Law School na kauli za mfa maji haishi kutapa tapa

brazaj

JF-Expert Member
Jul 26, 2016
27,815
35,804
Sakata la wanafunzi LST kufeli limeendelea kujipambanua.

Kadhia ya Law School "Wasomi Nguli" wasikilizwe

Inafahamika kuwa walimu LST nao ni products za vyuo hivi hivi hapa nchini. Kama vyuo vinatoa wanafunzi wasioiva hawa walimu wao walijiivisha namna gani?

Kufeli uwakili kilio Afrika Mashariki

Haya ya kuleta takwimu za kwingine kunako zile nchi zetu pendwa za Trump, ambako kutopenda mafanikio ya wengine nayo ni sehemu ya maisha kunatokea wapi?

Mbona takwimu za kuwahusu mabeberu, China, South Africa au India huko haziletwi?

Shule yenye maana ni Ile ambayo stages zake hadi graduation ni wazi na zinaheshimika.

"Shule haiwezi kuhitimishwa kwa kucheza bahati nasibu."

Hongereni majaji kwa kuunda tume yenu kufuatilia kadhia hii. Wadau zaidi na wachukue hatua ya kizalendo kama hii.

Misahafu inasema: "Tawi la mti lisilozaa hulikata na kulitupa."

LST isiyo na tija ni ya nini?
 
Sakata la wanafunzi LST kufeli limeendelea kujipambanua.

Kadhia ya Law School "Wasomi Nguli" wasikilizwe

Inafahamika kuwa walimu LST nao ni products za vyuo hivi hivi hapa nchini. Kama vyuo vinatoa wanafunzi wasioiva hawa walimu wao walijiivisha namna gani?

Kufeli uwakili kilio Afrika Mashariki

Haya ya kuleta takwimu za kwingine kunako zile nchi zetu pendwa za Trump, ambako kutopenda mafanikio ya wengine nayo ni sehemu ya maisha kunatokea wapi?

Mbona takwimu za kuwahusu mabeberu, China, South Africa au India haziletwi?

Shule yenye maana ni Ile ambayo stages zake hadi graduation ni wazi na zinaheshimika.

"Shule haiwezi kuhitimishwa kwa kucheza bahati nasibu."

Hongereni majaji kwa kuunda tume yenu kufuatilia kadhia hii. Wadau zaidi na wachuke hatua hii.

Misahafu inasema: "Tawi la mti lisilozaa hulikata na kulitupa." LST isiyo na tija ni ya nini?
HUNA HOJA wanafunzi Vilaza ndio maana Wamefeli Wanafunzi hawasomi Muda wote wana Bet Mipira Pombe na Ngono Watasoma saa ngapi? Wanafunzi Lugha ya Kiingereza ni Tatizo kubwa watajielezaje?Kwanini Wao Wafeli na Wenzao Wafaulu?Acheni kuleta SIASA kwenye Fani ya Sheria
 
Kitendo cha waziri kuunda tume yake, na hao majaji nao wakaunda tume yao naamini kitawaamsha wakina Dr. Mwakyembe.

Hizo ripoti mbili zitakapotolewa utakuwa ni wakati mzuri kwa jamii kuchanganya na akili zao ili wazijue mbivu na mbichi, sio kuendelea kuishi kwa mawazo ya kukaririshwa tu wanafunzi hawasomi, hiyo kauli kwangu ni sawa na kuaminishwa walimu wa LST ni malaika, hawana madhaifu.
 
Mdg wangu kama una Supplementary nenda kapambane utoe.
.
Hata uandike nyuzi laki3 hapa Jf kuhusu Lst hazitakusaidia Kitu

Watu kama wewe mmeangaziwa vyema na Prof. Shivji. Kwamba tatizo la law school ni tatizo la taifa (collapse of the educational system) na kwamba wewe ni mmoja wa waathirika yaani positive:

Prof. Shivji na maoni yake kuhusu kadhia ya Law School

Kwamba manguli wenye CV zao wanalitambua na wanachukua hatua ila kinyangarika wewe?
 
HUNA HOJA wanafunzi Vilaza ndio maana Wamefeli Wanafunzi hawasomi Muda wote wana Bet Mipira Pombe na Ngono Watasoma saa ngapi? Wanafunzi Lugha ya Kiingereza ni Tatizo kubwa watajielezaje?Kwanini Wao Wafeli na Wenzao Wafaulu?Acheni kuleta SIASA kwenye Fani ya Sheria

Prof Shivji anasema kama taifa tuna matatizo makubwa kuliko la LST. La LST is just a tip of the iceberg.

Prof. Shivji na maoni yake kuhusu kadhia ya Law School

Elimu imeparaganyika Kila jambo Lukumba Lukumba.

Wewe ulipo umekuwa hakimu una majibu rahisi kwenye maswali magumu yaliyoifanya serikali kuunda tume. Wala hujishangai unsshangaa wengine.

Kadhia ya Law School "Wasomi Nguli" wasikilizwe

Grow up man!
 
HUNA HOJA wanafunzi Vilaza ndio maana Wamefeli Wanafunzi hawasomi Muda wote wana Bet Mipira Pombe na Ngono Watasoma saa ngapi? Wanafunzi Lugha ya Kiingereza ni Tatizo kubwa watajielezaje?Kwanini Wao Wafeli na Wenzao Wafaulu?Acheni kuleta SIASA kwenye Fani ya Sheria
Waliofaulu ni Asilimia ngapi na waliofeli ni asilimia ngapi ndugu?Angalia majority
 
Serikali imeunda KAMATI na siyo TUME elewa hilo kwanza

Tume ni neno la kiswahili likiwa na maana ya kikundi cha watu wachache waliotumwa kufanya jambo la uchunguzi.

Kamati ni neno la kiswahili lenye maana ya kikundi cha watu chenye jukumu fulani lisilokuwa la kiuchunguzi.

Tume ni kamati ya uchunguzi.

Kamati pekee haiwezi kuwa tume ila ni tume kama ni ya uchunguzi. Ndiyo maana hakuna tume za harusi au misiba. Ila kamati za harusi na misiba.

NB: usidogoshe. Serikali imeunda kamati ya uchunguzi ambayo kwa jina moja huitwa TUME.

Ninakazia: Matatizo yetu ya elimu yako pale pale.
 
Wana roho za kimasikini sana

Watu hawa wanastahili Uzi kamili. Prof. Shivji kawagusia.

Kwa ufinyu wa mawazo yao wanadhani Shivji kawalenga LST peke Yao.

Makelele yote ya kujishangaa watanzania dhidi ya wananchi wa nchi zingine mzizi wake Iko kwenye kuparaganyika kwa elimu yetu.

Kutokuwa na capacity ya kuhoji yaani critical thinking ni msiba wa taifa. Hawa uwaonao ndiyo marehemu kabisa.
 
Duniani Law School haijawahi kuwa nyepesi, fuatilia majimbo ya Marekani napo ni vilio, ulaya napo vilio, kote kote haijawahi kuwa nyepesi na tatizo ni mitazamo ya watahiniwa.
 
Kasome mkuu.

Uwakili haupatikani mitandaoni.

Wakati kama nyie Shivji kaamua kuwatolea uvivu ndani ya kadhia hii.

Binadamu bila capacity to critical thinking ni sawa na ling'ombe tu.

Ndiyo maana akiandika mtu kuhusu ushoga mtamwita shoga. Akiandika kuhusu mitume mtamwita nabii. Akiandika kuhusu katiba mpya mtamwita Chadema. Nk, Nk.

Mjihurumie vipi wakati hamjitambui?

Watu kama nyie ni mzigo kwa taifa hili.
 
Mdg wangu kama una Supplementary nenda kapambane utoe.
.
Hata uandike nyuzi laki3 hapa Jf kuhusu Lst hazitakusaidia Kitu

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
Umenena vema. Huyu mleta mada alitumia muda mwingi kubet na kudanga badala ya kusoma. Sasa sehemu yake pekee ya kutokea ili apate cheti pale LST ni kwenye hili sakata. Ndiyo maana kalikomalia hatari.
 
Back
Top Bottom