Prof Koboko
JF-Expert Member
- Aug 15, 2020
- 350
- 2,549
Kati ya chaguzi ngumu za Ubunge CCM ni huu wa jimbo la Singida Kaskazini ambapo ndugu Lazaro Nyalandu kada wa zamani wa CCM na Waziri wa Maliasili na Utalii wa awamu ya 4 kupitia CHADEMA dhidi ya ndugu Ramadhani Ighondu kupitia CCM.
Hali ni ngumu sana kutokana na Lazaro Nyalandu kukubalika sana na jamii ya eneo hilo tangu akiwa mbunge mpaka sasa ambapo anatajwa kumiliki wanachama wote wa CCM ingawa yeye yupo CHADEMA.
Upande wa CCM ndugu Ramadhani Ighondu hautabiriki kwa maana siyo mtu anayefahamika sana na jamii ya watu wa eneo hilo ingawa inasemekana kuwa ni mtu mmoja wa mipango sana.
Ndugu Ighondu kutokana na ugeni wake katika siasa ametabiriwa kushindwa vibaya sana dhidi ya Nyalandu ambaye anapewa nafasi kubwa ya kushinda jimbo hilo.
Huyu ndugu Ighondu alikuwa mshindi wa pili kura za maoni chini ya Haidar Gulamali ambaye jina lake limeenguliwa.
Hali ni ngumu sana kutokana na Lazaro Nyalandu kukubalika sana na jamii ya eneo hilo tangu akiwa mbunge mpaka sasa ambapo anatajwa kumiliki wanachama wote wa CCM ingawa yeye yupo CHADEMA.
Upande wa CCM ndugu Ramadhani Ighondu hautabiriki kwa maana siyo mtu anayefahamika sana na jamii ya watu wa eneo hilo ingawa inasemekana kuwa ni mtu mmoja wa mipango sana.
Ndugu Ighondu kutokana na ugeni wake katika siasa ametabiriwa kushindwa vibaya sana dhidi ya Nyalandu ambaye anapewa nafasi kubwa ya kushinda jimbo hilo.
Huyu ndugu Ighondu alikuwa mshindi wa pili kura za maoni chini ya Haidar Gulamali ambaye jina lake limeenguliwa.