Lema alamba posho kikao cha madiwani Arusha!

FIDIVIN

Senior Member
Aug 4, 2010
187
41
MBUNGE wa Arusha Mjini, Godbless Lema amekiri kusaini na kuchukua posho ya kikao cha Baraza la Madiwani mwishoni mwa wiki, lakini akatetea uamuzi huo akisema alikwenda kuzima njama za kufukuzana.

Lema na madiwani wenzake watatu wa Chadema, walishiriki katika kikao cha Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Jiji la Arusha, kinyume cha msimamo wao wa kutohudhuria vikao hivyo.

Mapema mwaka jana, Lema na madiwani wote wa Chadema wa Jiji la Arusha waliweka msimamo wa kutomtambua Meya wa Jiji hilo, Gaudence Lyimo na kutohudhuria vikao vyote vya Baraza la Madiwani kwa madai kuwa Meya huyo hakuchaguliwa kwa mujibu wa sheria na kanuni na kuhudhuria vikao ni kumtambua.

Lakini Ijumaa iliyopita, Lema na madiwani Isaya Doita (Ngarenaro), Crispin Tarimo (Sekei) na Sabina Francis (Viti Maalumu), walihudhuria kikao hicho na kupokea posho kwa malipo ya kuhudhuria kikao.

Lema alikiri alisaini posho hiyo yeye na wenzake na kudai kulikuwa na njama za kutaka kuwafukuza madiwani wa Chadema kwa kukosa kuhudhuria vikao vitatu mfululizo bila ya kuwa na taarifa yoyote na kwa mujibu wa sheria na kanuni wangetimuliwa.

Alisema kwa kufanya hivyo siyo kama wamebadilisha msimamo wao wa kutomtambua Meya Lyimo na Naibu wake, Estomii Mallah, isipokuwa ilibidi wafanye hivyo kutegua mtego wao wa madai ya kufukuzwa madiwani.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Jiji la Arusha, Estomii Chang'a alisema madiwani wa Chadema walipewa posho baada ya kuhudhuria kikao hicho na wala hakukuwa na njama za kutaka kuwafukuza kama alivyodai Lema.

Source: Habari Leo
 
Mtajiju......Hata UDSM vijana wamepata akili za mgomo siku hizi,wanagoma siku mbili ya tatu darasani,siku2 ya3 class mpaka kieleweke,Safi kamanda,najua wanataka anzisha majungu hapa,akili kichwani maana wakifukuzwa hao madiwani wao si ndio watajiona wako sahihi!!!Twende kazi hakuna kulala mpaka mieleweke....
 
is it within the law for Lema to signed up for posho ? if it is not, call the authority to pick him up and stop complaining.
 
nafikiri ndiyo lilikuwa lengo lao kuwatimua, kama watu wamehudhuria kwa nini mkurugenzi alalamike kwenye vyombo vya habari je alitaka wasiudhurie?
 
Yaani hao habari leo bure kabisa ishu ni kudhuria kikao au posho?????
 
Viongozi wengi wa Chadema wamevutiwa kwenye siasa na pesa za posho ila wengi wao ni wanafiki na waongo tu. Mtu kama Zitto alishawahi kuhongwa VX na RA lakini anajifanya eti yupo mstari wa mbele kupinga posho za vikao! Huyu Lema naye ana historia ya wizi wa Magari kwahiyo siwezi kumshangaa kama ameamua kuiba na kuchukua posho za vikao za madiwani. Haya ni mambo ambayo niliyatarajia kabisa kwahiyo siwezi kushangaa.
 
Viongozi wengi wa Chadema wamevutiwa kwenye siasa na pesa za posho ila wengi wao ni wanafiki na waongo tu. Mtu kama Zitto alishawahi kuhongwa VX na RA lakini anajifanya eti yupo mstari wa mbele kupinga posho za vikao! Huyu Lema naye ana historia ya wizi wa Magari kwahiyo siwezi kumshangaa kama ameamua kuiba na kuchukua posho za vikao za madiwani. Haya ni mambo ambayo niliyatarajia kabisa kwahiyo siwezi kushangaa.

Mbona hutuelezi wewe umehongwa nini? Na hao magamba wanaoacha fani zao na kugombea uongozi wanafuata nini? Msipende kuufanya uongozi wa nchi yetu kuwa exclusive kwa magamba tu! We need change and PEOPLE'S POWER will prevail!!
 
Swala kubwa hapo ni lema kuhudhuria kikao au kulamba posho????!!!!
 
Njaa mbaya, kelele nyingi lakini mgao ukipita wao ndio wa kwanza kutanguliza bakuli. Lema ni jambazi sasa mlitegemea nini kutoka kwake? Kama aliweza kuua watu kwaajili ya pesa sasa unataka aziachie za bila jasho.
 
teh teh mtachonga sssssana, lakini kumbukeni uzuri wa wana chadema tumebarikiwa akili na ufaham!
sema yote kete tumewanyima antunasonga kwa nguvu ya uma! peeeeeples!
 
Njaa mbaya, kelele nyingi lakini mgao ukipita wao ndio wa kwanza kutanguliza bakuli. Lema ni jambazi sasa mlitegemea nini kutoka kwake? Kama aliweza kuua watu kwaajili ya pesa sasa unataka aziachie za bila jasho.

mungu akusamehe, haujui ulitendalo. Unaweza kudhibitisha ujambazi wa Lema?
 
Swala kubwa hapo ni lema kuhudhuria kikao au kulamba posho????!!!!
Kama hamtambui meya nadhani ni vizuri asingehudhuria vikao, akifukuzwa ubunge poa tu, lakini amesimamia anachokiamini na ambacho chama chake kinaamini. The same goes to CDM MPs.... wasingeitambua serikali ya JK.Anything else is BS.
 
Viongozi wengi wa Chadema wamevutiwa kwenye siasa na pesa za posho ila wengi wao ni wanafiki na waongo tu. Mtu kama Zitto alishawahi kuhongwa VX na RA lakini anajifanya eti yupo mstari wa mbele kupinga posho za vikao! Huyu Lema naye ana historia ya wizi wa Magari kwahiyo siwezi kumshangaa kama ameamua kuiba na kuchukua posho za vikao za madiwani. Haya ni mambo ambayo niliyatarajia kabisa kwahiyo siwezi kushangaa.

Kweli eeh hata mkisema walivutwa na pesa au nini wana cdm ni wajuvi wa mambo chadema ipo tangu 1992 hatuja kulupuka kuipenda hata kama lema alikuwa jambazi mbona jambazi wenzie kina Alex masawe,Zombe,francis nyari mmewaacha huru au sababu huwa wanafadhili kampeni
 
Viongozi wengi wa Chadema wamevutiwa kwenye siasa na pesa za posho ila wengi wao ni wanafiki na waongo tu. Mtu kama Zitto alishawahi kuhongwa VX na RA lakini anajifanya eti yupo mstari wa mbele kupinga posho za vikao! Huyu Lema naye ana historia ya wizi wa Magari kwahiyo siwezi kumshangaa kama ameamua kuiba na kuchukua posho za vikao za madiwani. Haya ni mambo ambayo niliyatarajia kabisa kwahiyo siwezi kushangaa.

mbona na wewe unachukua Posho kwa Nape ili ushinde humu JF
 
Viongozi wengi wa Chadema wamevutiwa kwenye siasa na pesa za posho ila wengi wao ni wanafiki na waongo tu. Mtu kama Zitto alishawahi kuhongwa VX na RA lakini anajifanya eti yupo mstari wa mbele kupinga posho za vikao! Huyu Lema naye ana historia ya wizi wa Magari kwahiyo siwezi kumshangaa kama ameamua kuiba na kuchukua posho za vikao za madiwani. Haya ni mambo ambayo niliyatarajia kabisa kwahiyo siwezi kushangaa.




Mwitaaaaaa!

Umeishiwa kabisa hoja! Imewauma sana maana hilo ni bao la kisigino. Mlitegemea kupeleka hoja ya kuwafukuza lakini wameizima. Sasa mmebaki mnazungumzia posho na propaganda.

Pole sana, mpambano bado unaendelea na tutatumia mbinu zote hadi kieleweke!
 
Njaa mbaya, kelele nyingi lakini mgao ukipita wao ndio wa kwanza kutanguliza bakuli. Lema ni jambazi sasa mlitegemea nini kutoka kwake? Kama aliweza kuua watu kwaajili ya pesa sasa unataka aziachie za bila jasho.

na kweli njaa mbaya, si unaona unavyolopoka kwa ku2mia masaburi, jikaze ndugu Nape anahesabu idadi ya post...
 
Viongozi wengi wa Chadema wamevutiwa kwenye siasa na pesa za posho ila wengi wao ni wanafiki na waongo tu. Mtu kama Zitto alishawahi kuhongwa VX na RA lakini anajifanya eti yupo mstari wa mbele kupinga posho za vikao! Huyu Lema naye ana historia ya wizi wa Magari kwahiyo siwezi kumshangaa kama ameamua kuiba na kuchukua posho za vikao za madiwani. Haya ni mambo ambayo niliyatarajia kabisa kwahiyo siwezi kushangaa.


Yani wewe ukiona thread inamuhusu Lema tu, lazima utie kalamu. Lema fanya mpango umuoe huyu Mwita25. Anakupenda sana.
 
Njaa mbaya, kelele nyingi lakini mgao ukipita wao ndio wa kwanza kutanguliza bakuli. Lema ni jambazi sasa mlitegemea nini kutoka kwake? Kama aliweza kuua watu kwaajili ya pesa sasa unataka aziachie za bila jasho.

Duh! Kweli mafisadi wameanza kazi yao humu ndani. Nimesema tangu jana ya kwamba humu hata mkiingia na gia ya kupandia milima hakika tutawatambua tu. Humu tumo wa2 na akili ze2 timamu wa kutambua nani huyu na ni nani yule. Wewe uliandika thread hii kawaambie ya kwmb huko hapaingiliki kihivyo ulivyokuja wewe. Hii ni karne ya 21 bila shaka magamba mtateseka sana.
 
Swali la msingi la kujiuliza hivi ni haramu diwani kuchukua posho aliyohudhuria kikao? Pia pana logic kusema kuwa hao madiwano wangefukuzwa kama wasingehudhuria kikao hicho maana kingekuwa kikao cha tatu kutohudhuria bila sababu ya msingi!
 
Swali la msingi la kujiuliza hivi ni haramu diwani kuchukua posho aliyohudhuria kikao? Pia pana logic kusema kuwa hao madiwano wangefukuzwa kama wasingehudhuria kikao hicho maana kingekuwa kikao cha tatu kutohudhuria bila sababu ya msingi!

Ni haramu sana kwasababu haiwezekani umkatae meya halafu hapohapo uhudhurie vikao. Hizi njaa zitawaua magwanda
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom