Law school of Tanzania Mwaka huu ya tia fora

chumvichumvi

JF-Expert Member
May 6, 2010
1,206
304
Law school ya Tanzania ya tia fora mwaka huu baada ya kuchagua wanafunzi wengi zaidi kuliko miaka iliyopita kama ilivyokuwa ada huko miaka ya nyuma. Ni leo jioni majina ya wanafunzia waliochaguliwa na chuo hicho yametolewa katika mfululizo wa batch 3, ya kwanza ikiwa inaingia mwezi april ambayo hiyo ni batch ya kumi na moja(11)na nyingine ikiwa inaingia mwezi wa 6 batch ya kumi na mbili(12) na kumi na tatu(13) kwa ufafanuzi zaidi tembelea website ya chuo hicho ambayo ni www.lst.ac.tz
 
Nendeni mkasome taifa bado lina uhitaji wa mawakili.

from my heart bado cjaona umuhimu wa wanasheria nchi hii. Mikataba kibao mibovu inasainiwa na ina vifungu kibao vya kisheria na kila ofisi ina mwanasheria, mswada wa sheria ya katiba umepitishwa kishabiki na mabadiliko mengine ya sheria hufanywa kisiasa na wao wapo. Katiba ya nchi inaendeshwa na mtu anavyotaka mfano suala la uraia wa sioi, uraia wa nchi mbili watu wanao na ni viongozi na katiba haitambui hilo. Watu wanabambikiwa kesi wakiwa mahakamani na wanafungwa. Hayo yote hawayaoni,mpaka sie tuliosoma bachelor of mathematics tupige kelele majukwaani ndo washtuke. Kuna wengine wamesoma na wanategemewa na jamii lakini ukiwasikiliza argument zao kwenye mambo ya kisheria hata mtoto wa first year medicine anamshinda. Wanatetea matumbo yao tu na hawasimamii ukweli mfano werema, tendwa,lubuva, kabudi nk.
 
from my heart bado cjaona umuhimu wa wanasheria nchi hii. Mikataba kibao mibovu inasainiwa na ina vifungu kibao vya kisheria na kila ofisi ina mwanasheria, mswada wa sheria ya katiba umepitishwa kishabiki na mabadiliko mengine ya sheria hufanywa kisiasa na wao wapo. Katiba ya nchi inaendeshwa na mtu anavyotaka mfano suala la uraia wa sioi, uraia wa nchi mbili watu wanao na ni viongozi na katiba haitambui hilo. Watu wanabambikiwa kesi wakiwa mahakamani na wanafungwa. Hayo yote hawayaoni,mpaka sie tuliosoma bachelor of mathematics tupige kelele majukwaani ndo washtuke. Kuna wengine wamesoma na wanategemewa na jamii lakini ukiwasikiliza argument zao kwenye mambo ya kisheria hata mtoto wa first year medicine anamshinda. Wanatetea matumbo yao tu na hawasimamii ukweli mfano werema, tendwa,lubuva, kabudi nk.
Mkuu salam, naomba nitofauti nawe kidogo. Japo ni kweli kuwa taifa lina wanasheria wasio kuwa na dhamira safi na maadili ila bado twahitaji wanasheria. Nina sema hivi kwa sababu, mfano kumbuka suala la uvunjwaji wa haki za binadamu nyamuma ni wanasheria(LHRC na wengineo) waliolivalia njuga hadi likafahamika na kuipeleka serikali mahakamani. Pia kuhusu katiba Chama cha Wanasheria Tanzania Bara (TLS) kwa miaka mingi kimekuwa kikidai mabadiliko ya katiba hii ya sasa. Pia kabla na baada ya muswada wa mabadiliko ya katiba TLS kilitoa waraka kupinga muswada ule 'mbovu', pia walifungua kesi mahakamani kuupinga muswada huo

Kuhusu kupitishwa kwa saheria mbovu mkuu waweza laumu wanasheria lakini nadhani watambua kuwa muswada huwa wapitishwa bungeni na kusainiwa na Rais(hiyo mihimili miwili sio wanasheria) ni wanasiasa mara nyingi hawana elimu ya sheria. Umeshajiuliza ni kwanini sheria mbovu zinapitishwa bungeni? Je ni sababu ya wanasheria? Kwangu mimi sababu kubwa ni wananchi, sisi wananchi ndio tunaowachagua viongozi wabovu na walio walarushwa, wao wanatuletea sheria mbovu. Wadhani tukichagua wabunge safi tutapata sheria mbovu? Kumbuka kuwa jamii isiyofikiria vizuri, jamii inayokumbatia viongozi wabovu na kuchagua walarushwa itatoa viongozi wabovu watao tunga sheria mbovu. Kinyume chake kama jamii yetu ikiwa na maadili itachagua viongozi safi watakao tunga sheria nzuri wanasheria watalazimika kutumia sheria nzuri.

Ninakubali kuwa kuna wanasheria wasio na maadili, ila nao ni zao la jamii isiyo na maadili inayowakumbatia. Je hatuna walimu, wahandisi, madaktari n.k wasio na maadili? Kuhusu matumizi ya sheria katika mikataba, japo ni kweli kuwa wanasheria ndio wanaandaa hiyo mikataba, kumbuka kuwa wanaandaa kwa kufuata dondoo za mwajili wao serikali na kuangalia sheria inasemaje, inasikitisha kuona kuwa mikataba mingi 'mibovu' haijavunja sheria za nchi japo kimaadili si mizuri, lakini kisheria, sheria yeyote ni halali mpaka pale itakapofutwa. Mfano Sheria zetu hazisemi mikataba ya biashara kati ya serikali na mwekezaji iingiwaje na hazitoi uwazi katika hilo.

Wanasheria wanahitajika kuwa wengi maana hii itawafanya wasambae sehemu nyingi na huenda ikashusha hata gharama. Ni ukweli usiopingika kuwa wananchi wengi wanaonewa kwa sababu ya kukosa mawakili, umesema kuhusu watu kubambikiwa kesi, kumbuka ukiwa na mwanasheria ni rahisi kushinda kesi uliyobambikiwa kuliko mtu asiye na wakili.

Kiujumla kwangu mimi japo ni kweli wanasheria (baadhi) hawana uzalendo na maadili, nao ni zao la jamii iliyokosa maadili na iliyokosa uzalendo.
 
from my heart bado cjaona umuhimu wa wanasheria nchi hii. Mikataba kibao mibovu inasainiwa na ina vifungu kibao vya kisheria na kila ofisi ina mwanasheria, mswada wa sheria ya katiba umepitishwa kishabiki na mabadiliko mengine ya sheria hufanywa kisiasa na wao wapo. Katiba ya nchi inaendeshwa na mtu anavyotaka mfano suala la uraia wa sioi, uraia wa nchi mbili watu wanao na ni viongozi na katiba haitambui hilo. Watu wanabambikiwa kesi wakiwa mahakamani na wanafungwa. Hayo yote hawayaoni,mpaka sie tuliosoma bachelor of mathematics tupige kelele majukwaani ndo washtuke. Kuna wengine wamesoma na wanategemewa na jamii lakini ukiwasikiliza argument zao kwenye mambo ya kisheria hata mtoto wa first year medicine anamshinda. Wanatetea matumbo yao tu na hawasimamii ukweli mfano werema, tendwa,lubuva, kabudi nk.
vipi kuhus majengo yanayodondoka kama lile la kisutu na chang'ombe house, hii nchi kila kona mbovu. wabunge wenu mnaowapitisha wanafanya mambo kishabiki, hata wanasheria wakiwaambia muswada huo unatatizo wao wapo kishabiki.
Jua kutofautisha kati proffessionalism na breach of code of conduct.
 
hata kama ni mradi wa m2 hamna means nyingine zaidi ya kwenda kama kweli unataka uadvocate otherwise utaendelea kuteseka mtaani as kila ofisi ukiingia wanakuuliza kuhusu law xul otherwise underpayment itakuhusu
 
unajua kuna swala moja naic tunachanganya au tunashindwa kutofautisha kati ya siasa na sheria nikiwa namaana ya kwamba m2 anaweza akawa mwanasiasa aliyebahatika ku-practice sheria sasa anapokuwa mwana siasa anasahau nini sheria inataka au mwanasheria ni nani na ikatokea akafanya vyote viwili kwa wakati m1 vyote huwa vinamshinda ndio mambo hayo unayoyasema kutokuwepo kwa uadilifu as its well know u cant serve 2 masters @ a time mmoja lazima aende mfano hai ni Tindu Lissu yule jamaa ana-practice uwanasheria bungeni na si siasa ndio maana kwenye miswada ya sheria huwa yuko moto na straight
ni hayo 2
 
sasa swala la magorofa na nyumba kudondoka ni swala la wakandarasi ndugu yangu
 
Tanzania ina wanasheria wengine wamesoma Havard lakini bure. Mikataba kwenye madini ovyo, wameruhusu mpaka wanasiasa wawe kwenye kamati za maadili za mahakama. Tena wengine washawahi kuwa majaji,sasa kama huku hivije kwenye ujaji ilikuwaje
 
ingewezekana kila raia wa TZ angekuwa na mwanasheria wake lakini mawakili ni wachache na uhitaji ni mkubwa wangetoa hata batch 5 ni sawa tu
 
No research no right talk. Kaa chini fanya uchunguzi kwanza ukishaelewa/ukishapata ufahamu wa suala unalotaka kulizungumzia ndiyo ulizungumzie kwa jamii.
 
mkuu nimeshindwa kukugongea like kama mia tano hivi mka
 
Last edited by a moderator:
ni sawa lakini kuiweka dar peke yake inaumiza watanzania wengine especially wale waliomaliza llb kutoka mikoani pia inawabagua watanzania kwani bodi ya mkopo haihusiki huko na wengi hatuna uwezo wa kujisomesha
 
Mkuu salam, naomba nitofauti nawe kidogo. Japo ni kweli kuwa taifa lina wanasheria wasio kuwa na dhamira safi na maadili ila bado twahitaji wanasheria. Nina sema hivi kwa sababu, mfano kumbuka suala la uvunjwaji wa haki za binadamu nyamuma ni wanasheria(LHRC na wengineo) waliolivalia njuga hadi likafahamika na kuipeleka serikali mahakamani. Pia kuhusu katiba Chama cha Wanasheria Tanzania Bara (TLS) kwa miaka mingi kimekuwa kikidai mabadiliko ya katiba hii ya sasa. Pia kabla na baada ya muswada wa mabadiliko ya katiba TLS kilitoa waraka kupinga muswada ule 'mbovu', pia walifungua kesi mahakamani kuupinga muswada huo

Kuhusu kupitishwa kwa saheria mbovu mkuu waweza laumu wanasheria lakini nadhani watambua kuwa muswada huwa wapitishwa bungeni na kusainiwa na Rais(hiyo mihimili miwili sio wanasheria) ni wanasiasa mara nyingi hawana elimu ya sheria. Umeshajiuliza ni kwanini sheria mbovu zinapitishwa bungeni? Je ni sababu ya wanasheria? Kwangu mimi sababu kubwa ni wananchi, sisi wananchi ndio tunaowachagua viongozi wabovu na walio walarushwa, wao wanatuletea sheria mbovu. Wadhani tukichagua wabunge safi tutapata sheria mbovu? Kumbuka kuwa jamii isiyofikiria vizuri, jamii inayokumbatia viongozi wabovu na kuchagua walarushwa itatoa viongozi wabovu watao tunga sheria mbovu. Kinyume chake kama jamii yetu ikiwa na maadili itachagua viongozi safi watakao tunga sheria nzuri wanasheria watalazimika kutumia sheria nzuri.

Ninakubali kuwa kuna wanasheria wasio na maadili, ila nao ni zao la jamii isiyo na maadili inayowakumbatia. Je hatuna walimu, wahandisi, madaktari n.k wasio na maadili? Kuhusu matumizi ya sheria katika mikataba, japo ni kweli kuwa wanasheria ndio wanaandaa hiyo mikataba, kumbuka kuwa wanaandaa kwa kufuata dondoo za mwajili wao serikali na kuangalia sheria inasemaje, inasikitisha kuona kuwa mikataba mingi 'mibovu' haijavunja sheria za nchi japo kimaadili si mizuri, lakini kisheria, sheria yeyote ni halali mpaka pale itakapofutwa. Mfano Sheria zetu hazisemi mikataba ya biashara kati ya serikali na mwekezaji iingiwaje na hazitoi uwazi katika hilo.

Wanasheria wanahitajika kuwa wengi maana hii itawafanya wasambae sehemu nyingi na huenda ikashusha hata gharama. Ni ukweli usiopingika kuwa wananchi wengi wanaonewa kwa sababu ya kukosa mawakili, umesema kuhusu watu kubambikiwa kesi, kumbuka ukiwa na mwanasheria ni rahisi kushinda kesi uliyobambikiwa kuliko mtu asiye na wakili.

Kiujumla kwangu mimi japo ni kweli wanasheria (baadhi) hawana uzalendo na maadili, nao ni zao la jamii iliyokosa maadili na iliyokosa uzalendo.
Kasahau hata madaktari wanakata kichwa badala ya mguu, na engineers wanabomoa gorofa kwa kuanza chini badala ya juu. Hizo ni challenges ambazo ziko katika kila fani. Lakini huwezi sema yaani huoni kabisa umuhimu wa wanasheria. Uhukumiwe kifo halafu mwanasheria akusemee mahakamani ndio utatambua umuhimu wake.
 
Tatizo sio wingi wa watu je watafaulu na kuwa mawakili?ukweli ni kuwa input na output hazishabiani ata kidg..mfano cohort ya 10 waliingia watu zaidi ya 240 waliofaulu first sitting ni 30 tu.Ushauri wangu ni kuwa dnt go there unless una mda vizuri wa kusoma otherwise watakula kichwa cjawai ona shule ngumu km ile
 
Back
Top Bottom