TANZIA Lawrance Mafuru, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango afariki dunia

Mtoa Taarifa

JF-Expert Member
Sep 21, 2024
211
662
Screenshot_2024-11-09-11-43-38-112_com.instagram.android-edit.jpg

Lawrence Nyasebwa Mafuru, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango amefariki Dunia leo Novemba 9, 2024 katika hospitali ya Apollo nchini India.

Rais Samia Suluhu Hassan ameandika katika Mitandao yake ya Kijamii kuhusu Kifo cha Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango,
Screenshot_2024-11-09-12-33-55-661_com.instagram.android-edit.jpg

"Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Bw. Lawrence Nyasebwa Mafuru, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango kilichotokea leo tarehe 09 Novemba, 2024 katika hospitali ya Apollo nchini India.

Ninatoa pole kwa familia, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Mheshimiwa Prof. Kitila Alexander Mkumbo, watumishi wa Tume ya Mipango, ndugu jamaa na marafiki kufuatia msiba huu.

Bw. Mafuru atakumbukwa kwa utumishi wake uliotukuka, bidii na ubunifu alipotumikia nafasi mbalimbali ndani ya Serikali.

Mwenyezi Mungu aijalie familia yake subra na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu na ailaze roho yake mahali pema."


Wasifu wa Mafuru

Lawrence Mafuru ni mtaalamu mashuhuri wa masuala ya fedha mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika benki, uwekezaji, na sera za serikali. Ni Certified Chartered Banker kutoka Taasisi ya Wataalamu wa Benki ya London na pia ni Certified Financial Markets Dealer aliyeidhinishwa na ACI Financial Markets.

Alianza safari yake mwaka 1998 katika Benki ya Standard Chartered, akijikita katika Ufadhili wa Biashara za Kimataifa. Kwa kipindi cha zaidi ya miongo miwili iliyofuata, alishika nyadhifa mbalimbali za uongozi katika sekta ya fedha nchini Tanzania, ikiwemo kuwa Mkuu wa Hazina katika Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, na Mwenyekiti wa Chama cha Mabenki Tanzania (TBA).

Uzoefu wake unaenda zaidi ya benki za biashara, kwani pia aliwahi kuhudumu kama Msajili wa Hazina katika Wizara ya Fedha. Kama mamlaka inayotambulika katika masuala ya benki na fedha, Bw. Mafuru huombwa mara kwa mara kuwa mzungumzaji kwenye mijadala ya sekta hiyo. Ana shauku ya kutumia utaalamu wake ili kuleta manufaa kwa wateja na wadau wake.

Kabla ya nafasi yake ya sasa, Bw. Mafuru alichangia pakubwa katika kuunda sera za uchumi za Tanzania. Alihudumu katika Wizara ya Fedha kama Kamishna wa Idara ya Uchambuzi wa Sera na baadaye kama Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Sera za Usimamizi wa Uchumi.

Hadi kifo kinamkuta, Bw. Lawrence Nyasebwa Mafuru alikuwa akihudumu kama Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango.
 
View attachment 3147717
Rais Samia Suluhu Hassan ameandika katika Mitandao yake ya Kijamii kuhusu Kifo cha Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango,

Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Bw. Lawrence Nyasebwa Mafuru, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango kilichotokea leo tarehe 09 Novemba, 2024 katika hospitali ya Apollo nchini India.

Ninatoa pole kwa familia, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Mheshimiwa Prof. Kitila Alexander Mkumbo, watumishi wa Tume ya Mipango, ndugu jamaa na marafiki kufuatia msiba huu.

Bw. Mafuru atakumbukwa kwa utumishi wake uliotukuka, bidii na ubunifu alipotumikia nafasi mbalimbali ndani ya Serikali.

Mwenyezi Mungu aijalie familia yake subra na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu na ailaze roho yake mahali
pema.
Inna li Llahi wa inna Ilayhi rajiun.
 
View attachment 3147717
Rais Samia Suluhu Hassan ameandika katika Mitandao yake ya Kijamii kuhusu Kifo cha Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango,

Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Bw. Lawrence Nyasebwa Mafuru, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango kilichotokea leo tarehe 09 Novemba, 2024 katika hospitali ya Apollo nchini India.

Ninatoa pole kwa familia, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Mheshimiwa Prof. Kitila Alexander Mkumbo, watumishi wa Tume ya Mipango, ndugu jamaa na marafiki kufuatia msiba huu.

Bw. Mafuru atakumbukwa kwa utumishi wake uliotukuka, bidii na ubunifu alipotumikia nafasi mbalimbali ndani ya Serikali.

Mwenyezi Mungu aijalie familia yake subra na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu na ailaze roho yake mahali
pema.
ipango ipi hawa huwa wanapanga? responsibility yake ni ipi? RIP
 
View attachment 3147717
Rais Samia Suluhu Hassan ameandika katika Mitandao yake ya Kijamii kuhusu Kifo cha Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango,

Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Bw. Lawrence Nyasebwa Mafuru, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango kilichotokea leo tarehe 09 Novemba, 2024 katika hospitali ya Apollo nchini India.

Ninatoa pole kwa familia, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Mheshimiwa Prof. Kitila Alexander Mkumbo, watumishi wa Tume ya Mipango, ndugu jamaa na marafiki kufuatia msiba huu.

Bw. Mafuru atakumbukwa kwa utumishi wake uliotukuka, bidii na ubunifu alipotumikia nafasi mbalimbali ndani ya Serikali.

Mwenyezi Mungu aijalie familia yake subra na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu na ailaze roho yake mahali
pema.
R.I.P Lau dah!
 
View attachment 3147717
Rais Samia Suluhu Hassan ameandika katika Mitandao yake ya Kijamii kuhusu Kifo cha Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango,

"Nimepokea kwa masikitiko taarifa ya kifo cha Bw. Lawrence Nyasebwa Mafuru, Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango kilichotokea leo tarehe 09 Novemba, 2024 katika hospitali ya Apollo nchini India.

Ninatoa pole kwa familia, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais (Mipango na Uwekezaji) Mheshimiwa Prof. Kitila Alexander Mkumbo, watumishi wa Tume ya Mipango, ndugu jamaa na marafiki kufuatia msiba huu.

Bw. Mafuru atakumbukwa kwa utumishi wake uliotukuka, bidii na ubunifu alipotumikia nafasi mbalimbali ndani ya Serikali.

Mwenyezi Mungu aijalie familia yake subra na uvumilivu katika kipindi hiki kigumu na ailaze roho yake mahali pema."



Wasifu wa Mafuru

Lawrence Mafuru ni mtaalamu mashuhuri wa masuala ya fedha mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka 20 katika benki, uwekezaji, na sera za serikali. Ni Certified Chartered Banker kutoka Taasisi ya Wataalamu wa Benki ya London na pia ni Certified Financial Markets Dealer aliyeidhinishwa na ACI Financial Markets.

Alianza safari yake mwaka 1998 katika Benki ya Standard Chartered, akijikita katika Ufadhili wa Biashara za Kimataifa. Kwa kipindi cha zaidi ya miongo miwili iliyofuata, alishika nyadhifa mbalimbali za uongozi katika sekta ya fedha nchini Tanzania, ikiwemo kuwa Mkuu wa Hazina katika Benki ya Taifa ya Biashara (NBC), Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, na Mwenyekiti wa Chama cha Mabenki Tanzania (TBA).

Uzoefu wake unaenda zaidi ya benki za biashara, kwani pia aliwahi kuhudumu kama Msajili wa Hazina katika Wizara ya Fedha. Kama mamlaka inayotambulika katika masuala ya benki na fedha, Bw.

Mafuru huombwa mara kwa mara kuwa mzungumzaji kwenye mijadala ya sekta hiyo. Ana shauku ya kutumia utaalamu wake ili kuleta manufaa kwa wateja na wadau wake.

Kabla ya nafasi yake ya sasa, Bw. Mafuru alichangia pakubwa katika kuunda sera za uchumi za Tanzania. Alihudumu katika Wizara ya Fedha kama Kamishna wa Idara ya Uchambuzi wa Sera na baadaye kama Naibu Katibu Mkuu anayeshughulikia Sera za Usimamizi wa Uchumi.

Hadi kifo kinamkuta, Bw. Lawrence Nyasebwa Mafuru alikuwa akihudumu kama Katibu Mtendaji wa Tume ya Mipango.
Ndiyo maana sipendi mamlaka, bora kuendelea kuwa mfanya biashara jamani. Bora angebaki na firm yake ya consultancy
 
Back
Top Bottom