zaidi ya laki 370 ikiwa ni ongezeko la wapiga kura hewa zaidi ya 100 .
Lema amesema baada ya kumuuliza dkt. Pima ameshindwa kutoa ufafanuzi badala yake aliwatuliza viongozi wa chadema na kuwataka wafike Ofisini kwake ili atoe ufafanuzi.
Hata hivyo Lema amesema Chama chake kimejipanga kuandika barua ya malalamiko kwa Mkurugenzi wa uchaguzi NEC ,dkt Wilson Mahera kupeleka kilio chao
Amesema ameshutushwa pia na hatua ya Mgombea wa ccm,Mrisho Gambo kwenda kuomba kura kwa wanafunzi wa sekondari ambao alidai ndio wametayatishwa kupiga kura siku ya uchaguzi jambo ambalo aliwaonya Wazazi wao kutowaachia watoto wao waliochini ya miaka 18 kushiriki mchezo huo mchafu wakati hawakujiandikisha kuwa wapiga kura.
Halikadhalika amesema kuwa ameshangaa katika Ofisi ya Mkurugenzi kumkuta mkuu wa wilaya ya Arusha Kenan Kihongosi na DSO wakichambua fomu za mawakala jambo ambalo mkuu wa wilaya hahusiki kabisa na suala la uchaguzi na kudai kuwa kuna mpango wa maksudi wa kuhujumu mawakala wao.
Hata hivyo waandishi wa Habari waliofurika katika Ofisi za jiji la Arusha kutaka kupata ufafanuzi wa tuhuma hizo kwa dkt Pima msimamizi msaidizi wa uchaguzi, alikataa kutolea ufafanuzi jambo hilo huku akiahidi kuita wanahabari kwa muda wake.
"Nitawaita wakati mwingime nitaonga na nyingi si jambo hili tu nitawaeleza na mengine yanayohusi uchaguzi" alisema huku akiingia Ofisini kwake.