Lazima mke ashuke tu kwa mumewe vinginevyo hakuna ndoa

Tukiwaambia "haki sawa" ni mchochezi wa kuvunja ndoa wabishi kama mawe yapigwayo na mawimbi baharini lkn hayatakati kamwe!

Wazazi wa kizazi hiki wanalea watoto kimayai mayai bila kujua wanawaanda wake za Watu kizazi cha kesho.

Mwanamke anamaliza form six hajui kupika, kufua nguo wala kudeki nyumba zaidi ya kufuga kucha kama paka shume.

Binti yuko darasa la 3 kashajua kila aina ya mitandao inayohamasisha ngono na kujibu Watu hovyo hovyo matusi bila aibu wala hofu.

USA & ULAYA kiujumla wameshavunja ndoa sana kupitia hilo pepo la "haki sawa" hadi kuongoza idadi kila mwaka duniani na kuamua wafunge ndoa za mikataba ambazo ni kinyume na Mungu.

Wanaume wenye hekima sasa hivi wanaogopa Wanawake wasomi na wenye ajira zao kama ebola, hujiulizi kwanini ndoa nyingi sana zenye changamoto ktk maelewano ni hao hao wasomi?


Mungu atusaidie sana tuliojaliwa upeo kuona mbele zaidi athari za ulimbukeni wa kuiga iga utandawazi toka nchi za magharibi unaochangia kiasi kikubwa sana kuathiri mila na desturi zetu Waafrika hadi kuharibu matunda mazuri ya ndoa bora.

Naomba muitunze hii sms kuwa ushuhuda ili miaka 10 ijayo iwe ushahidi Mungu akipenda tuwe hai.
Kwahiyo una maana kuwa huo utandawazi mbovu umewakumba watoto wa kike tu? Si wapo na wa kiume ambao umewakumba au kwa watoto wa kiume ukiwakumba ni sawa?

Halafu unaposema eti ni lazima mwanamke ukitaka kumuoa umkuta anajua kufanya kazi za nyumbani zote unamaanisha nini? Unamaanisha kwamba hauwezi kumvumilia mwanamke ambaye hatatimiza majukumu yake si ndiyo?

Kwahiyo unataka kusema kwamba na sisi wanawake tusiolewe na wanaume ambao hawajui kutafuta pesa tusubiri wakishatafuta wakapata ndo tukaolewe nao si ndiyo? Maana hata sisi hatuwezi kuwavumilia wanaume ambao hawataweza kutimiza majukumu yao

Kwa mitazamo hii acha tu na sisi wanawake tuendelee kutafuta wanaume wenye pesa tu kwa kweli haiwezekani wanaume mshindwe kutimiza majukumu yenu kwa kisingizio cha kuwa hamna uwezo halafu mnataka wake zenu watimize majukumu yao yote tena wawasaidie na ya kwenu kabisa halafu nyie kuwasaidia ya kwao hamtaki mnaita umume bwege
 
Waache waendelee na mashindano si wanadhani kuna tuzo

Watu wenyew wako kibao afu waendelee kutuumiza kichwa ni kuwatumia na kuwatupa huko
Yaani mnavyoongeaga hizo kauli mnajikutaga miungu wenyewe mnadhani mnamkomoa nani sasa? Kwa Mungu mwanaume malaya na mwanamke malaya wote wana dhambi

Na kama ni kwenye jamii sidhani kama siku hizi wanawake tunajali tena jinsi tutakavyoonekana kwenye jamii yaani wanawake wa hivyo wamebaki wachache mno na ndo hao ambao wako tayari kuwa hata watumwa kwa wanaume ili tu waolewe lakini wengine tushashituka siku hizi

Ndoa anapanga Mungu na siyo binadamu na Mungu hakumleta mwanamke duniani aje ateseke wala kuwa mtumwa wa mwanaume na wala Mungu hakutaka ndoa zile za mwanamke kujifanya mjinga hata kama mumewe kakosea vipi

Dunia imeshabadilika siku hizi wanaume kubalianeni tu na hali halisi na kama mnaona kuwa hao wanawake mnawatumia endeleeni kujidanganya maana sidhani kama unaweza kusema eti unamtumia mtu ambaye anafanya kitu kwa raha zake
 
1. Rejea kichwa cha habari ujue kinataka nini.

2. Fungua uzi kuhusu Marioo ili ujenge hoja yako vizuri.

3. Pole kwa kuolewa na Mwanaume kilema wa akili/asiyetambua wajibu wake ktk ndoa.

4.Karibu tena.
Kwahiyo una maana kuwa huo utandawazi mbovu umewakumba watoto wa kike tu? Si wapo na wa kiume ambao umewakumba au kwa watoto wa kiume ukiwakumba ni sawa?

Halafu unaposema eti ni lazima mwanamke ukitaka kumuoa umkuta anajua kufanya kazi za nyumbani zote unamaanisha nini? Unamaanisha kwamba hauwezi kumvumilia mwanamke ambaye hatatimiza majukumu yake si ndiyo?

Kwahiyo unataka kusema kwamba na sisi wanawake tusiolewe na wanaume ambao hawajui kutafuta pesa tusubiri wakishatafuta wakapata ndo tukaolewe nao si ndiyo? Maana hata sisi hatuwezi kuwavumilia wanaume ambao hawataweza kutimiza majukumu yao

Kwa mitazamo hii acha tu na sisi wanawake tuendelee kutafuta wanaume wenye pesa tu kwa kweli haiwezekani wanaume mshindwe kutimiza majukumu yenu kwa kisingizio cha kuwa hamna uwezo halafu mnataka wake zenu watimize majukumu yao yote tena wawasaidie na ya kwenu kabisa halafu nyie kuwasaidia ya kwao hamtaki mnaita umume bwege
 
Katika miaka ya karibuni kumekuwa na upungufu mkubwa wa wanawake wazuri. Kwa sura, shape au mwonekano hasa mijini.

Pengine hii inatokana na mabadiliko ya tabia ya nchi na ukweli kwamba watu siku hizi hawapati lishe bora kama walivyopata wazee wetu.

Kupungua kwa idadi ya wanawake wazuri hasa katika jiji la Dar Es Salaam' Mbeya nk.. kumeendana pia na ongezeko la wanawake wenye viburi, lugha mbaya, wabishi, wagomvi na kwa ujumla washamba wa mahba.

Lugha mbaya inamfukuza mume nyumbani. Kiburi kinamkosesha mke zawadi. Gubu linamfanya mume ajifunze kwenda baa hata kama hiyo sio style yake.

Tabia ya kumchunga sana mumeo na kushindana nae kila mara huichimbia ndoa kaburini kama unaitaka ndoa yako basi usimjibu vibaya mumeo hasa mbele za watu na hasa rafiki zake.

Mpokee mumeo akirudi kazini hata kama umetingwa kiasi gani. Usimtume house girl kumpokea mzigo mumeo. Ni kosa la kiufundi.

Mwite mumeo kwa jina lake la kwanza. Usimwite 'wee' au 'huyu'... Sio sahiii. Na mume vilevile usimwite mkeo wewe au huyu!!

Ndoa inastawi au kubomoka kwa vitu vidogo sana. Yanasema maandiko kwa mujibu wa Paulo: "Enyi wake watiini waume zenu. Nanyi wanaume wapendeni wake zenu"

Kuna amri kuu mbili za kuzingatia ili ndoa idumu.
Kwanza, ni lazima mke amheshimu na kumtii mumewe.

Pili ni wajibu wa mume kumtunza na kumthamini mkewe kwa kila hali. NB: kulingana na uwezo wa mwanaume husika ni busara pia kwa mwanamke kuridhika na hali ya kiuchumi ya mumewe.

Mke akiwa na tamaa ni chanzo cha mifarakano katika ndoa. Kama huwezi kuvumilia hali yake ni bora muachane kuliko kumpa stress kila siku kaka wa watu.

Najua siku hizi wanawake wengi wana vipato vikubwa na wengine hiyo huwa sababu ya kuwadharau au kutaka kushindana na waume zao ukweli mchungu ni kwamba kama unataka ndoa lazima uwe submissive kwa mumeo.

Kama kipato kinawazuzua na mnaona hamuwezi kumtii mume ni bora akina dada wa aina hii waishi peke yao.
Wanawake pitieni huku kuna tiba yenu huku, wasipokuelewa basi aliyewaroga atakuwa kafa.
 
1.Rejea kichwa cha habari ujue kinataka nini.

2.Fungua uzi kuhusu Marioo ili ujenge hoja yako vizuri.

3.Pole kwa kuolewa na Mwanaume kilema wa akili/asiyetambua wajibu wake ktk ndoa.

4.Karibu tena.
Mkuu siyo kila anayetetea vichaa basi na yeye ni kichaa hivyo basi siyo kwa sababu nimewatetea wanawake walioolewa na marioo basi na mimi nimeolewa na marioo kwanza kabisa mimi sijaolewa na mpenzi wangu naweza kusema anajitahidi sana katika kusimamia nafasi yake na kutimiza wajibu wake kwangu lakini nimeamua niwaseme wale wanaume ambao siku hizi nao wanatafuta wanawake ambao wana akili ya maisha au ambao wanajua kutafuta pesa

Ili wawasaidie hao wanaume kutafuta pesa na kuhudumia familia kumbe mnajua kuwa wanaume wa design hiyo wapo na ndo hao marioo sasa mbona hamuwasemi kutwa kutusema wanawake tu niamini mimi mwanamke akishaanza kuingilia majukumu ya mume wake lazima tu atakuwa na dharau huyo mume atake asitake na kama hataki basi ndo atimize majukumu yake yote kama mwanaume bila kusubiri mke amsaidie
 
Sisi tunatambua tangu muda mrefu,yaani mkituheshimu na kututii,hapo hakuna uchawi wala ndumba,sisi tutawapenda na kuwajali mpaka mjishangae
Tatizo kuheshimu na kutii mnakotaka nyie ni ile mkifanya makosa tukae kimya tusiongee chochote na mkiamua jambo basi ndo mmeamua hamtaki kukosolewa hamtaki kurekebishwa hamtaki kushauriwa wala hamtaki kuambiwa ukweli

Ndo heshima mnayoitaka hiyo si ndiyo? Halafu kwanini mwanamke ndo aanze kutii halafu mwanaume ndo afuate kupenda? Kwanini mwanaume ndo asianze kupenda halafu mwanamke akaanza kutii?

Biblia haijasema nani aanze ila kumbuka wanaume ndo mlianza kuumbwa na nyie ndo mnaotongoza sasa kama ambavyo mnataka muwe viongozi kwenye kila kitu tunaomba pia muwe viongozi hata kwenye mapenzi ninyi ndo muanze kuonyesha huo upendo halafu muone kama wake zenu hawatawaonyesha utii

Na tunaposema kupenda tunamaanisha ni pamoja na kutokusaliti wake zenu achaneni na huo utafiti uchwara kuwa eti mwanaume anaweza akamsaliti mume na bado akawa anampenda hakuna kitu ambacho kama hicho hivyo basi mwanaume anayemsaliti mkewe hatakiwi kupewa utii na mkewe sasa kwa sababu dunia ya sasa wanaume hamuwapendi wake zenu mnawasiliti basi ndo maana hata wanawake hawawatii waume zao wanawadharau
 
Tatizo kuheshimu na kutii mnakotaka nyie ni ile mkifanya makosa tukae kimya tusiongee chochote na mkiamua jambo basi ndo mmeamua hamtaki kukosolewa hamtaki kurekebishwa hamtaki kushauriwa wala hamtaki kuambiwa ukweli

Ndo heshima mnayoitaka hiyo si ndiyo? Halafu kwanini mwanamke ndo aanze kutii halafu mwanaume ndo afuate kupenda? Kwanini mwanaume ndo asianze kupenda halafu mwanamke akaanza kutii?

Biblia haijasema nani aanze ila kumbuka wanaume ndiyo mlianza kuumbwa na nyie ndo mnaotongoza sasa kama ambavyo mnataka muwe viongozi kwenye kila kitu tunaomba pia muwe viongozi hata kwenye mapenzi ninyi ndo muanze kuonyesha huo upendo halafu muone kama wake zenu hawatawaonyesha utii

Na tunaposema kupenda tunamaanisha ni pamoja na kutokusaliti wake zenu achaneni na huo utafiti uchwara kuwa eti mwanaume anaweza akamsaliti mume na bado akawa anampenda hakuna kitu ambacho kama hicho hivyo basi mwanaume anayemsaliti mkewe hatakiwi kupewa utii na mkewe sasa kwa sababu dunia ya sasa wanaume hamuwapendi wake zenu mnawasiliti basi ndo maana hata wanawake hawawatii waume zao wanawadharau
Umeongea meengi sana katika comment yako,ila kwa uvivu wangu wa kuandika naomba nikuambie machache.

Angalia namna unavyoongea na mmeo,sio unaongea kama uko saloon alafu unasema unashauri ,

Maandiko kamwe hayajipingi kasome tena,ilivyoandikwa katika Bible basi wewe yakupasa utekekeze ,na hapo utajua nani anapaswa kuanza kutekeleza hayo

Kuchepuka ile tafiti iko real, wanaume tunachepuka kwa kukata tamaa tu,ila mwanamke akichepuka kapenda kweli,na siri zote za ndani atatoa.

Hivyo mkitutii na kutuheshimu amini nakwambia hata bar nyingi zitakosa wateja. ,
 
Mwanaume yupo juu siku zote na atabaki kuwa juu.
Mwanaume amepewa nafasi ya kuwa kichwa katika familia .
Mwanamke ameagizwa utii kwa mumewe
Mwanaume ameagizwa kuishi na mwanamke wa akili.,pia kumpenda mkewe
Tatizo huja pale wanaume wengi wanapokosa akili za kuishi na wake zao,,,hawawezi kusimama katika nafasi zao ipasavyo.

Shida huanzia kwa Mwanaume...
Mipango yote huanzia kichwani...
Kichwa huamua Nini mguu ufanye na Nini usifanye ,,Nini mkono ufanye Nini usifanye
Kama kichwa hakina maamuzi mazuri hata mwili pia utakaa vibaya

Vivyohivyo kiburi kwa mwanamke Ni matokeo ya mumewe kishindwa kusimama vema kwenye nafasi yake Kama kichwa
Asante Chief
 
Umeongea meengi sana katika comment yako,ila kwa uvivu wangu wa kuandika naomba nikuambie machache,,
Angalia namna unavyoongea na mmeo,sio unaongea kama uko saloon alafu unasema unashauri ,

Maandiko kamwe hayajipingi kasome tena,ilivyoandikwa katika Bible basi wewe yakupasa utekekeze ,na hapo utajua nani anapaswa kuanza kutekeleza hayo

Kuchepuka ile tafiti iko real, wanaume tunachepuka kwa kukata tamaa tu,ila mwanamke akichepuka kapenda kweli,na siri zote za ndani atatoa.

Hivyo mkitutii na kutuheshimu amini nakwambia hata bar nyingi zitakosa wateja. ,
Kwahiyo ninyi hamuwezi kuanza kuwapenda wake zenu halafu wao ndo wakafuata kuwatii?
 
Kwahiyo ninyi hamuwezi kuanza kuwapenda wake zenu halafu wao ndo wakafuata kuwatii?
Toka tunapowatongoza automatically huwa sisi ndio tumeeaza kuwapenda, kinachosalia huwa ni wajibu wenu kutuheshim na kututii,na ukipunguza kimoja wapo basi lazima uhisi upendo unaanza kupungua.
 
Kama mume ananipenda basi hakika na mimi namtii hakuna hilo halina ubishi hapo
Upendo bila utii utoke wapi? Naweza kukupenda kama mke wangu ila huna utii hakiamungu usione huo upendo unaohitaji.
 
Haaa jamani siyo nyie mnaosemaga kwamba mkiwa mnatongoza ile mara ya kwanza mnakuwa hamjatupenda bali mnakuwa mmetutamani tu halafu upendo wenu utategemea na tabia za hao wanawake mliowatongoza?
Toka tunapowatongoza automatically huwa sisi ndio tumeeaza kuwapenda,kinachosalia huwa ni wajibu wenu kutuheshim na kututii,na ukipunguza kimoja wapo basi lazima uhisi upendo unaanza kupungua
 

Similar Discussions

57 Reactions
Reply
Back
Top Bottom