Lazima Lowassa ashitakiwe kwa Ufisadi!!

Allen Kilewella

JF-Expert Member
Sep 30, 2011
18,113
33,609
Kiashiria cha udhaifu kwa binadamu wakati mwingine ni pale anaposhindwa kulifikisha mwisho jambo la muhimu analotakiwa kulikamilisha. Sisi kama taifa tumekuwa tunatangatanga na Jambo lililosababishwa na mtu mmoja tu na sisi kama taifa tumeshindwa kufikia mwisho wake.

Tarehe 7/2/2008 aliyekuwa Waziri wa Mkuu wa Tanzania wakati ule, Edward Ngoyai Lowassa alijiuzulu wadhifa wake baada ya kutuhumiwa kuingilia mchakato wa Zabuni ya Ufuaji Umeme iliyosababisha kuletwa kwa Kampuni ya Ufuaji Umeme ya Richmond nchini. Tangu kujiuzulu kwa Lowassa mpaka sasa imeshapita miaka zaidi ya 8 na miezi kadhaa, lakini bado suala la sakata la Richmond halijaisha

Mitambo iliyoletwa na Kampuni ya Richmond ambayo bado ipo Pale Pale ilipofungwa na Kampuni ya Richmond, imeshabadilishwa umiliki wake mara mbili. Imetoka kwa Richmond ikanunuliwa na Dowans na sasa inamilikiwa na Kampuni ya Symbion ya Marekani. Lakini sisi kama taifa tumeachwa pale pale tulipokuwa Mwaka 2008.

Kwa kuwa kuna Mahakama ya Mafisadi inaundwa na sisi kama taifa tunayumbishwa na suala la mtu mmoja tu, ambaye si kiongozi wa serikali kwa sasa, nashauri Kesi ya Kwanza kwenye Mahakama ya Mafisadi iwe ni hii ya "Ufisadi" wa Edward Ngoyai Lowassa kuhusu Ufisadi wa zabuni ya ufuaji umeme iliyosababisha Sakata la richmond.

Ni lazima Lowassa ashitakiwe ili kama yeye anao ushahidi tofauti na ule ambao wapinzani wake wanao aje nao mahakamani ili upimwe kwenye mizani ya kisheria tujue nani mkweli kati yake yeye na wapinzani wake.

Haiwezekani mitambo ile iliyoletwa na Kampuni (Feki?) ya Richmond bado ipo nchini mwetu, inafua umeme, Tannesco wanalipa Capacity charges tanesco wanauziwa umeme kutokana na mitambo ile ile iliyokuwa ya Richmond, mkataba ule ule wa kati ya Richmond na Tannesco ndiyo umekuwa ukihuhishwa na Dowans na sasa Symbion, lakini sisi kama taifa bado tunakumbushana mambo ya mwaka 2008.

Kuukata Mzizi wa fitina ni lazima Lowassa na kama wapo na wengine waliohusika na sakata la Richmond wafikishwe kwenye Mahakama ya mafisadi mara tu Mahakama hiyo itakapoanza kazi. Tunataka Kesi ya kwanza kwenye mahakama hiyo iwe dhidi ya Lowassa na wenzake waliohusika na suala la Richmond.

KESI YA LOWASSA ISIPOKUWA YA KWANZA KWENYE MAHAKAMA YA MAFISADI NITASHANGAA KWELI KWELI!!
 
kwa hii serikali dhaifu ya ccm usitegemee kitu kama hicho. afu sasa cha ajabu utaendelea kuishabikia hiyo serikali wakati haiwezi kuchulia hatua za kisheria watuhumiwa, sasa sijui utakuwa mtu wa aina gani?!
Ndiyo maana sisi wengine ambao tunaiona hii serikali ni Imara tunaihamasisha wampeleke Lowassa kwenye Mahakama ya Ufisadi, kinyume cha hapo wakae kimya!!
 
Ni kweli lazima ashitakiwe kama mshtakiwa wa Kwanza. Hata Mimi pamoja na UKADA wangu naona dhahiri Richmond ilikuwa galasa la kisiasa kwa EL. Mwakyembe alifanya siasa na kamati yake ili kuweza kumwepusha MTU mwingine na kikombe kile. Basi apelekwe Mahakama ya Mafisadi akahukumiwe baada ya kuhukumiwa na Mwakyembe the lawyer..
 
Mimi pia ningependa lowassa na sumaye wspandishwe kizimbani, mmoja ajibu tuhuma za ufisadi,mwingine matumizi mabaya ya madaraka na mauwaji ya watanzania huko visiwani.
 
Ni kweli lazima ashitakiwe kama mshtakiwa wa Kwanza. Hata Mimi pamoja na UKADA wangu naona dhahiri Richmond ilikuwa galasa la kisiasa kwa EL. Mwakyembe alifanya siasa na kamati yake ili kuweza kumwepusha MTU mwingine na kikombe kile. Basi apelekwe Mahakama ya Mafisadi akahukumiwe baada ya kuhukumiwa na Mwakyembe the lawyer..
Kwenye Hotuba yake pale bungeni alikazia sana suala la Natural Justice. Kwa nini Mwakyembe na Kamati yake hakwenda kumhoji Lowassa?
 
Mimi mwenyewe nimeshachoka na kelele Lowasa ni Fisadi bla bla wampeleke sasa mahakamani wakathibitishe ufisadi wa Lowasa ,

Ukistaajabu ya Musa ya Firauni sijui yatakuaje ,wizi wa Escorow ni mara mbili ya Richmond lakini hili limepita tayari kana kwamba hamna kilichotokea

Lowasa alikua waziri mkuu wa Tanzania na sio Tanganyika
 
Lowasa alikua waziri mkuu wa Tanzania na sio Tanganyika
Ili upate Tanzania ni lazima uunganishe na Zanzibar. Zanzibar wana Waziri Kiongozi na Waziri Mkuu unayetaka tumwite wa Tanzania hana madaraka Zanzibar!!
 
Imagine unampeleka Lowassa Mahakamani halafu anapata Mawakili huku Lissu kule Kibatala
 
Kiashiria cha udhaifu kwa binadamu wakati mwingine ni pale anaposhindwa kulifikisha mwisho jambo la muhimu analotakiwa kulikamilisha. Sisi kama taifa tumekuwa tunatangatanga na Jambo lililosababishwa na mtu mmoja tu na sisi kama taifa tumeshindwa kufikia mwisho wake.

Tarehe 7/2/2008 aliyekuwa Waziri wa Mkuu wa Tanganyika wakati ule, Edward Ngoyai Lowassa alijiuzulu wadhifa wake baada ya kutuhumiwa kuingilia mchakato wa Zabuni ya Ufuaji Umeme iliyosababisha kuletwa kwa Kampuni ya Ufuaji Umeme ya Richmond nchini. Tangu kujiuzulu kwa Lowassa mpaka sasa imeshapita miaka zaidi ya 8 na miezi kadhaa, lakini bado suala la sakata la Richmond halijaisha

Mitambo iliyoletwa na Kampuni ya Richmond ambayo bado ipo Pale Pale ilipofungwa na Kampuni ya Richmond, imeshabadilishwa umiliki wake mara mbili. Imetoka kwa Richmond ikanunuliwa na Dowans na sasa inamilikiwa na Kampuni ya Symbion ya Marekani. Lakini sisi kama taifa tumeachwa pale pale tulipokuwa Mwaka 2008.

Kwa kuwa kuna Mahakama ya Mafisadi inaundwa na sisi kama taifa tunayumbishwa na suala la mtu mmoja tu, ambaye si kiongozi wa serikali kwa sasa, nashauri Kesi ya Kwanza kwenye Mahakama ya Mafisadi iwe ni hii ya "Ufisadi" wa Edward Ngoyai Lowassa kuhusu Ufisadi wa zabuni ya ufuaji umeme iliyosababisha Sakata la richmond.

Ni lazima Lowassa ashitakiwe ili kama yeye anao ushahidi tofauti na ule ambao wapinzani wake wanao aje nao mahakamani ili upimwe kwenye mizani ya kisheria tujue nani mkweli kati yake yeye na wapinzani wake.

Haiwezekani mitambo ile iliyoletwa na Kampuni (Feki?) ya Richmond bado ipo nchini mwetu, inafua umeme, Tannesco wanalipa Capacity charges tanesco wanauziwa umeme kutokana na mitambo ile ile iliyokuwa ya Richmond, mkataba ule ule wa kati ya Richmond na Tannesco ndiyo umekuwa ukihuhishwa na Dowans na sasa Symbion, lakini sisi kama taifa bado tunakumbushana mambo ya mwaka 2008.

Kuukata Mzizi wa fitina ni lazima Lowassa na kama wapo na wengine waliohusika na sakata la Richmond wafikishwe kwenye Mahakama ya mafisadi mara tu Mahakama hiyo itakapoanza kazi. Tunataka Kesi ya kwanza kwenye mahakama hiyo iwe dhidi ya Lowassa na wenzake waliohusika na suala la Richmond.

KESI YA LOWASSA ISIPOKUWA YA KWANZA KWENYE MAHAKAMA YA MAFISADI NITASHANGAA KWELI KWELI!!
Your lyt Lowassa lazima akamatwe
 
Ili upate Tanzania ni lazima uunganishe na Zanzibar. Zanzibar wana Waziri Kiongozi na Waziri Mkuu unayetaka tumwite wa Tanzania hana madaraka Zanzibar!!
Kwa hiyo Magufuli ni Raisi wa Tanganyika sio ?? Kwa sababu Zanzibar wana rais wao ?
 
MANENO YA MWAKYEMBE ALIPO HOJIWA KUHUSU SAKATA LA RICHMOND
July 21 2016 Waziri wa katiba na sheria, Dk. Harrison Mwakyembe alikuwa akihojiwa katika kipindi cha Clouds 360 cha clouds TV na kujibu maswali mbalimbali yanayohusu katiba na sheria na hili sakata la Richmond likagusiwa.

Mtangazaji wa clouds TV, Hudson Kamoga alimuuliza Waziri mwakyembe kuhusiana na sakata la Richmond wakati akiwa mwenyekiti wa kamati iliyokuwa inachunguza sakata hilo ambapo walikuja na ripoti ambayo ilipelekea aliyekuwa Waziri mkuu kwa wakati huo, Edward Lowassa kujiuzulu. Hudson ametaka kujua kama kuna mambo ambayo watanzania hawakuyajua kuhusu sakata la Richmond

Waziri Mwakyembe amesema ….>>>‘kesi ya Richmond tuliifanya kwa roho safi na kwa kupiga magoti kwa Mungu na tuliifanya haki kwa kila mtu tulichoamua hata tuamue kesho asubuhi nirudie tena hata koma haitabadilika itakuwa vilevile na mimi nitafurahi sana’

>>>’chini ya kanuni tunaruhusiwa kuifufua tena Richmond ili ichunguzwe upya na ninaaapa wanaweza wote wakahama wakaniacha peke yangu na uhakika mimi mwenyewe nilichonacho nitajenga hoja sidhani kama kuna mtu hata mmoja atasalimika kwenda jela‘
 
Back
Top Bottom