Ritz
JF-Expert Member
- Jan 1, 2011
- 46,903
- 32,312
Kiingereza kama zilivyo lugha zingine, ni chombo cha mawasiliano lakini siyo utaalam wala siyo kipimo cha elimu au ujuzi. Wakuu wa China, Ujerumani, Urusi, Italy, n.k. wakienda mataifa mengine wanaongea lugha zao, siyo kiingereza, na hilo haliwapunguzii chochote. Kama Lema kiingereza kama hakijui, anaweza kuongea kiswahili, na hilo halitampunguzia chochote.
Humu JF, wengi wa wasiokijua kiingereza ndiyo wanaonekana kuhusudu sana mjadala wa lugha, kwa vile ni kitu kinachowasumbua, wanadhani ni kitu muhimu sana. Nenda kule Brazil, Chile, Argentina, Peru, Mexico na hicho kiingereza chako cha kubabaisha ungejiona kutokuwa tofauti na yeyote asiyejua hata neno moja la kiingereza. Bila hata ya kiingereza, leo uchumi wa Brazil ni wa tano kwa ukubwa Duniani.
Mkuu umeongea mengi bila sababu tatizo hapa sio masuala ya uchumi watu wanahoji Lema kaongea nini na huyo Meya wa London wakati hajui kingereza bahati mbaya Meya wa London naye hajui kiswahili...unatakiwa kujibu hili.