Latino na harakati za kuzamia ughaibuni mpaka kutoswa baharini

Naamu kwa jina la jamhuri ya muungano wa jamii forum mzigo unaendelea thanos

Latino mwamba ana endelea na story yake...........

Wale wa giriki walitupa iyo biblia ya kujiombea uko majini baada ya kutoswa pia walitupa pesa wote jumla kama dola 100 ivi kila mtu yake lakin namaanisha ukijumlisha ndio inaweza fikia apo pia na maji ya kunywa kwenye kidumu flani,
kwa haraka niliona jamaa wanaona kabisa atuwez pona iyo biblia ni kama kujiombea tupokelewe uko akhera akuna jipya kwetu tena ivi vingne ni gelesha tu atuta toka navyo huo ndio utakua mwisho wetu sisi ni marehemu watarijiwa tu.
Lakini jamaa ni kama walituonea huruma tu awakuamua kutuua moja kwa moja ila walijua sie kutoka wazima ni ishu kwaiyo kama yupo atakae pona basi izo pesa zimsaidie mbeleni wale jamaa huwaga wanawafunga watu vyuma na kamba ukishikwa alafu wanakutosa baharini ivyo vyuma vinakupeleka chini kabisa na ndio mwisho wako.

Basi wakatoa kile kiboya kipo mfumo wa boti na wakatupakia mule ndani kisha wakakifunga kamba mbele na nyuma alafu wakaanza kukiteremsha taratibu awakuturusha hapa tulifika mpaka kwenye maji wao wakaona hapa sasa pana tosha wakakata zile kamba na sie tukabaki majini na lile life boya wao wakatembea mbele.
Lakini pia sie pale tulipokua atukua mbali sana na fukwe za msumbiji isipokua upepo sasa ndio ikawa shida kwetu na lile boya ndio likawa linapelekwa na upepo linafata uelekeo wa upepo unakoenda atukujua wapi tunakwenda kama kwenye maji mengi kina kirefu au wapi iyo ilikua ni twende twende tukisubiri tu kudra za mwenyezi mungu.
P
Ki ukweli hapa ndio tuliona sasa jamaa ndio wameamua kabisa kutuuua akuna jipya palikua na mawimbi na tukaona kabisa hapa tunakwenda kua msosi wa papa chakula ya papa akuna jingine.

pale tulipo atukuona ata mwisho zaidi ya kuona tu wingu limefika chini kisha bahari tulizungukwa na maji tu kiujumla na pale tulipo tulikua ni eneo la maji meusi au sehemu yenye mkondo kina kirefu apo ata meli uwezi weka nanga yani apo unaweza ukatumbukiza mistimu ya umeme ata 40 ndio ikafika chini au isifike ndio mana panakua na weusi yani pana kiza kwaiyo ni kina hasa.

Basi sehemu kama izo kwa watu wenye utalamu na maji ayo ni maneo ambayo papa ndio nyumbani kwao kwaiyo apo papa kukupitia ni dakika sifuri tu hii ilikua hofu yetu sana na atukujua Yale mawimbi yata tupeleka mpaka wapi.
Kuna muda ilifika tukaona kama taa mbele yetu kwa mbali kidogo lakini tulipokua tuna karibia atuzioni zinapotea kabisa jamaa yetu mmoja akasema hawa ni viumbe wa kwenye maji wanafanya shughuli zao mida iyo wanaitwa (vibwengo) ni kama majini tu ndio huonekana na kupotea na ukikutana nao ni wakorofi korofi wanatishia watu tu.
Kama mnakutana macho kwa macho utakiwi kukimbia cha msingi we mkazie macho alafu Fanya kama una mzungukia kwa nyuma awataki kabisa uwaone mgongoni ila inahitaji roho ngumu kufanya ivyo sio laisi imani ina hitajika sana apo lazima atoke atakimbia.

Basi muda umekwenda upepo mkali bardi usiseme ni Kali hasa miili yetu ikaanza kushikwa na chumvi mwili wote yani unakua ka kitoweo ivi ile chumvi ya bahari ni Kali ndugu basi tukasonga mbele tukipeana mioyo kibishi tu ila mbele zoruba ya mawimbi ilizidi ikawa inatuyumbisha mno mwenzetu mmoja hali yake aikua nzur ilishindwa kuhimili vile vishindo kutkana na zile pepo za kusi ivyo hali ilikua mbaya uyu tulimpoteza alifariki ila kabla ya kufa aliacha ujumbe kama ikitokea tutarudi nyumbani sisi basi tumpe taarifa bi mkubwa wake na tumwambie chumbani kwake kuna visjisent alichimbia chini ya kitanda kwaiyo avichukue kisha mshkaji akatulia akiwa ana tabasamu tu lakini si tulimwambia huwez kufa bado mungu yu nasi jamaa aliongea dunia ina mambo mengi mi ndio nafia hapa kweli badae alitulia mazima kabisa tuli ndio ikawa kaenda mwanetu.
Tulijifunga kamba wote wa nne ili kama ikitokea mmoja akabebwa na wimbi iwe laisi kumsaidia sasa baaada ya mshkaji kufariki tukamtoa kwenye kamba tukampigia dua mwenyezi ampoke kisha tukamshusha kwenye maji ilikua ni majozi na akuna namna tusingeweza kukaa na maiti sababu mahiti ina mambo mengi pia ingetupa uzito jamaa alikwenda namna iyo apo tukabaki wa tatu tu.
Tulizidi kusonga zaidi mbele tukisubir nini kitatokea mbeleni apo sijui ni siku ngapi toka jamaa watutose tulikaa alafu pia ata njaa atukuiskia lakini tulikua tunakunywa maji Yale walaiyo tupa baadae ya liisha Yale maji na toka yule mmoja wetu afariki aikupita siku nyingi tukaja pata msaada kuna muda boti ya watalii ilipita mwenzetu mmoja alikua anajiweza kidogo alichukua nguo na kunyoosha juu kwa mkono kama bendera ivi hii ilisaidia wale watu wakatuona na wakaja mpaka tulipo pale na kutupa msaada wakatutoa kwenye lile boya na kisha kutuingiza kwenye boti yao tukiwa hoi dhoofu atujiwezi aiku chukua muda tukazimia wote tukiwa ndani ya boti tulizimia.
Tulikuja shtuka baadae tukiwa pwani ya msumbiji tukipewa huduma ya kwanza lakini pia walituandalia uji baada ya kuamka wote walitupatia uji tulikunywa tukamaliza akatupa mwingne nao tulimaliza tukaomba mwingne wakatunyima sababu pale tuliona bado atushibi kumbe tumbo bado alijawa kwenye hali yake baadae lilipokuja kukaa sawa ndio tukaona tulishiba kupitiliza.
Sasa basi baada ya kukaa sawa jamaa walituhoji ilikuaje tuka wadanganya kwamba tulipata matatizo sisi ni wavuvi tulikumbwa na matatizo ndio ikapelekea mpaka kua hapa atukuwaambia ukweli kwamba tulikua stolo way.
Basi katika wale wa tatu tuliobaki sele yule wa manundu alirudi Pemba mwingne aliitwa mangushi uyu alielekea richadbay Mimi niliamua kubaki pale pwani ya msumbiji sikuona haja ya kuondoka tena na pale ilikua bichi kuna shughuli za uvuvi zinafanyika basi nikaona nijiongeze pale kwenye mishe ya uvuvi.
pale nikajiunga na washkaji flani wa pale msumbiji ambao walikua wenyeji wa kusin uku mtwara uzuri kiswahili walikiweza vizuri na palikua na wa makonde na makabila mengne ya msbiji ivyo ikawa wepesi kwangu kuelewana nao.
Sasa katika ile pwani ya Mozambique republican ambapo ndio nilijiunga na wale washkaji palikua na kisiwa kinaitwa Angoche island kina samaki wengi sana isipokua kisiwa hiki kilikua na maajabu mengi mengi na hata watu ilikua nadra kwenda uko kilihusishwa sana na imani za kishirikina ila inavyosemekana aya mambo kwenye icho kisiwa yalianza kitambo sana kwaiyo sisi ni ubishi tu kwamba izo ni imani tu na ilikua zamani enzi hizo kwaiyo akuna kipya sie tuende kwa kujiamin kwenda kufanya shughuli zetu za uvuvi ndani ya angoche island kinachosemekana kilikua na maajabu iki kisiwa.....................
Tupumzike tutarejea swaumu kali
Sio kwieli ThemiOne
Duh
 
Tumerejea nakazia Latino ndio mwenye mkasa sio Mimi kama umeshawai sikia popote kisa chake basi OK ndio mana nikasema Anasimulia wapo awajakiskia ndio wanasoma hapa nafikiri tumeeelewana then ilo LATINO sio jina lake halisi ilo jina kajipa kutokana na harakati zake za uzamiaji.... OK

Tuendelee......
Basi tulikwenda kule kwenye kile kisiwa jumla tulikua wanne kweli samaki walikua wanapatikana pale kisiwani na tulikua na boti kubwa kidogo na pia ilikua na barafu ya kutosha ya kuhifazia samaki wasiharibike kwa kipindi kirefu pamoja na masunduku makubwa ya kuhifazia samaki ivi vitu ni oda tulipewa na boss flani tunapopata mana ake tupeleke kwake pia tulibeba vitu vingne kama kisu iki kisu chenye boya ata kikitumbukia majini akizami kiberiti cha chuma pia na baruti zile za kupasulia miamba sasa tuliingia kwenye uvuvi haramu yes tukaweka kambi kwenye kile kisiwa tukatafuta eneo zuri tukaweka makazi safi kila tutakapo maliza shughuli zetu basi tutarudi pale kupumzika.

Kuhusu kisiwa inasemekana kwamba miaka ya nyuma palikua na watu wanaishi pale waliweka makazi kifamilia lakini watu wale ghafla tu walitoweka na aikujulikana walikwenda wapi na hata kutoka kwao awakuonekana kama wamevuka kwenda upande gani ila ilisemekana kile kisiwa ni lango kuu la viumbe vya ajabu ambavyo vinatoka angani na kuja eneo lile lakini upande wa pili inasemekana kulikua na jamii nyingne iliishi uko.
Lakini pia pembeni kulikua na kisiwa kingne ambacho kiliibuka tu apakua na historia ya kuwai kuwapo ilisemekana ni nyangumi kwaiyo kile atuku deal nacho sie tulibaki pale tulipofikia, basi shughuli iliyotupeleka pale ikaanza rasmi siku iyo kama kawaida tukaingia mzigoni kwenda kuvua samaki tulipofikia eneo la tukio kwenye kina kirefu tukatoa zile baruti tayari kwa kuzilipua ila kabla ya atujalipua tukaanza pata ishara mbaya ilikuaje mwenzetu mmoja akaingia chini alishuka kwenye maji kwenda kuangalia uwepo wa samaki maeneo yale na jamaa uwezo wake uliluhusu alikua ana pumzi ya kutisha lakini pia kuogelea alikua njema basi jamaa alizamia kwenda kucheki alicheki lakn kupitia maelezo yake baadae kule chini alimuona papa sasa kwa vile ye ni mtaaalamu aling'amua fasta kwamba hapa pana hatari na ukiwa kwenye maji papa kukona ni laisi kupitia viganja vya mikono au miguu vingang'aa kwaiyo laisi kukuona jamaa alivyogundua kwamba yupo kwenye hatari ikabidi aludi juu sasa kwa kupiga makasia akaibuka juu na kuita kwamba tusogeze boti alipoibukia alikua mbali kidogo nasi fasta tukaanza paleleka boti kule kwake nae akawa anakuja kwetu spidi alijiatidi kuyakata maji vilivyo wakati huo yule papa sasa ndio anakuja nae spidi kumfata mshkaji.
Sasa jamaa alipofikia boti na kukamata akitaka kudandia ndani yule papa alikuja ghafla akamralua jamaa kwenye kisigino cha mguu pia akagonga na ile boti nusu ipinduke jamaa akaingia ndani wakati huo tayari keshaumia mguuni damu zinatiririka kwa wingi.

Basi mshkaji tukafunga bandeji mguuni tulimpa huduma ya kwanza na hapo tuakageuza tukarudi atukufanya tena kazi tulirudi kule kisiwani kwetu kuandaa maakuli na vitu vingne.

Kile kisiwa kumbe ilikua ikifika usiku kuna sauti zinasikika toka porini na azieleweki za nni kama sokwe au mbwa ni sauti za ajabu tulikua tunaskia lakini habari za sauti atukuskia kabisa ndio tulizipata pale sasa.
Kwaiyo pale tuliendelea kuwepo kwa siku kazaa tukiendelea kuvua samaki kama kawaida kuna siku tuliingia kuvua usiku wakati tupo katikati, bahari ikabadilika ikachafuka pakawa na zile pepo za kusi za nguvu maji yakabadirika rangi yanakua kama matope ivi alafu mawimbi makubwa makubwa usawa wa nyumba kile chombo chetu kikaanza kuyumba hasa na pia tulikua na taa yetu moja karabai lakini sio ya kujaza upepo ilikua ya utambi ok ambayo tunatumia kuvutia samaki ile taa ilikua na utambi flani ivi sasa ule utambi uliisha ila sisi atukujua icho kitu kabla ya kuja nayo.

Ile zoruba ya bahari na upepo ile taa ikazima tulipojarbu kupandisha utambi kisha upepo ule mkali kwenye kuangaika uku na uku ile taa ikaenda na upepo hapa sasa tukawa kiza atuna hata harama ya kuashiria tupo pale kwajili ya kuonekana kama itatokea meli kubwa zisitugonge ilikua ni mida ya usiku mkubwa iyo kama saa 8 au Tisa ivi ndio tupo kwenye icho kizaa zaa.

Aikuchukua muda sana wakati tupo hapo atuna ili wala lile ghafla meli hii hapa na ipo usawa wetu ila sio sana apo atuja jianda mana imetushtukiza tu akuna la zaidi ile meli ikaja ikatupalaza ilitupita pembeni lakin iliturusha na kile chombo chetu kilipasuka na kila mtu alilushwa upande wake ni vurugu tupu.

Uzuri atukua kati kati kabisa pale tungekufa ilitupitia pembeni apo sasa kila mtu aokoe uhai wake binafsi niliwai dumu la maji lilikua na maji kidogo pia na kamba nikajifunga tumboni liwe boya langu sasa nisije kuzama kama ntaishiwa upepo.

Wale wenzangu sasa sikujua walirushwa wapi mi nikaanza kupiga makasia kwa kuhsi tu maana sina uelekeo wowote nikayakata maji nikayakata maji ikafika muda pumz imekata sina upepo nikakata moto nikazimia kabisa fahamu zikapotea
Sikuelewa kilicho endelea saa kumi na moja alfajiri kwa makadirio nikashtuka nipo ufukweni ina maana muda nazima nilikua karibu na ufukwe kule kisiwani.
Ina maana lile dumu lilinivuta vuta mpaka pale kwenye ufukwe wa bahari nikabaki hapo..
Basi nikajivutavuta mpaka pale kisiwani angoche Niko mwenyewe tu wale wenzangu siku waona kwa haraka nikajua wazi sasa wamekufa. Nikasubiri kukuche mana mvua ilikua inanyesha na lile banda letu liliku Lina vuja ivyo kulivyokucha nikafanya utaratibu wa kurekebsha nikiwa mwenyewe na pale nilipo hapana uhakika wa kupita mtu mana pale kisiwani watu huwa awendi kutokana na imani zile za kishirikina .

Pale palikua na kibiriti pia kisu pamoja na bangi kwajili ya kufukuzia mambo ya majini na vibwengo awapendi ile harufu ya mjani ila sina hakika basi nikaingia msituni mule kwenye kisiwa nikatafuta Magogo ya maana makubwa ili nikiwasha moto usizme mana isije mbele kiberiti kikaisha ikawa tabu na pale na kihitaji muda wote.
Nilianza kuishi pale mwenyewe nikiwa nakula kaa gogo mikaa flani ivi mikubwa ile ambayo ina mikasi mikubwa kama ianakamata kidole inakata nilichonga mti vizuri ndio nikawa nawindia wale walikuapo pale pembezoni mwa ufukwe kwenye vimiti miti nikiwakuta nilikua nawachoma nakuja kuchoma pale kwenye moto na kua msosi palikua na miti ya minazi nilikua naangua Yale madafu kwajili ya maji ya kunywa yalikua yananisaidia pale.
Sasa kile kisiwa ilikua sasa iifika usiku ni hatari mzee zile kelele kama za wanyama ndio zina sikika sasa alafu sometimes unaona kam mtu kavaa ushungi ka mwarabu anakuja Mara ghafla anapotaea Mara unasikia marashi yapo karibu yako kabisa ki ukweli lile eneo ilikua ikikfika usiku basi amani inanitoka akuna usalama zaidi ya hofu tu kwangu ..............
Wakuu
Latino ata endelea si muda

Maphoto yapi tena Mirlz B Matthew
 
Tumerejea nakazia Latino ndio mwenyewe mkasa sio Mimi kama umeshawai sikia popote kisa chake basi OK ndio mana nikasema Anasimulia wapo awajakiskia ndio wanasoma hapa nafikiri tumeeelewana then ilo LATINO sio jina lake halisi ilo jina kajipa kutokana na harakati zake za uzamiaji.... OK

Tuendelee......
Basi tulikwenda kule kwenye kile kisiwa jumla tulikua wanne kweli samaki walikua wanapatikana pale kisiwani na tulikua na boti kubwa kidogo na pia ilikua na barafu ya kutosha ya kuhifazia samaki wasiharibike kwa kipindi kirefu pamoja na masunduku makubwa ya kuhifazia samaki ivi vitu ni oda tulipewa na boss flani tunapopata mana ake tupeleke kwake pia tulibeba vitu vingne kama kisu iki kisu chenye boya ata kikitumbukia majini akizami kiberiti cha chuma pia na baruti zile za kupasulia miamba sasa tuliingia kwenye uvuvi haramu yes tukaweka kambi kwenye kile kisiwa tukatafuta eneo zuri tukaweka makazi safi kila tutakapo maliza shughuli zetu basi tutarudi pale kupumzika.

Kuhusu kisiwa inasemekana kwamba miaka ya nyuma palikua na watu wanaishi pale waliweka makazi kifamilia lakini watu wale ghafla tu walitoweka na aikujulikana walikwenda wapi na hata kutoka kwao awakuonekana kama wamevuka kwenda upande gani ila ilisemekana kile kisiwa ni lango kuu la viumbe vya ajabu ambavyo vinatoka angani na kuja eneo lile lakini upande wa pili inasemekana kulikua na jamii nyingne iliishi uko.
Lakini pia pembeni kulikua na kisiwa kingne ambacho kiliibuka tu apakua na historia ya kuwai kuwapo ilisemekana ni nyangumi kwaiyo kile atuku deal nacho sie tulibaki pale tulipofikia, basi shughuli iliyotupeleka pale ikaanza rasmi siku iyo kama kawaida tukaingia mzigoni kwenda kuvua samaki tulipofikia eneo la tukio kwenye kina kirefu tukatoa zile baruti tayari kwa kuzilipua ila kabla ya atujalipua tukaanza pata ishara mbaya ilikuaje mwenzetu mmoja akaingia chini alishuka kwenye maji kwenda kuangalia uwepo wa samaki maeneo yale na jamaa uwezo wake uliluhusu alikua ana pumzi ya kutisha lakini pia kuogelea alikua njema basi jamaa alizamia kwenda kucheki alicheki lakn kupitia maelezo yake baadae kule chini alimuona papa sasa kwa vile ye ni mtaaalamu aling'amua fasta kwamba hapa pana hatari na ukiwa kwenye maji papa kukona ni laisi kupitia viganja vya mikono au miguu vingang'aa kwaiyo laisi kukuona jamaa alivyogundua kwamba yupo kwenye hatari ikabidi aludi juu sasa kwa kupiga makasia akaibuka juu na kuita kwamba tusogeze boti alipoibukia alikua mbali kidogo nasi fasta tukaanza paleleka boti kule kwake nae akawa anakuja kwetu spidi alijiatidi kuyakata maji vilivyo wakati huo yule papa sasa ndio anakuja nae spidi kumfata mshkaji.
Sasa jamaa alipofikia boti na kukamata akitaka kudandia ndani yule papa alikuja ghafla akamralua jamaa kwenye kisigino cha mguu pia akagonga na ile boti nusu ipinduke jamaa akaingia ndani wakati huo tayari keshaumia mguuni damu zinatiririka kwa wingi.

Basi mshkaji tukafunga bandeji mguuni tulimpa huduma ya kwanza na hapo tuakageuza tukarudi atukufanya tena kazi tulirudi kule kisiwani kwetu kuandaa maakuli na vitu vingne.

Kile kisiwa kumbe ilikua ikifika usiku kuna sauti zinasikika toka porini na azieleweki za nni kama sokwe au mbwa ni sauti za ajabu tulikua tunaskia lakini habari za sauti atukuskia kabisa ndio tulizipata pale sasa.
Kwaiyo pale tuliendelea kuwepo kwa siku kazaa tukiendelea kuvua samaki kama kawaida kuna siku tuliingia kuvua usiku wakati tupo katikati, bahari ikabadilika ikachafuka pakawa na zile pepo za kusi za nguvu maji yakabadirika rangi yanakua kama matope ivi alafu mawimbi makubwa makubwa usawa wa nyumba kile chombo chetu kikaanza kuyumba hasa na pia tulikua na taa yetu moja karabai lakini sio ya kujaza upepo ilikua ya utambi ok ambayo tunatumia kuvutia samaki ile taa ilikua na utambi flani ivi sasa ule utambi uliisha ila sisi atukujua icho kitu kabla ya kuja nayo.

Ile zoruba ya bahari na upepo ile taa ikazima tulipojarbu kupandisha utambi kisha upepo ule mkali kwenye kuangaika uku na uku ile taa ikaenda na upepo hapa sasa tukawa kiza atuna hata harama ya kuashiria tupo pale kwajili ya kuonekana kama itatokea meli kubwa zisitugonge ilikua ni mida ya usiku mkubwa iyo kama saa 8 au Tisa ivi ndio tupo kwenye icho kizaa zaa.

Aikuchukua muda sana wakati tupo hapo atuna ili wala lile ghafla meli hii hapa na ipo usawa wetu ila sio sana apo atuja jianda mana imetushtukiza tu akuna la zaidi ile meli ikaja ikatupalaza ilitupita pembeni lakin iliturusha na kile chombo chetu kilipasuka na kila mtu alilushwa upande wake ni vurugu tupu.

Uzuri atukua kati kati kabisa pale tungekufa ilitupitia pembeni apo sasa kila mtu aokoe uhai wake binafsi niliwai dumu la maji lilikua na maji kidogo pia na kamba nikajifunga tumboni liwe boya langu sasa nisije kuzama kama ntaishiwa upepo.

Wale wenzangu sasa sikujua walirushwa wapi mi nikaanza kupiga makasia kwa kuhsi tu maana sina uelekeo wowote nikayakata maji nikayakata maji ikafika muda pumz imekata sina upepo nikakata moto nikazimia kabisa fahamu zikapotea
Sikuelewa kilicho endelea saa kumi na moja alfajiri kwa makadirio nikashtuka nipo ufukweni ina maana muda nazima nilikua karibu na ufukwe kule kisiwani.
Ina maana lile dumu lilinivuta vuta mpaka pale kwenye ufukwe wa bahari nikabaki hapo..
Basi nikajivutavuta mpaka pale kisiwani angoche Niko mwenyewe tu wale wenzangu siku waona kwa haraka nikajua wazi sasa wamekufa. Nikasubiri kukuche mana mvua ilikua inanyesha na lile banda letu liliku Lina vuja ivyo kulivyokucha nikafanya utaratibu wa kurekebsha nikiwa mwenyewe na pale nilipo hapana uhakika wa kupita mtu mana pale kisiwani watu huwa awendi kutokana na imani zile za kishirikina .

Pale palikua na kibiriti pia kisu pamoja na bangi kwajili ya kufukuzia mambo ya majini na vibwengo awapendi ile harufu ya mjani ila sina hakika basi nikaingia msituni mule kwenye kisiwa nikatafuta Magogo ya maana makubwa ili nikiwasha moto usizme mana isije mbele kiberiti kikaisha ikawa tabu na pale na kihitaji muda wote.
Nilianza kuishi pale mwenyewe nikiwa nakula kaa gogo mikaa flani ivi mikubwa ile ambayo ina mikasi mikubwa kama ianakamata kidole inakata nilichonga mti vizuri ndio nikawa nawindia wale walikuapo pale pembezoni mwa ufukwe kwenye vimiti miti nikiwakuta nilikua nawachoma nakuja kuchoma pale kwenye moto na kua msosi palikua na miti ya minazi nilikua naangua Yale madafu kwajili ya maji ya kunywa yalikua yananisaidia pale.
Sasa kile kisiwa ilikua sasa iifika usiku ni hatari mzee zile kelele kama za wanyama ndio zina sikika sasa alafu sometimes unaona kam mtu kavaa ushungi ka mwarabu anakuja Mara ghafla anapotaea Mara unasikia marashi yapo karibu yako kabisa ki ukweli lile eneo ilikua ikikfika usiku basi amani inanitoka akuna usalama zaidi ya hofu tu kwangu ..............
Wakuu
Latino ata endelea si muda

Maphoto yapi tena Mirlz B Matthew
Aisee inahitaji ujasiri kuyaishi maisha hayo
 
Back
Top Bottom