Lawyers,Hivi Mfanyakazi Akiwa Kwenye Probation Period Anaweza Kufukuzwa Kazi Bila Kufuata Utaratibu?

SJUMAA26

JF-Expert Member
Jan 25, 2012
607
167
WanaJF na hasa Wanasheria,

Ningependa kuuliza, hivi Mfanyakazi akiwa ndani ya Probation Period anaweza kufukuzwa kazi bila ya kufuata utaratibu ulioainishwa ktk Sheria ya Kazi ya Mwaka 2004 na Kanuni zake?

Manake nina ndugu yangu alikuwa akifanya kazi ofisi moja nyeti ya serikali. Jamaa alikuwa akituhumiwa na Kosa la Kughushi/Wizi na kesi iko mahakamani tangu 2009, haijaanza hata kusikilizwa kwa madai kuwa upelelezi bado unaendelea. Alipopata kazi kwenye hiyo taasisi, alimueleza Mkuu wa Kaya kuhusiana na kesi. Cha ajabu Mkuu huyo akamwambia ajitahidi kesi iwe imeisha ndani ya miezi 2 na baada ya hapo Alimwandikia barua ya Kumwachisha Kazi kwa madai kuwa ana tuhuma mahakamani na kesi ameshindwa kuimaliza ndani ya muda aliopewa!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom