Learn From History: Kama Waziri Huyu Alitunga Uongo Huu, Kuwa Waandishi Wametishia Kumuua!, Then..

Mkuu Pascal embu kwa vitu vingine uwe unatumia ile ID nyingine bhana.....
Hatutaki kumpoteza hata mmoja wetu humu.......
Hali ni tete..pongezi na maandamano ya pongezi kila kona..wew unaleta hizi to the public?

Pls .....
Kweli hata mimi nimestuka kweli kweli. Kuna jambo linaendelea na inawezekana "Bwana Njaa" kaamua kujitoa mhanga!
 
sio vibaya bwana paskali ukatupa kidogo fununu za nani walikuwa wamiliki wa gazeti hilo kwa kipindi hicho ambacho makala nyingi kumhusu huyo waziri tajwa zilifululiza.

Tukishawafahamu; tutaweza kujua na marafiki zao pia.

Itatusaisia sana kujenga hoja zetu kumhusu na kuhusiana na hizo allegations.
 
stroke hapa habari ni kwamba waziri alipofungua kesi hakurudi tena kuifuatilia. Halafu ni ajabu unatishiwa kuuawa na waandishi wa habari na wewe unakaa kimya, tena mmojawapo anakuja kuwa Mkuu wa wilaya na wewe wala hustuki!
 
Hongera sana mkuu mayalla kwa review nzuri na inayofaa kukumbukwa kwa kila kizazi na wazalendo Wa kweli wasiokuwa na alama ya unafiki, ama hakika ni heri kumuombea mtu ambaye penye zuri anasifia na penye baya anakemea kuliko yule anayekata kuombewa tu ilhali hayupo tayari kujitafakari au kurudi nyuma pale anapokosea. Mungu aendelee kukuweka hai,akujaalie nguvu na hekima katika kazi zako
 
Kwa bandiko hili la Mayallah,kiti cha mkuu wa wilaya ya Makete nichamoto na lolote laweza tokea ikiwemo cheo cha mtu kutenguka

Makada na watanzania wengine wanaojua "K3" wajiandae kulamba bingo maana uteuzi mpya unahusika hapa
 
Kinachonitisha ni kwamba huyo former minister ni mnafiki anaeweza kusema uongo mpaka akauapia ili uwe ukweli.... hutumia nguvu sana kujinasibu yu Msafi kumbe fisadi tuuu....

Siku niliyoenda kwao akatuomba tumtolee sadaka mamake ndo siku niliyobaini dhahiri huyu ni fisadi aliyevaa miwani ndani ana macho ya kondoo
 
Kuna usemi usemao Once muongo always muongo. Kama mtu na madaraka makubwa ya uwaziri unaenda Polisi na kufungua mashtaka ya uongo kuwa unatishiwa kuuwawa na masikini waandishi wa habari vipi ukipata madaraka zaidi ambayo hayahojiwi utafanya nini kwa binadamu wenzako? Ni wazi utawatungia vitu vingi vya ajabu ili kuwakomesha na huku ukiandaa vijana wa kuandamana kukusifu kwa nyimbo na mapambio kuwa unatenda haki.
Hiki ni kisa cha kusikitisha sana, na kwa kweli ingekuwa ni nchi za wenzetu walio starabika hili jambo lingeibuliwa kwa uwazi zaidi maana ni kosa kubwa la kijinai na linaweza kumtoa mtu ofisini kwani ni ukosefu wa maadili ya kiuongozi.
Paskali asante sana kwa somo la historia, hili litasababisha wale vijana wa juzi wasiojua "watu" na wanasukumwa na nguvu ya upepo wajiulize mara mbili mbili jee propaganda wanazolishwa ni kweli? Au wanafanywa wajinga!
 
Kinachonitisha ni kwamba huyo former minister ni mnafiki anaeweza kusema uongo mpaka akauapia ili uwe ukweli.... hutumia nguvu sana kujinasibu yu Msafi kumbe fisadi tuuu....

Siku niliyoenda kwao akatuomba tumtolee sadaka mamake ndo siku niliyobaini dhahiri huyu ni fisadi aliyevaa miwani ndani ana macho ya kondoo
Ukienda mbali zaidi, utaona kuwa pengine hata yule dada adui yake mkubwa mitandaoni yaweza kuwa asilimia kubwa ya yale asemayo kuhusu former minister yaweza kuwa na ukweli.
 
Wanabodi,

Declaration of interest: Mimi ni mpenzi wa somo la historia, ambalo ni somo la mambo ya zamani, kuwianisha na mambo ya sasa, ili kujua mambo yajayo. Hivyo kila nipatapo fursa, hupekua kwenye historia ya mambo ya zamani na kulinganisha ni hiki kinachoendelea sasa, ili kujua nini kitakachokuja kutokea siku za baadae.

Leo nimekikumbuka kisa cha waandishi fulani wawili wa habari, ambao walishitakiwa kituo cha polisi Mabatini kwa kosa la kutishia kumuua, waziri fulani.

Kisa chenyewe ni kwa waziri huyo, baada ya kuandikwa vibaya na gazeti hilo, aliamua kubuni kesi ya kizushi, kwa kutunga uongo kuwa waandishi hao wa habari, wamemtishia maisha kuwa watamuua!, akaenda kuripoti uongo huo kituo cha polisi cha Mabatini ili kuwakomoa waandishi hao washughulikiwe!, na kweli waandishi wale walishughulikiwa kwa kuitwa polisi na kuhojiwa, kisha kuachiwa kwa dhamana kusubiria muendelezo wa hiyo kesi. Kilichofuata Waziri hakurudi tena kituoni kuthibitisha madai yake, kwa vile yalikuwa ni madai ya uongo!, hivyo kesi ikafa natural death.

Sasa kama tuhuma hii ni kweli, mtu anaweza kumzushia binadamu mwenzake tuhuma nzito kama hii, then this leaves much to be desired in the present situation and in future!. Mkumbuke, binadamu anaweza kubadili tuu tabia, lakini hulka huwa haibadiliki, anaweza tuu kuificha, lakini siku ya siku hulka huibuka!.



NB. Hili ni bandiko la ma GT, hivyo naombeni sana tusitaje taje majina.
Angalizo: Kwa wasio fahamu essence ya somo la Historia, naombeni sana, mjipitie tuu kwenye uzi huu na kujiendelea zenu na safari zenu, pia naomba nisiulizwe jambo lolote kuhusu mkasa huu kwa sababu jukumu langu ni kuwaletea historia tuu.

Kitendo cha kuripoti kitu cha uongo kwenye kituo cha polisi ni kosa la jinai, na makosa ya jinai, hayana time limitation, hivyo kesi hiyo ya kuripoti uongo kwenye kituo cha polisi, inaweza kuibuliwa wakati wowote na mhusika akapandishwa kizimbani!.

Hivyo tujifunze kutoka historia, Kama Waziri Huyu Aliweza Kutunga Uongo Huu, Kuwa Waandishi Wametishia Kumuua!, Then...

Paskali


Mkuu Paskali, vipi? Kila ukiandika unaponda kiaiana. Kwema kaka?
 
Back
Top Bottom