Langa akikutana na mangwear

Kiwa

JF-Expert Member
Oct 4, 2011
2,102
905
Kwa ninavyohisi kama langa anaona haya yanayotokea kuna mengi sana atakuwa anajiuliza na kama kweli huko alipo ataweza kukutana na Ngwear atamuuliza maswali mengi sana. Kikubwa atataka ajue ni kitu gani Ngwear alifanya ambacho langa hakufanya ambacho kimefanya kifo chake kisipewe uzito kama cha ngwear.

Haya ni baaadhi tu ya mambo yaliyofanyika kwenye msiba wa ngwear:

1. Watu walihairisha shows zao kupisha kifo cha Ngwear ila ni tofauti na Langa ambaye amekufa jana tu na leo watu show kama kawa

2. Blogs zilikuwa zimetawaliwa sana na kifo cha ngwear na ni tofauti na leo ninavyoona kwa langa. habari chache saaana.

3. Radio stations zilikuwa busy sana kureport kila kitu kuhusu kifo cha ngwear na ni tofauti kwa ilivyo kwa Langa. Wote wanaendelea na programs zao as if nothing has happened. Wengine walituma hadi presenter SA

4. Nyimbo nyingi sana zilitungwa kwa ajili ya ngwear na kuwekwa kwenye blogs but hadi now sijaona wala kusikia wimbo wowote wa kuomboleza kuhusu langa.

5. Wasanii wa bongo fleva walikuwa busy sana kwenye twitter ana Facebook kupost kuhusu ngwear ila kwa langa leo ni adimu sana kuona tweets au posts za wasanii wengine.


Kiufupi me naona kama langa hajapewa heshma yake kama inavyostahili japo najua kwamba hakuwa mkubwa sana compare to Ngwear but tunajua kilichomtokea (kuwa drugs addict) ila alikiri na kuacha na kurudi normal.
Wote walikuwa wanatumia madawa ila duh Kifo cha langa kimechukuliwa poa sana.

Ni maoni yangu tu.
 
watu wanaangalia kula kaka, plus controversy ya kifo cha ngea kilfanya apate attention, si unajua wabongo kwa umbea...hiki cha langa kiko clear sana...and ngea alifia sauziiiiiii...... cheki pia kanumba vs sajuki...au sharomilionea na huyu mdada (hata sijui jina) alovuta majuzi...ukitaka umaarufu vuta kicontroversal...
 

Similar Discussions

0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom