n00b
JF-Expert Member
- Apr 10, 2008
- 1,006
- 2,667
MBUNGE wa Jimbo la Arusha Godbless Lema CHADEMA) ameionya na kuitaka Idara ya Usalama wa Taifa nchini kujifunza kutoka kwa Kiongozi wa Libya Muammar Gadaffi.
Mbali na kuinyoshea vidole Idara hiyo Lema pia amewataka Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha na Kamanda wa Polisi mkoani hapa kutambua kuwa kazi yao si kukitetea Chama cha Mapinduzi (CCM) bali ni kutetea maslahi ya taifa.
"Kama Idara ya Usalama wa Taifa, Jeshi la Polisi wanafikiri wao wana nguvu sana wanapaswa kujua kwamba wanajidanganya. Kama wanataka kujua nguvu zao zina uwezo kiasi gani, wasafiri kwenda kuiuliza Idara ya Kijasusi ya Libya kama ilimsaidia Gadaffi asipinduliwe kwenye nchi aliyoingoza kwa miaka zaidi ya 40," alidai Lema.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana mjini Arusha Lema alidai taarifa za Kiintelijensia walizonazo zimedhibitishia pasipo shaka kuwa Idara ya Usalama wa Taifa mkoani Arusha inatumika kwenye mgogoro wa Meya.
Godbless Lema akiongea na waandishi
Alidai kuwa mtu anayetuhumiwa kuongoza mpango huo mchafu unaolenga kuwaangamiza viongozi wa kisiasa wa CHADEMA ni Msaidizi wa Mkuu wa Usalama wa Taifa Mkoa wa Arusha.
Endelea >>> FikraPevu | Lema 'aichana' idara ya Usalama wa Taifa
Mbali na kuinyoshea vidole Idara hiyo Lema pia amewataka Mkuu wa Upelelezi Mkoa wa Arusha na Kamanda wa Polisi mkoani hapa kutambua kuwa kazi yao si kukitetea Chama cha Mapinduzi (CCM) bali ni kutetea maslahi ya taifa.
"Kama Idara ya Usalama wa Taifa, Jeshi la Polisi wanafikiri wao wana nguvu sana wanapaswa kujua kwamba wanajidanganya. Kama wanataka kujua nguvu zao zina uwezo kiasi gani, wasafiri kwenda kuiuliza Idara ya Kijasusi ya Libya kama ilimsaidia Gadaffi asipinduliwe kwenye nchi aliyoingoza kwa miaka zaidi ya 40," alidai Lema.
Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana mjini Arusha Lema alidai taarifa za Kiintelijensia walizonazo zimedhibitishia pasipo shaka kuwa Idara ya Usalama wa Taifa mkoani Arusha inatumika kwenye mgogoro wa Meya.
Godbless Lema akiongea na waandishi
Alidai kuwa mtu anayetuhumiwa kuongoza mpango huo mchafu unaolenga kuwaangamiza viongozi wa kisiasa wa CHADEMA ni Msaidizi wa Mkuu wa Usalama wa Taifa Mkoa wa Arusha.
Endelea >>> FikraPevu | Lema 'aichana' idara ya Usalama wa Taifa