sky soldier
JF-Expert Member
- Mar 30, 2020
- 5,408
- 19,032
MUHIMU: PICHA HII SIO YA PAKA WA HAPA KWETU
Hapa kwangu napoishi tuna paka, Sio mimi niliemleta bali ni mke wangu.
Hatuna tatizo la panya kwa hio bado sielewi paka anahitajika wa nini.
Kuna jirani ana fuga ngombe huwa anatuuzia maziwa nyumba chache, Mke wangu alilipia ujazo wa ziada alipomleta huyu paka wake ili anywe nae maziwa, huwa aakunywa kila asubuhi na jioni, huu ni ufujaji wa pesa.
Kila mara 2 kwa wiki lazima mke wangu amletee paka samaki, huwa naumia sana kuna paka anagharamiwa wakati hakuna kitu anachofanya, kuna watu wana njaa mitaani her wao wangepewa.
Muda mwingi huyu paka huwa kasinzia na kunenepa tu, anaweza kulala juu ya friji, kwenye kochi, n.k
Huwa sitaki kabisa awe karibu na mimi ila cha ajabu ni kama analazimisha nimzoee huwa anapenda kujipitisha miguuni badala ya kwenda kwa wanaopendaga kumchezea.
Faida pekee ambayo mke wangu anaisema ni kwamba kamfundisha kujisaidia kwenye ka box kake na huwa anamuogesha kila wiki, sasa hii ni faida gani?