Hamna kitu ndio maana CCM inashinda kwa kishindo, wiki iliyopita povu linamtoka kwamba apewe majina ya uswisi ayataje hadharani, leo anasema ana DVD aifanyie duplicate wasambaze na waweke youtube watu waone kama wanaogopa ushahidi kuharibiwa na serikali. Waitoe DVD tuone ili tuihoji serikali kwenye kisanduku cha kura la sivyo yaleyale ya ''Cambridge international college'-chuo kipo online'(ulaghai mtupu), sasa tume ya kimahakama ataiamini vipi?wakati Jaji mkuu ni mteule wa raisi (kwa katiba ya sasa).Kila kukicha anawaambia watu kwamba dhambi kubwa ni uoga wakati yeye ni mwoga.........alijificha ndani ya nyumba yake usiku kucha polisi wasimkamate kwa agizo la mkuu wa mkoa.........!Katika Bunge linaloendelea hivi sasa Dodoma, Mb Lema katika kuwasilisha mchango wake kuhusu ripoti iliyowasilishwa bungeni juu ya wizara ya mambo ya ndani amesema
"Katika ripoti yote iliyoandikwa katika kitabu hiki sijaona ikielezea au kuzungumzia bomu la soweto wakati bomu la olasiti limezungumziwa, Chadema ilisema tunaushaidi wa DVD juu ya aliyehusika na ulipuaji wa bomu la soweto na tukashauri Raisi aunde tume huru ya kimahakama ili tuwasilishe ushaidi wetu. Cha kushangaza haijaundwa mpaka leo na hawataki kufuatilia swala hilo" mwisho wa kunukuu.
My take
Hapa inaonyesha kuwa Chadema walionewa na ni kweli Serikali inausika juu ya ulipuaji wa bomu la soweto na sasa wanachokifanya ni kupiga chenga ili kuficha ukweli.