Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Atakuoa bila kukupenda!?Nasema hivi mume anayempenda mkewe ndiyo anayestahili utii na siyo vinginevyo narudia tena mume anayempenda mkewe ndiyo anayestahili utii na si vinginevyo
Mungu hawezi mpangia ndoa kichwa maji kama wewe...unaonekana ulishindikana sehemu na bado inakuuma,itakua umri umeenda huna tumaini la ndoa.Yaani mnavyoongeaga hizo kauli mnajikutaga miungu wenyewe mnadhani mnamkomoa nani sasa? Kwa Mungu mwanaume malaya na mwanamke malaya wote wana dhambi
Na kama ni kwenye jamii sidhani kama siku hizi wanawake tunajali tena jinsi tutakavyoonekana kwenye jamii yaani wanawake wa hivyo wamebaki wachache mno na ndo hao ambao wako tayari kuwa hata watumwa kwa wanaume ili tu waolewe lakini wengine tushashituka siku hizi
Ndoa anapanga Mungu na siyo binadamu na Mungu hakumleta mwanamke duniani aje ateseke wala kuwa mtumwa wa mwanaume na wala Mungu hakutaka ndoa zile za mwanamke kujifanya mjinga hata kama mumewe kakosea vipi
Dunia imeshabadilika siku hizi wanaume kubalianeni tu na hali halisi na kama mnaona kuwa hao wanawake mnawatumia endeleeni kujidanganya maana sidhani kama unaweza kusema eti unamtumia mtu ambaye anafanya kitu kwa raha zake
Haya Ni maneno yako.we huoleki na hutokuja kuolewa kamwe
Watapita kama hawaoni hii komentiMwanaume yupo juu siku zote na atabaki kuwa juu.
Mwanaume amepewa nafasi ya kuwa kichwa katika familia .
Mwanamke ameagizwa utii kwa mumewe
Mwanaume ameagizwa kuishi na mwanamke wa akili.,pia kumpenda mkewe
Tatizo huja pale wanaume wengi wanapokosa akili za kuishi na wake zao,,,hawawezi kusimama katika nafasi zao ipasavyo.
Shida huanzia kwa Mwanaume...
Mipango yote huanzia kichwani...
Kichwa huamua Nini mguu ufanye na Nini usifanye ,,Nini mkono ufanye Nini usifanye
Kama kichwa hakina maamuzi mazuri hata mwili pia utakaa vibaya
Vivyohivyo kiburi kwa mwanamke Ni matokeo ya mumewe kushindwa kusimama vema kwenye nafasi yake Kama kichwa
WanapwayaHivi ninyi mnaohangaika na kulialia hamheshimiwi ni wanaume kweli
Hivi mkeo anashindwa vipi kukutii? Hebu mjitathmini kama mnatosha kwenye hizo nafasi.
Amen...!Nasema hivi mume anayempenda mkewe ndiyo anayestahili utii na siyo vinginevyo narudia tena mume anayempenda mkewe ndiyo anayestahili utii na si vinginevyo
Hii umeandika as if mabadiliko haya yameathiri upande mmoja tu wa ke.Tukiwaambia "haki sawa" ni mchochezi wa kuvunja ndoa wabishi kama mawe yapigwayo na mawimbi baharini lkn hayatakati kamwe!
Wazazi wa kizazi hiki wanalea watoto kimayai mayai bila kujua wanawaanda wake za Watu kizazi cha kesho.
Mwanamke anamaliza form six hajui kupika, kufua nguo wala kudeki nyumba zaidi ya kufuga kucha kama paka shume.
Binti yuko darasa la 3 kashajua kila aina ya mitandao inayohamasisha ngono na kujibu Watu hovyo hovyo matusi bila aibu wala hofu.
USA & ULAYA kiujumla wameshavunja ndoa sana kupitia hilo pepo la "haki sawa" hadi kuongoza idadi kila mwaka duniani na kuamua wafunge ndoa za mikataba ambazo ni kinyume na Mungu.
Wanaume wenye hekima sasa hivi wanaogopa Wanawake wasomi na wenye ajira zao kama ebola, hujiulizi kwanini ndoa nyingi sana zenye changamoto ktk maelewano ni hao hao wasomi?
Mungu atusaidie sana tuliojaliwa upeo kuona mbele zaidi athari za ulimbukeni wa kuiga iga utandawazi toka nchi za magharibi unaochangia kiasi kikubwa sana kuathiri mila na desturi zetu Waafrika hadi kuharibu matunda mazuri ya ndoa bora.
Naomba muitunze hii sms kuwa ushuhuda ili miaka 10 ijayo iwe ushahidi Mungu akipenda tuwe hai.
Kwa mawazo yako unadhani kuna mtu unamkomoa, si mpaka umpate huyo wa kumtumia sasaWaache waendelee na mashindano si wanadhani kuna tuzo
Watu wenyew wako kibao afu waendelee kutuumiza kichwa ni kuwatumia na kuwatupa huko
Na utii bila Upendo mnataka sisi tukachukue wapi?Upendo bila utii utoke wapi? Naweza kukupenda kama mke wangu ila huna utii hakiamungu usione huo upendo unaohitaji.
AmenBasi sawa roho wa bwana aweke utii ndani yetu sie wanawake na nyie mtupende sawasawa kama kristo alivyolipenda kanisa...
Na ninyi mnapokuwa na matabia ya hovyo mbona mnasingiziq sisi ndio tunasababisha?Mm hili jambo silikubali kwa 100%... HV hakuna wanawake viburi naturally??
HV hakuna wanawake wenye Tania mbaya naturally??
Iweje mke akiwa na tabia mbaya mseme n lazma mume kahusika kumfanya awe na tabia mbovu??
Umesema kweli mkuu ndoa si mashindano na hata ukisema unamkomoa kila mwanamke mwisho wa siku utakayeumia ni weweKila mwanamke ana akili zake......hata mkiongea sana hii battle hakuna atakayeshinda.....mwisho wa siku maisha yataendelea...ndoa n kusaidiana,kuvumiliana na kupendana.
Ngoja nikwambie, hakuna mwanamke anapenda kuwa juu ya mwanaume. Mwanamke anafeel secured anapokuwa yupo chini ya mwanaume wake, ndoto ya kila mwanamke ni kupata mwanaume anayejielewa ili amtii na kumsikiliza for the rest of her life ila inapotokea kinyume chake mwanamke anaona haina haja ngoja wote wawili tushike usukani vinginevyo chombo kitatumbukia shimoniWanawake wa siku hizi wanaviburi sana wanataka kuwa juu ya wanaume ndio maana ndoa nyingi zinavunjika na wanawake wengi kuwa ma single mother's
HayaAhsante rafiki!
But will confirm tomorrow
Heee mkuu umelichoka kweli kweli duhKwa ujeuri wao ndo maana mengi yanakua singo maza.
Mimi nimeliacha moja lilikua lijeuri,sasa wanaligonga tu na kuliacha,juzi limenipigia simu oooh umeniroga ndo maana sipati mume,nikaliambia mchawi ni domo lako kama chai jaba.