Asante, umeona kuwa katika hali ya kawaida, ile scenery nzima mtu angesema kuwa alikusudia kuua maana alishatamka kwamba utanitambua.... sasa nikifa tena wewe ukaniua kwa mwichi, akili ya kawaida ni kuwa ulikusudia kabisa. Lakini angali majaji walivyochukua angle tofauti kabisa.
Katika hii kesi majaji wa Mahakama ya rufaa walijipa mamlaka ya kuchambua upya ushahidi uliowwekwa mbele ya trial court. Wakabadili verdict toka murder hadi kuwa manslaughter, na hatimae wakafanya mitigation suo mottu, intra-partes, na kutoa sentence.
Mahakama inayosikiliza rufaa inayo mamlaka ya kupitia upya ushahidi na kuudadavua. Wakili wa utetezi (Nyange) aligusi kuhusu kupunguzwa kwa kosa kutoka la mauaji hadi kuua pasipo kukusudia. Somo linalopatikana hapa ni kuwa mawakili wa utetezi wanao wajibu wa kutetea mteja wao kwa kadri ya sheria na kanuni zake. Mwanzo (katika trial court) wakili wa utetezi hakufanya jitiada zozote kumuokoa mteja wake. Majaji wa rufaa waliliona hili na kuamua kuokoa jahazi.