Lecturers' Corner - Ushauri, Changamoto & Mengineyo

Prof Decentman

JF-Expert Member
Jul 14, 2013
276
140
Napenda kutumia jukwaa hili kuwakaribisha wahadhiri wenzangu popote mlipo tuweze ku-share changamoto zetu, maendeleo ya elimu hasa ya chuo, ushauri kwa wanafunzi wa vyuo, vituko tunavyokutana navyo na mambo mengineyo.

Natambua tunapokuwa darasani tunakuwa strict sana ila hapa tuwe flexible sababu tuna-share mambo ambayo yawezekana wengi hawayajui.

Japo uzoefu wangu chuoni si mkubwa sana around 10 years naweza sema nimeona wanafunzi bright na wengi wasiojiweza kimasomo yaani bora liende. Wanafunzi hawa kuwaongoza na kuwatengeneza wawe vzr ni changomoto kubwa sana. Uzuri chuoni walimu tuna nguvu kubwa hivyo unaweza kwa kiasi fulani kumlazimisha mtu awe unavyotaka maana asipofata taratibu anaweza kufeli.

Changamoto moja ninayoikumbuka ni siku moja nikiwa nasimamia mtihani nikamwona kwa mbali binti mmoja ana hangaika hangaika, nikahisi hapa si bure. Niwaibie siri kwa wale wanafunzi, mwl ni rahisi sn kumgundua mwanafunz mwenye kibuti au anayeibia unless mwl aamue kupotezea. So nika-trace vzr kbs, nikamfata mpaka pale alipokaa taratibu kbs nikakuta amefungua paja lake anaibia majibu maana alikuwa amejiandika, nilisikitika sn kwa kitendo hicho. Maamuzi niliyochukua siri yangu.

Tabia nyingine inayonishangaza ni kula karatasi za vibuti aka migi, how comes mwanafunzi unameza karatasi, au tumbo lako linaweza ku-digest karatasi bila shida?

Kingine wanafunzi wa siku hizi vyuoni acheni kupenda slope. Watu hawasomi kucha kuzurura na starehe, ukifika muda wa course work mnaanza kusumbua, mara make up, mara mnatupa majaribu kuwa 'chochote utakachotaka nitakupa' walimu wenzangu msijaribu kuruhusu kuingia ktk huu mtego ni hatari sana.

Nakaribisha wahadhiri wote katika maeneo mbalimbali ya kitaalam tushauriane na kushare changamoto, na pia wanafunzi wa vyuo kama una maswali uliza wataalam watajibu.

Pengine tujikite katika maeneo yafuatayo;
1. Namna ulivyoweza kuingia ktk kazi ya kufundisha - njia ulizopita. Hii itakuwa ni namna ya kuwatia moyo wale wanaotaka kuwa wahadhiri.
2. Ushauri wa kimasomo. Hii itahusu masuala ya kimasomo ama elimu kwa yule atakayependa kujua.
3. Maadili - ya Walimu & wanafunzi wa Vyuoni .
4. Mfumo wa elimu yetu ya vyuo (in general) na namna inavyowaanda wasomi ktk ajira.
5.Maisha ya Vyuoni.
6. Maslahi ya walimu.
7. Changamoto za kazi ya ualimu vyuoni.
8. Mbinu bora za ufundishaji zenye ubunifu.
9. Uandishi wa vitabu, machapisho, kufanya tafiti na shauri za kitaalam.
10. Udahili wa wanafunzi - Uwezo na ubora, Kujituma na ubunifu,
11. Nidhamu za Wanafunzi

Na mambo mengineyo.

Aksante!
 
I can bet wewe sio lecturer wala Tutorial Assistant. Kama taifa lina wahadhiri wa namna yako sio tu limepotoka bali linaangamia na kutumbukia kwenye kina kirefu.

Kwa uandishi huu na reasoning unayoonesha napata wasiwasi uhadhiri uliutolea wapi na ulipata kwa sifa zipi. Maana hakuna hata chembe ya dalili ya Ph.D wala mtu mwenye published and referred work.
 
I can bet wewe sio lecturer wala Tutorial Assistant. Kama taifa lina wahadhiri wa namna yako sio tu limepotoka bali linaangamia na kutumbukia kwenye kina kirefu.

Kwa uandishi huu na reasoning unayoonesha napata wasiwasi uhadhiri uliutolea wapi na ulipata kwa sifa zipi. Maana hakuna hata chembe ya dalili ya Ph.D wala mtu mwenye published and referred work.

Haina shida kiongozi. Dhumuni la uzi huu ni ku-share mambo ya kawaida tu ya kazi, ushauri na hata changamoto. Ndo maana nikasema hapo mwanzo tuwe 'flexible' kama umenipata vzr. Pili si lazima uamini kama mm ni mhadhiri, ukiamini ni sawa, usipoamini ni sawa pia.
 
Nakushauri tu kama kweli unataka mchango wa wahadhiri hapa andika like one.
 
Sasa na hapa wawe serious tena kama huko madarasani?
Shida yetu walimu ni moja ' we tend to take everything academically' ndio maana it is common to see laymen become successfully in so many arena, mention politics, business, sports, technology to mention a few, while the so called professors, dr and other academicians tunashindwa kuacha legacy ktk maisha halisi na mahitaji ya jamii zetu. Na hili ni common hasa ktk ulimwengu wetu wa tatu.
Mfano wakati nikiwa kijana mdogo niliona ndoa za wasomi wa vyuo zikiwa taabani, nikawa najiuliza sasa kwa wasomi ni hivi je wasiosoma itakuwaje.
Pamoja bado naamini wasomi wana michango mizuri katika maeneo yao ya expertise japo wengine wanakosa practice ya field.

Ndio maana nikamjibu ndugu hapo tuli-relax, tuwe flexible..
 
Malecturer wengi wapenda kutoa maksi za kuwavua chupi wadada,wananikera sana eti hatusomi wanaume ila mabinti maksi za mezani...Natamani nimfaham kama lecturer wangu mmoja mpuuzi wa chuo flani nmchane live,alinifanya niichukue linguistics akati naipenda na ilikuwa inapanda.Lakn nashukuru mungu mwsho wa siku nimehitimu salama.Mana hyo lecturer alipendelea wanawake tu na wale wanaume wakumnyenyekea kama mfaulme.Mbaya zaidi anatunga test hata yeye majbu hajui.
 
Ki
Malecturer wengi wapenda kutoa maksi za kuwavua chupi wadada,wananikera sana eti hatusomi wanaume ila mabinti maksi za mezani...Natamani nimfaham kama lecturer wangu mmoja mpuuzi wa chuo flani nmchane live,alinifanya niichukue linguistics akati naipenda na ilikuwa inapanda.Lakn nashukuru mungu mwsho wa siku nimehitimu salama.Mana hyo lecturer alipendelea wanawake tu na wale wanaume wakumnyenyekea kama mfaulme.Mbaya zaidi anatunga test hata yeye majbu hajui.[/QUOTE
Kiongoz, haya mambo huwa yanatokea na kwa mtazamo wangu zipo sababu kadhaa;
1. Maadili ya mwalimu husika, hili linategemeana na background yake. Kama ni mtu wa maadili sana hawezi fanya uonevu na upendeleo wowote.
2. Nilisema mwanzoni, muda mwingine majaribu toka jinsia KE kama mwalimu ni ME huwa ni kubwa sana. Mtu anaweza kuwa na maadili yake lakini ikifika stage fulani anaweza shawishika kuyafanya hayo yasio takiwa kama binadamu.
3. Mazingira ya kazi na maslahi ya walimu; muda mwingine kwa sababu ya kutojaliwa ktk maslahi yao waalimu wengi wanaweza kuamua kufanya ndivyo sivyo yaani bora liende. Nina mfano wa chuo fulani palikuwa na msemo maarufu wa 'marupurupu' ya waalimu.
4. Kama ikitokea ukiona hautendewi haki vyuo vingi vina namna ya kushughulikia malalamiko japo bado mwl ana nafasi kubwa sana ya kusababisha 'usumbifu' kwa mwanafunzi akitaka.

Uzuri ni kuwa umeshamaliza so pole kwa hizo changamoto.
 
Malecturer wengi wapenda kutoa maksi za kuwavua chupi wadada,wananikera sana eti hatusomi wanaume ila mabinti maksi za mezani...Natamani nimfaham kama lecturer wangu mmoja mpuuzi wa chuo flani nmchane live,alinifanya niichukue linguistics akati naipenda na ilikuwa inapanda.Lakn nashukuru mungu mwsho wa siku nimehitimu salama.Mana hyo lecturer alipendelea wanawake tu na wale wanaume wakumnyenyekea kama mfaulme.Mbaya zaidi anatunga test hata yeye majbu hajui.


Kiongoz, haya mambo huwa yanatokea na kwa mtazamo wangu zipo sababu kadhaa;
1. Maadili ya mwalimu husika, hili linategemeana na background yake. Kama ni mtu wa maadili sana hawezi fanya uonevu na upendeleo wowote.
2. Nilisema mwanzoni, muda mwingine majaribu toka jinsia KE kama mwalimu ni ME huwa ni kubwa sana. Mtu anaweza kuwa na maadili yake lakini ikifika stage fulani anaweza shawishika kuyafanya hayo yasio takiwa kama binadamu.
3. Mazingira ya kazi na maslahi ya walimu; muda mwingine kwa sababu ya kutojaliwa ktk maslahi yao waalimu wengi wanaweza kuamua kufanya ndivyo sivyo yaani bora liende. Nina mfano wa chuo fulani palikuwa na msemo maarufu wa 'marupurupu' ya waalimu.
4. Kama ikitokea ukiona hautendewi haki vyuo vingi vina namna ya kushughulikia malalamiko japo bado mwl ana nafasi kubwa sana ya kusababisha 'usumbifu' kwa mwanafunzi akitaka.

Uzuri ni kuwa umeshamaliza so pole kwa hizo changamoto.
 
Shida yetu walimu ni moja ' we tend to take everything academically' ndio maana it is common to see laymen become successfully in so many arena, mention politics, business, sports, technology to mention a few, while the so called professors, dr and other academicians tunashindwa kuacha legacy ktk maisha halisi na mahitaji ya jamii zetu. Na hili ni common hasa ktk ulimwengu wetu wa tatu.
Mfano wakati nikiwa kijana mdogo niliona ndoa za wasomi wa vyuo zikiwa taabani, nikawa najiuliza sasa kwa wasomi ni hivi je wasiosoma itakuwaje.
Pamoja bado naamini wasomi wana michango mizuri katika maeneo yao ya expertise japo wengine wanakosa practice ya field.

Ndio maana nikamjibu ndugu hapo tuli-relax, tuwe flexible..

Mimi sio lecturer nimeshauri tu kwa kuwa uandishi uliotumika kwenye uzi sio professional. Lecturer anetegemewa kutokuandika lugha ya kitaalam katika masuala ya kijamii lakini anapoandika kama vijana wa kileo ninashawishika kumshauri.

Assume hao malecture wenzio waje watuhadithie mambo ya mabinti kuandika kwenye mapaja siamini kama ndio changamoto mnazotaka kujadiliana hapa.
 
Mimi sio lecturer nimeshauri tu kwa kuwa uandishi uliotumika kwenye uzi sio professional. Lecturer anetegemewa kutokuandika lugha ya kitaalam katika masuala ya kijamii lakini anapoandika kama vijana wa kileo ninashawishika kumshauri.

Assume hao malecture wenzio waje watuhadithie mambo ya mabinti kuandika kwenye mapaja siamini kama ndio changamoto mnazotaka kujadiliana hapa.
Amin amin nakuambia..hapa watakuja wachache sana..kuna tatizo kubwa la baadhi au wengi wa wahadhiri wetu kwenye kujiamini wengi wanasumbuliwaga na intellectual arrogance ..ndio.maana wanapelekea vijana kukariri vi slide vya powerpoint tuuu...mijadala ya wazi kama hapa wanasepa...
 
Mimi sio lecturer nimeshauri tu kwa kuwa uandishi uliotumika kwenye uzi sio professional. Lecturer anetegemewa kutokuandika lugha ya kitaalam katika masuala ya kijamii lakini anapoandika kama vijana wa kileo ninashawishika kumshauri

Assume hao malecture wenzio waje watuhadithie mambo ya mabinti kuandika kwenye mapaja siamini kama ndio changamoto mnazotaka kujadiliana hapa.

Aksante.

Hata hivyo, kwa uzoefu wangu hiyo niliyoitaja ni changamoto kubwa sana tu. Inaitwa udanganyifu ama 'cheating' wanafunzi wengi ni wahanga wa hili. Mara nyingi linaleta ugomvi ama chuki baina ya wahusika. Nimetumia lugha rahisi ya kawaida kwa jamii. Kwa walengwa wameielewa hasa, wengi wa wanafunzi ni vijana na pia majaribu haya yanawakumba hasa walimu vijana na sio sana kwa wazee au watu wazima sana. Namaanisha hadhira husika imepata ujumbe juu ya changamoto hii.
 
Aksante.

Hata hivyo, kwa uzoefu wangu hiyo niliyoitaja ni changamoto kubwa sana tu. Inaitwa udanganyifu ama 'cheating' wanafunzi wengi ni wahanga wa hili. Mara nyingi linaleta ugomvi ama chuki baina ya wahusika. Nimetumia lugha rahisi ya kawaida kwa jamii. Kwa walengwa wameielewa hasa, wengi wa wanafunzi ni vijana na pia majaribu haya yanawakumba hasa walimu vijana na sio sana kwa wazee au watu wazima sana. Namaanisha hadhira husika imepata ujumbe juu ya changamoto hii.

Hoja yako kwa maana ya academic dishonest ni changamoto kwelikweli ila maelezo ya kuhusu mapaja hayakuwa na tija. Hata hivyo hiyo ni mbinu ya kizamani sana vijana tuliomaliza enzi za JK tulishuhudia mbinu mpya na za kisasa. Japo zinaweza kutumika na wale wanaotumia extra materials kufanya mitihani
 
Amin amin nakuambia..hapa watakuja wachache sana..kuna tatizo kubwa la baadhi au wengi wa wahadhiri wetu kwenye kujiamini wengi wanasumbuliwaga na intellectual arrogance ..ndio.maana wanapelekea vijana kukariri vi slide vya powerpoint tuuu...mijadala ya wazi kama hapa wanasepa...

Upo sahihi kabisa kiongozi ndo maana nataka wenzangu waache vyeo vyao na 'academic arrogance' tujadili mambo ya kawaida kabisa na wanafunzi wetu au wanataaluma wenzetu...

Siku nilijifunza kuwa mnapokuwa chuo ni sehemu muhimu kujenga mahusiano ya haki, heshima na kitaaluma na wanafunzi wako sababu huijui kesho.

Siku moja nilikuwa nasafiri kwenda nje ya nchi. Bahati mbaya nilikuwa najiamini mizigo yangu uzito upo sawa. Kuingia ndani wakati huo nimeshabadilisha Tsh zote. Kuanza kupima kumbe uzito umezidi. Muhusika akanambia nilipie nikamwambia sina Tsh nina pesa ya kigeni tu akanambia Nop nenda nje kabadilishe huku nikichek muda naona unaenda. Ghafla nikasikia mtu ananiita, sikumtambua akanambia njoo, shida ni nini? Nikamueleza, alichofanya alichukua tiketi yangu na kuigonga then kanambia niondoke. Kuja kuchek kumbe ni mwanafunzi wangu.
 
Hoja yako kwa maana ya academic dishonest ni changamoto kwelikweli ila maelezo ya kuhusu mapaja hayakuwa na tija. Hata hivyo hiyo ni mbinu ya kizamani sana vijana tuliomaliza enzi za JK tulishuhudia mbinu mpya na za kisasa. Japo zinaweza kutumika na wale wanaotumia extra materials kufanya mitihani
Kiongozi ebu zitaje hizo mbinu hapa. Maana kama ninasimamia mtihani mwanafunzi anaye cheat nitamdaka tu bila shaka nikitaka.
 
Mfano mtu anaweza kuprint statistical tables zake zikiwa na added information
Hiyo ni kweli ni rahisi mwl kutotambua ila nikwambie kitu; unless huyo mwanafunzi awe ni mzoefu ktk cheating anaweza pona na wasimamizi wasiwe serious na wawe wachache kinyume na hapo ni rahisi kumkamata sababu ya hofu atakayokuwa nayo mara mwl akipita au kumtazama. Kwa mwl ukiona tu mwanafunzi ana hofu isiyo ya kawaida jua kuwa kuna jambo.
Muda mwingine tunatumia mbinu ya kusimama kwa muda mrefu jirani na mwanafunzi unayemuhisi. Kwa vyovyote vile atashindwa kuandika chochote so inakula kwake.
Pili huwa baadhi ya wanafunzi wanavujisha mbinu zao kwa walimu na muda mwingine tunaweza kuwa na majina ya waliokubuhu michezo hiyo hasa kwa madarasa/kozi za watu wachache.
 
Duuuuuu kama wewe ni lecture mi nachoma magamba yangu yote
Hamna lecture mwenye mwandiko km wewe, labda lecture wa saut songea
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom