Lazaro Nyalandu: Tatizo kubwa la CHADEMA ni Uongozi wa juu, CCM imejaliwa mfumo

Yesu Kristo alisema huwezi kumpa mbwa chakula cha watoto, chadema haiwezi kuwapa uenyekiti makanjanja wa ccm ni kuua chaama
Watu wamepewa hadi nafasi za kugombea urais nini nafasi ya uenyekiti bhana?

Chadema ni kama jalala kila uchafu toka ccm unatupwa huko kisha unaokotwa tena kuja kufanyiwa recycle
 
Alimgalagaza Lissu watu wakasema huyu anaweza kuwa kama Lowasa tusimpe... Je Walioyasema Hayo Na Yeye Aliyemgalagaza Lissu Nani Alikua Sahihi Au Nani Tumuamini!!?
 
Mfumo wa fomu moja bila copy, ukitaka kugombea unafukuzwa huo ndiyo mfumo?
Nyalandu hana hata chembe ya akili. Hivi mfumo wa fomu moja tu nao ni mfumo?

Haya atwambie leo wagombea wa uenyekiti wa CCM Taifa juzi walikuwa wangapi? Kwa nini?
 
Nyalandu hana hata chembe ya akili. Hivi mfumo wa fomu moja tu nao ni mfumo?

Haya atwambie leo wagombea wa uenyekiti wa CCM Taifa juzi walikuwa wangapi? Kwa nini?
Chadema wagombea walikuwa wangapi wa nafasi ya urais shidi ya dictator mmoja ccm
 
Akiwa 360 Clouds ameliongea hili leo na yuko live mpaka sasa, anasema tatizo lipo kwenye uongozi. Amesema wanachama wa chini kabisa hawana tatizo kabisa, matumaini yao yanaharibiwa na uongozi wa juu.

Angalizo: Mbowe uongozi wako umeshindwa vibaya sana, achia ngazi

=======

“Nilipoenda nchi ya ugenini (CHADEMA) wimbo ulikuwa haumbiki kwa namna ambavyo nilikuwa naangalia matukio, ilipotokea Mheshimiwa Rais anaumwa kuna baadhi ya viongozi walijitolea wakasema huyu hafai aondoke tufurahi, ilikuwa inanikwaza kupita kiasi”

“Niliposafiri kwenda Chato kuzika mashambulizi ambayo yalikuwa yananipata, hayakutoka kwa wana-CCM, hayakutoka kwa wana-CHADEMA wa kawaida, yalitoka kwa baadhi wenye msimamo mkali, unamshambuliaje mtu alieenda kuzika kiongozi wake wa nchi?"

“Wakati wa matatizo ya Lissu mimi binafsi sikujali kwamba ni CHADEMA, nilimuona ni Mtanzania ni kiongozi mwenzangu kule Singida, nakumbuka hata Mhe Rais alienda pia kumuona. Lakini wanachama wa CCM kuanzia Rais hadi viongozi hakuna aliepiga simu au kututukana”

“Kuna mitihani ilitokea kwenye uchaguzi, kulikuwa na chaguzi za aina mbili, moja ilikuwa kupigiwa kura kwenye kamati, tunaenda kwenye Baraza Kuu. Kwenye Kamati Kuu Nyalandu alipata 100%, nilimgaragaza kweli kweli, kilichotokea viongozi wakasema Nyalandu asije akawa kama Lowassa”

“Uchaguzi wa mgombea ubunge Singida Kaskazini, wajumbe wamefika usiku ule kuanzia saa kumi na mbili watu wananipigia simu wananiambia mbona mgombea Urais wako hakutaki anasema kidogo umkoseshe kugombea Urais kule Dar es Salaam”

“Wana-CHADEMA watu wa kawaida wengi ni watu wazuri, ni watu ambao wanatamani nchi bora, ambacho wanawazidi wana-CCM wewe itisha mkutano watakuja kwa mguu, watatoka walikotoka, watajitolea katika hali ambayo hutoamini”

“Siasa sio matusi, siasa sio kukoseana heshima, sio kutukana kiongozi wa nchi, siasa sio kuwatukana wale unaotofautiana nao, ni kusema hoja zako mbadala”

“Chama Cha Mapinduzi kimejaliwa mfumo, kilivyotengeneza itifaki ya chama, namna ambavyo walitengeneza mfumo wa kutoa dukuduku zako, mfumo wa kuchaguana. Kina strength ya mfumo, naamini imani ya watu tukipeleka kwa public, mwananchi wa kawaida anatoa kura” -
Aelewe pia kwamba CCM viongozi wa juu wako safi lakini kule mikoani na wilayani, kuna watu wanakuponda kwa mawe kwa sababu tu wako CCM.
 
Majambazi yaliyofilisi mali za Watanzania yanaanza kurudi mmoja baada ya mwingine baada ya jiwe kufariki. Serikali ya Msoga mpeni cheo mwenzenu huyo karudi nyumbani kuendeleza uovu mlioufanya wa wizi wa mali za Watanzania
 
"..Nyalandu alipata 100 wajumbe walikuwa 30 nilipata kura zote Tundu Lissu alipata kura 24 nilimgalagaza kweli kweli" . Ebu nieleweshe hii hesabu.
Mpuuzi tu huyo. Kwanza Kamati kuu hachagui wagombea, inapendekeza majina... Na wote tunajua CDM walikua na majina 3....Bora angesema kuwa alidhulumiwa kura kwenye baraza kuu.

Hivi hao waandishi wa Habari hawajui kuuliza maswali au ndiyo upeo wao ulipoishia...!?
 
Nchi hii Dictator number 1 ni Freeman Aikaeli Mbowe huyu siku Mungu akimuita utazuka ugomvi mkubwa sana wa kugombea madaraka Chadema kati ya familia na ukoo wa Mbowe na wanaharakati uchwala kina Lissu na wenzake.
Na huko kwingine kuna nafasi haziombwi! Siku zikiombwa, tafakari kitakachotokea
 
emoji23.png
emoji23.png
emoji23.png
emoji23.png
kwa msaada wa BASATA na wasanii wake
emoji23.png
emoji23.png
emoji23.png
emoji23.png
emoji23.png
1620053711816.png


1620053467980.png



eti wanasema kwa msaada wa nani vile
 
Nchi hii Dictator number 1 ni Freeman Aikaeli Mbowe huyu siku Mungu akimuita utazuka ugomvi mkubwa sana wa kugombea madaraka Chadema kati ya familia na ukoo wa Mbowe na wanaharakati uchwala kina Lissu na wenzake.
Ni bora huyo dictator kuliko hao vinjaa njaa hebu pata picha Nyalandu leo hii angekuwa Mwenyeketi wa chama si tungekua tushauzwa mpaka wanachama wenyewe kama walivyouzwa TLP na NCCR

CCM inajaribu kubomoa CDM kwa sababu tayari wanaona ni chama ambacho kimeshakomaa mikiki yote na hila za kila aina choni ya MBOWE hivyo wanawasiwasi ukomavu huo soon utawang'oa madarakani
 
Kuna vitu unajiuliza sana kuhusu Watanzania

Nayalandu kama raia ana haki ya kushiriki siasa popote pale alipo bila kuulizwa lolote au chochote
Nyalandu alipohama CCM ilikuwa kwa matakwa yake binafsi

Kinachokera ni kwamba baada ya kurudi CCM sasa anakwenda kueleza katika vyombo vya habari mambo yasisyohusiana na haki yake kama Raia ya kushirikia siasa.

Nyalandu alikuwa na haki ya kueleza hayo akiwa katika chama halafu aondoke. Hili la kueleza baada ya kupokewa ambalo tunajua lina ahadi ni njia ya kujitangaza ili mkono uende kinywani.

Kukaa kimya kunamjengea mtu heshima, haya ya Nyalandu ni kujivua nguo hadharani
Ipo siku tutasikia pia akitueleza ya chumbani sidhani kama anaelewa haki, wajibu na stara.

This is too low Nyalandu, hata kaheshima ulikokuwa nako sidhani kama kapo tena.
Ukimuona alivyo nadhifu hutaamini ..

JokaKuu Pascal Mayalla
 
Back
Top Bottom