Proved
JF-Expert Member
- Sep 10, 2018
- 27,542
- 34,868
Kama wewe ndio Leila pole sana kwa kuitwa teja, najua inaumiza sana kutupiwa kashfa ambazo sio za kweli, msamehe tu huyo jamaa.Ulitegemea kasichana, mwanafunzi wa chuo kikuu arudi na mbaula, Cantor, Suzuki?
Karudi na begi moja lenye Jeans 2, t Sheti 3, sketi moja, dera na mtandio wa kusali, na vitabu.
Karudi na B. A. Politics and Government
Karudi na M. A. African Studies.
Karudi na Higher Diploma in Journalism and Film Making.
Na maadili yake na uzalendo wake.
Hongera kwa kusoma na kuhitimu vizuri.