Equation x
JF-Expert Member
- Sep 3, 2017
- 29,270
- 40,080
Katika dunia hii iliyojaa makabila tofauti tofauti, kila kabila au jamii ina utaratibu wake wa kutoa mahari. Kuna wengine wanatoa njiwa wanapata mke, wengine wanatoa aina fulani ya mifugo wanapata mke, wengine wanatoa dumu la asali na kupata mke n.k. Sasa najiuliza hawa wa kwetu wanaotaka mavitu makubwa makubwa wanayataka ya nini, au ndio kuuziwa binadamu (mke)? Kwa wale ambao hawajaolewa mpaka nyakati hizi, jaribuni kulegeza masharti angalau mahari iwe ata debe la mahindi,ili na wewe uwe na mume.