Laptop computers 10 zaibwa shule ya sekondari Moshi Technical - Mkoa wa Kilimanjaro

peno hasegawa

JF-Expert Member
Feb 24, 2016
12,793
21,367
Kumekuwepo na usiri mkubwa , kwenye sakata la wizi wa laptop computers 10 uliofanyika shule ya Moshi Technical kule kilimanjaro, ambapo shule hii Ina kitengo maalumu cha wanafunzi wenye matatizo ya kutokusikia vizuri. Hii ni mara ya pili kufanyika kwa wizi huo ndani ya mwaka mmoja.

Kimsingi mkuu wa shule hiyo ameshindwa kuisimamia shule hiyo kongwe nchini kutokana na kukosa uzoefu wa kazi hiyo sambamba na kukosa ushirikiano na afisaelimu sekondari wa Moshi mjini. Kutokana na kukidhiri kwa wizi huo, afisaelimu sekondari moshi manispaa na mkuu wa shule hiyo wamegoma kutoa ushirikiano katika utatuzi na upatikanaji wa computer hizo.

Tunashauri taasisi muhimu za uchunguzi zifanye uchunguzi wa kina na mkuu wa shule na afisaelimu sekondari moshi manispaa wapishe uchunguzi. Ili haki iweze kutendeka. Pia ikumbuke kuwa shule hiyo ilifanyiwa ukarabati za zaidi ya Tsh billion moja ambapo hakuna value for money.

Na mhasibu wa shule hiyo, alivyomaliza ukarabati wa shule hiyo ,alihamishiwa shule nyingine kongwe iliyoanza tena kukarabatiwa kwa Tsh 900milion. Kwa mantiki hiyo kuna mlolongo mkubwa wa upigaji wa fedha za umma na wizi wa mali ya umma ndani ya shule hiyo.
 
Yaelekea una bifu moja kwa moja na Mkuu wa Moshi Tech wewe na huenda ni bifu la kimaslahi

Ila kama sivyo na usemayo ni ya kweli Ukaguzi ngazi ya mkoa wafanye kazi yao kwenye ofisi ya uhasibu hapo shuleni
 
Kumekuwepo na usiri mkubwa , kwenye sakata la wizi wa laptop computers 10 uliofanyika shule ya Moshi Technical kule kilimanjaro, ambapo shule hii Ina kitengo maalumu cha wanafunzi wenye matatizo ya kutokusikia vizuri. Hii ni mara ya pili kufanyika kwa wizi huo ndani ya mwaka mmoja.

Kimsingi mkuu wa shule hiyo ameshindwa kuisimamia shule hiyo kongwe nchini kutokana na kukosa uzoefu wa kazi hiyo sambamba na kukosa ushirikiano na afisaelimu sekondari wa Moshi mjini. Kutokana na kukidhiri kwa wizi huo, afisaelimu sekondari moshi manispaa na mkuu wa shule hiyo wamegoma kutoa ushirikiano katika utatuzi na upatikanaji wa computer hizo.

Tunashauri taasisi muhimu za uchunguzi zifanye uchunguzi wa kina na mkuu wa shule na afisaelimu sekondari moshi manispaa wapishe uchunguzi. Ili haki iweze kutendeka. Pia ikumbuke kuwa shule hiyo ilifanyiwa ukarabati za zaidi ya Tsh billion moja ambapo hakuna value for money.

Na mhasibu wa shule hiyo, alivyomaliza ukarabati wa shule hiyo ,alihamishiwa shule nyingine kongwe iliyoanza tena kukarabatiwa kwa Tsh 900milion. Kwa mantiki hiyo kuna mlolongo mkubwa wa upigaji wa fedha za umma na wizi wa mali ya umma ndani ya shule hiyo.
Hii habari inamchimba mtu haikulenga kutujuza laptop zilizoibiwa
 
Dah "shule yetu Ufundi Mungu ibariki bariki wanafunzi nao walimu, tupate amani upendo umoja ushirikiano na udumu daima..tuwe watu watii tuwajibike na kuzibuni mbinu za kazi..."
My former camp ilinifunza maisha hii shule, wapi Mwl Mpande😃
 
Yaelekea una bifu moja kwa moja na Mkuu wa Moshi Tech wewe na huenda ni bifu la kimaslahi

Ila kama sivyo na usemayo ni ya kweli Ukaguzi ngazi ya mkoa wafanye kazi yao kwenye ofisi ya uhasibu hapo shuleni
Nitafaidika vipi na wizi wa computer za watoto walemavu ,mkuu.? Pale Pana mtandao mkubwa wa upigaji wa fedha za umma kuanzia ngazi ya mkoa,wilaya,bodi ya shule na mkuu wa shule hiyo kongwe nchini.
 
Mwalimu nimekufahamu. Wewe ndiye unamsumbua sana mkuu kupeleka vimaneno fb na jf ili kumuharibia. Tukutane kazini
 
"Tatizo wizi wa mali za umma ni majungu"
1.Umesema Mkuu wa Shule Hana Uzoefu Wa Kuendesha Shule KONGWE,
¶ Wewe Ulitaka Apatie Wapi Uzoefu Kama Si Uroho Wako wa Madaraka?

2.Umedai Muhasibu Muhasibu Kasimamia Ukarabati Wa Shule KONGWE Ukarabati wa 1B na Hakuna Value Of Money.Ukasema Kahamishwa Shule Nyingine KONGWE Yenye Ukarabati Kama Huo Kwa 900M.
¶Are You Mkandarasi Kujua Thamani Na Gharama Mbalimbali za Ukarabati Zilizotumika?
¶Je Kuhamishwa Na Kuaminiwa kwa Mhasibu Huyo Kwenda Shule Nyingine Yenye Ukarabati Kama Hip Inakuuma Nini?

3.Umesema Kuna Upigaji Unaowahusisha Wakuu wa Idara Mbalimbali Hapo DC.
¶Unao Ushahidi Pasi na Shaka Kwa Hao Unaotaka Wachunguzwe Utakaowatia Ndugu Zetu Hawa Hatiani Au Ni Hila Zako Tu Mkuu?

4.Umesema Uchunguzi Ambao Umefanyika Kubaini Wizi wa Tarakilishi Hizo Wakuu Wameshindwa Kutoa Ushirikiano.
¶Upo Kitengo cha Upelelezi?
¶Unajadilije Swala Ambalo Mamlaka Husika Haijatoa Tamko,Au Wewe Ni Msemaji Wa Jeshi La Polisi? 😁

Mkuu,Tafuta Hela Acha Majungu
 
1.Umesema Mkuu wa Shule Hana Uzoefu Wa Kuendesha Shule KONGWE,
¶ Wewe Ulitaka Apatie Wapi Uzoefu Kama Si Uroho Wako wa Madaraka?

2.Umedai Muhasibu Muhasibu Kasimamia Ukarabati Wa Shule KONGWE Ukarabati wa 1B na Hakuna Value Of Money.Ukasema Kahamishwa Shule Nyingine KONGWE Yenye Ukarabati Kama Huo Kwa 900M.
¶Are You Mkandarasi Kujua Thamani Na Gharama Mbalimbali za Ukarabati Zilizotumika?
¶Je Kuhamishwa Na Kuaminiwa kwa Mhasibu Huyo Kwenda Shule Nyingine Yenye Ukarabati Kama Hip Inakuuma Nini?

3.Umesema Kuna Upigaji Unaowahusisha Wakuu wa Idara Mbalimbali Hapo DC.
¶Unao Ushahidi Pasi na Shaka Kwa Hao Unaotaka Wachunguzwe Utakaowatia Ndugu Zetu Hawa Hatiani Au Ni Hila Zako Tu Mkuu?

4.Umesema Uchunguzi Ambao Umefanyika Kubaini Wizi wa Tarakilishi Hizo Wakuu Wameshindwa Kutoa Ushirikiano.
¶Upo Kitengo cha Upelelezi?
¶Unajadilije Swala Ambalo Mamlaka Husika Haijatoa Tamko,Au Wewe Ni Msemaji Wa Jeshi La Polisi? 😁

Mkuu,Tafuta Hela Acha Majungu
Haya ndio majibu ya Tume au umetumwa kuhalalisha ufisadi na wizi wa mali za umma?
 
Bure Kabisa
tatizo mtoa mada kaanza na tatizo la wizi wa kompyuta 10 hivyo angejikita zaidi na suala la upungufu wa ulinzi mazingira ya shule na kuarifu vyombo husika kufanya uchunguzi juu ya wizi huo
ila ghafla akabadili gia angani na kuanza kutuhumu uongozi wa shule ndo maana wadau wakaona dalili za majungu na fitina za wazi wazi ni vema mtoa mada akajipanga vema
 
tatizo mtoa mada kaanza na tatizo la wizi wa kompyuta 10 hivyo angejikita zaidi na suala la upungufu wa ulinzi mazingira ya shule na kuarifu vyombo husika kufanya uchunguzi juu ya wizi huo
ila ghafla akabadili gia angani na kuanza kutuhumu uongozi wa shule ndo maana wadau wakaona dalili za majungu na fitina za wazi wazi ni vema mtoa mada akajipanga vema
Exactly........
 
Back
Top Bottom