Pdidy
JF-Expert Member
- Nov 22, 2007
- 50,720
- 21,778
Kuna wanaume kwa wanawake wengi walio kwenye ndoa wanavyoishi maofisini laiti wenza wao wangekuwa karibu nahisi asilimia nyingi wangekuwa juu ya kitanzi cha ndoa.
Kuna watu maofisini wake kwa waume za watu wanaitana sweetbaby, honey na mbaya zaidi kuna ambao wanashikana shikana kama hawajaolewa ama kuoa na wengine lunch time huamua kujifungia ndani ya ofisi kabisa eti wanapiga story ghafla mazungumzo yanakatika kunaashiria ishara ya ukimya, kama una shida ya dharura utapiga hodi mpaka basi..
Baada ya lunch time unashangaa wanatoka kwa kuagana ati ulikuwa wapi wewe, kilichofanyika mnajua.
Wanandoa embu jiulizeni sasa mnavyojiachia ovyo jamani wakati wewe mke wa mtu ama mume wa mtu unamwita mfagiaji king'ast na mchana mnajifungia ofisini, hizo ofisi kweli ama lah..... Mi nahisi lile saa limoja la lunch linachangia sana kuambukiza UKIMWI kwenye familia. Kumbuka muda huo ni ngumu sana kukumbuka condom ofisini.
Narudia naomba kama umeamua kuoa ama kuolewa jiheshmu, ishi kama uko na mkeo ama mumeo ofisini achana na vijisecretary vinajifanya kukuita bosii bossii waambie bosi mama zao.
Mungu awasaidie kuishi maisha matakatifu na kulinda ndoa zenu hasa kipindi hiki kigumu gonjwa la kunyonyana ndimi limeingia na unakufa kwa kubadilika rangi..
Mungu aturehemu sana, atupe uoga.
Kuna watu maofisini wake kwa waume za watu wanaitana sweetbaby, honey na mbaya zaidi kuna ambao wanashikana shikana kama hawajaolewa ama kuoa na wengine lunch time huamua kujifungia ndani ya ofisi kabisa eti wanapiga story ghafla mazungumzo yanakatika kunaashiria ishara ya ukimya, kama una shida ya dharura utapiga hodi mpaka basi..
Baada ya lunch time unashangaa wanatoka kwa kuagana ati ulikuwa wapi wewe, kilichofanyika mnajua.
Wanandoa embu jiulizeni sasa mnavyojiachia ovyo jamani wakati wewe mke wa mtu ama mume wa mtu unamwita mfagiaji king'ast na mchana mnajifungia ofisini, hizo ofisi kweli ama lah..... Mi nahisi lile saa limoja la lunch linachangia sana kuambukiza UKIMWI kwenye familia. Kumbuka muda huo ni ngumu sana kukumbuka condom ofisini.
Narudia naomba kama umeamua kuoa ama kuolewa jiheshmu, ishi kama uko na mkeo ama mumeo ofisini achana na vijisecretary vinajifanya kukuita bosii bossii waambie bosi mama zao.
Mungu awasaidie kuishi maisha matakatifu na kulinda ndoa zenu hasa kipindi hiki kigumu gonjwa la kunyonyana ndimi limeingia na unakufa kwa kubadilika rangi..
Mungu aturehemu sana, atupe uoga.