“Laana” ni nini?

Quemu

JF-Expert Member
Jun 27, 2007
984
128
Hivi, tumekuwa tukisikia vitisho vya “kimaneno” mbalimbali katika jamii yetu...

Mojawapo ya vitisho hivyo ni upewaji “laana”.

Inasemekana kuwa “laana” utolewa na mzazi kwa mtoto aliye mtukutu au aliye kaidi mwongozo wa wazazi.

Tetesi ni kwamba “laana” inayorushwa na mtu mwingine, zaidi ya mzazi wako, huwa haikudhuru.

Jamani, hiki kitisho huwa kinafanya kazi kweli? Au ni moja ya mikwara “bogus” ambayo imetapaa kila kona ya utamaduni wetu?

Je “laana” ni nini?
 
Hivi, tumekuwa tukisikia vitisho vya “kimaneno” mbalimbali katika jamii yetu...

Mojawapo ya vitisho hivyo ni upewaji “[
B]laana[/B]”.

Inasemekana kuwa “laana” utolewa na mzazi kwa mtoto aliye mtukutu au aliye kaidi mwongozo wa wazazi.

Tetesi ni kwamba “laana” inayorushwa na mtu mwingine, zaidi ya mzazi wako, huwa haikudhuru.

Jamani, hiki kitisho huwa kinafanya kazi kweli? Au ni moja ya mikwara “bogus” ambayo imetapaa kila kona ya utamaduni wetu?

Je “laana” ni nini?

"Inaitwa LAANA JAMII", jamii inaweza kukulaani yakakupata kweli.
 
Laana ni kumuapiza mtu au jamii .. ili kama anakwenda/kaenda kinyume na jambo fulani au miiko .. ambapo kabainika au hajabainika .. adhurike na abainike ..

Mtu /jamii hutoa kiyapo ili iwe kama hukumu kwa yeyote atakae/anaenda kinyume na taratibu ambazo mwenzake/jamii a/itaona ni kitendo cha kinyama au kupitiliza kosa au ubaya.

Laana inampata mtu kweli ... inaweza hata ikaangamiza familia nzima
Mtu yeyote anaweza kumlaani na kulaaniwa kutegemea na kosa alilolifanya
Hata mke/mume anaweza kumlaani mwenziwe akadhurika ... kadhalika mama huweza kumlaani hata mtoto pia
 
mfano hiviii:
sisi watanzania tumelaaniwa ndio maana unaona tuna kichwa cha mwendawazimu.
 
Laana inakupata ukimtendea mtu yeyote mabaya. Kwa hiyo chunga. Ishi kwa maadili na usiwe tapeli au fisadi kwani utapata laana.
 
"Inaitwa LAANA JAMII", jamii inaweza kukulaani yakakupata kweli.

Bubu,
A)Kwa hiyo jamii mzima inaweza kutoa laana kwa mwanajamii?

B)Au mwanajamii anaweza kutoa laana kwa jamii mzima?


Laana ni kumuapiza mtu au jamii .. ili kama anakwenda/kaenda kinyume na jambo fulani au miiko .. ambapo kabainika au hajabainika .. adhurike na abainike ..

Mtu /jamii hutoa kiyapo ili iwe kama hukumu kwa yeyote atakae/anaenda kinyume na taratibu ambazo mwenzake/jamii a/itaona ni kitendo cha kinyama au kupitiliza kosa au ubaya.

Laana inampata mtu kweli ... inaweza hata ikaangamiza familia nzima
Mtu yeyote anaweza kumlaani na kulaaniwa kutegemea na kosa alilolifanya
Hata mke/mume anaweza kumlaani mwenziwe akadhurika ... kadhalika mama huweza kumlaani hata mtoto pia

Naima,
Umesema laana = kuapiza. Kuapiza as in "Haki ya Mungu", "naahidi sitafanya kinyume na matakwa yako", or what?

mfano hiviii:
sisi watanzania tumelaaniwa ndio maana unaona tuna kichwa cha mwendawazimu.

Haika,
Sasa ni nani ametulaani sisi? Je ni sisi wenyewe tumejilaani?

Speaking of kujilaani, je inawezekana kwa mtu kujilaani mwenyewe?

Laana inakupata ukimtendea mtu yeyote mabaya. Kwa hiyo chunga. Ishi kwa maadili na usiwe tapeli au fisadi kwani utapata laana.

Wajinga,
Kwa hiyo sio lazima mtu au jamii ikulaani...yaani hata mazingira uishiyo au matendo ufanyayo yanaweza kukulaani?
******************************************************

Asanteni kwa ufafanuzi wenu.

Kutokana na ufafanuzi wenu hapo juu, ninalazimika kufikiri kuwa "laana" ni "imani." Kama vile tunaposema fulani "amelogwa", tuna express imani yetu kuwa kuna tendo la "kichawi" limetokea kwa mtu huyo.

Sasa kama "laana" ni imani, basi ni wale tu wanafuata imani hiyo ndio wana hatari ya kudhurika. Au?

I mean, kuna tofauti gani kati ya "imani" ya laana na "imani" ya dini...iwe ya kiislam, kikristo, au kipagani? Zote si ni imani tu....na zinafanya kazi kwa wanao amini. Au?
 
Laana inakupata ukimtendea mtu yeyote mabaya. Kwa hiyo chunga. Ishi kwa maadili na usiwe tapeli au fisadi kwani utapata laana.

...inakupata kutoka wapi, kwa nguvu ya nani, gani, inaitwaje, electromagnetic force or something?
 
Si kweli kwamba laana inatoka kwa mzazi tu. Na pia mtoa laana hupatwa na laana vilevile. Maandiko yanasema USILAANI.


.
 
Si kweli kwamba laana inatoka kwa mzazi tu. Na pia mtoa laana hupatwa na laana vilevile. Maandiko yanasema USILAANI.
.

Kwa hiyo laana inaweza kudunda na kukurudia mwenyewe? lol

Kuhani ameuliza swali kwamba hii "laana" inatoka kwenye nguvu gani? Na nini hasa?

Tunajuwa kuwa kuna wata wanaamini "uchawi" ni sehemu ya sayansi. Lakini kuna wengine waamini "uchawi" unatokana na nguvu ya giza (whatever that means).

Je laana urushwa kwa kutumia nguvu gani?
 
Sikubali kwamba kuna laana kama ya mzazi wako kukufanyia kitendo fulani unapata kichaa, ila naamini katika the karmic and natural laws of cause and effect.

Hivyo basi, kwa mfano wa "laana" ya wazazi (wengine wanaita kukosa radhi), wazazi hawa ni watu ambao kwa kawaida wanapenda sana watoto zao. Na wazazi kwa kawaida huvumilia mengi sana mabaya ambayo watoto wao wanaweza kuwafanyia, hivyo basi, ikifikia kipindi wazazi wameshindwa kuvumilia na kutoa "laana" basi huyu mtoto anayepewa laana anakuwa kashaharibikiwa tayari na matokeo yake anaweza kupatwa na mabaya.

Akipatwa na mabaya watu wanasema ni kwa sababu ya laana ya wazazi, bila kujua kuwa hiyo laana / kukosa radhi kumekuja baada ya wazazi kukata tamaa kwamba kuna redemption yoyote kwa mwana wao.

Kwa hiyo laana ni matokeo, si sababu.
 
laana ni maapizo kutoka kwa MWENYEZI MUNGU,ni mambo uyafanyayo ambayo MWENYEZI MUNGU hayupo radhi nayo na UNAYEMFANYIA hayupo radhi nayo,mfano;MWNYEZI MUNGU amewalaani(hawatapata japo bahati ya kuuona mlango wa pepo) wale wote wanaowasodoma/sodomwa(mchezo wa kinyumenyume),
tumeshazoea kusikia kuwa wazazi ndio wenye kutoa laana,si kweli,mzazi yeye kazi yake ni kumshtakia mwenyezi MUNGU.pia si vizuri kwa mwanadamu kulaani laani au kujiona kama umelaaniwa,kwani kwani NENO LINAUMBA.
 
Sikubali kwamba kuna laana kama ya mzazi wako kukufanyia kitendo fulani unapata kichaa, ila naamini katika the karmic and natural laws of cause and effect.

Hivyo basi, kwa mfano wa "laana" ya wazazi (wengine wanaita kukosa radhi), wazazi hawa ni watu ambao kwa kawaida wanapenda sana watoto zao. Na wazazi kwa kawaida huvumilia mengi sana mabaya ambayo watoto wao wanaweza kuwafanyia, hivyo basi, ikifikia kipindi wazazi wameshindwa kuvumilia na kutoa "laana" basi huyu mtoto anayepewa laana anakuwa kashaharibikiwa tayari na matokeo yake anaweza kupatwa na mabaya.

Akipatwa na mabaya watu wanasema ni kwa sababu ya laana ya wazazi, bila kujua kuwa hiyo laana / kukosa radhi kumekuja baada ya wazazi kukata tamaa kwamba kuna redemption yoyote kwa mwana wao.

Kwa hiyo laana ni matokeo, si sababu.

Pundit
Utawaambiaje wale wanao amini kuwa familia fulani "imelaaniwa" kwa sababu wana mtiririko wa matatizo fulani fulani? Je hali hii usababishwa na sio "laana", bali matokeo ya utukutu?

Je laana ndio huitwa "spell/curse" kwa kizungu?
 
laana ni maapizo kutoka kwa MWENYEZI MUNGU,ni mambo uyafanyayo ambayo MWENYEZI MUNGU hayupo radhi nayo na UNAYEMFANYIA hayupo radhi nayo,mfano;MWNYEZI MUNGU amewalaani(hawatapata japo bahati ya kuuona mlango wa pepo) wale wote wanaowasodoma/sodomwa(mchezo wa kinyumenyume),
tumeshazoea kusikia kuwa wazazi ndio wenye kutoa laana,si kweli,mzazi yeye kazi yake ni kumshtakia mwenyezi MUNGU.pia si vizuri kwa mwanadamu kulaani laani au kujiona kama umelaaniwa,kwani kwani NENO LINAUMBA.

Neno Mungu, limedhihirisha kuwa "laana" ni imani. Na kama imani nyingine yeyote, basi wale tu waaminio ndio hudhurika.
 
Neno Mungu, limedhihirisha kuwa "laana" ni imani. Na kama imani nyingine yeyote, basi wale tu waaminio ndio hudhurika.

kumbuka kuwa hapa duniani wapo wanaoabudu miti,ng'ombe,milima,mito nk,na hawa wote wana makatazo yao,na wakienda kinyume nayo hulaaniwa,hivyo laana ipo kwa mwenye kuamini na asiyeamini
 
Pundit
Utawaambiaje wale wanao amini kuwa familia fulani "imelaaniwa" kwa sababu wana mtiririko wa matatizo fulani fulani? Je hali hii usababishwa na sio "laana", bali matokeo ya utukutu?

Je laana ndio huitwa "spell/curse" kwa kizungu?

Yote ni cause and effect, au inaweza hata kuwa genetics.

Mfano, inawezekana katika familia fulani kuna genes za kuwafanya watu wawe susceptible kwa magonjwa ya akili, au ulevi, watu wengi wakitokea kuwa na ukichaa au ulevi watu watasema "wamelaaniwa" kumbe ni genetics.

Mara nyingine inakuwa ni habits zilizojengeka kwa siku nyingi tu.

Laana ni more of curse kuliko spell, spell inaweza kuwa kitu kam hypnotism zaidi kuliko laana.
 
Laana ni kama mbegu mbaya ipandwayo ardhini, mbegu mbaya yoyote ile huota kwa bidii sana tena bila hata kuiwekea mbolea, lakini panda mbegu nzuri hata ukiiwekea mbolea vipi utavuna mavuno kidogo sana.

Sasa "laana" ni maneno ambayo mtu huambiwa iwe kwa kukatazwa jambo au hata kwa kuonywa au hata kwa kusisitizwa vyovyote neno hilo litakavyotoka basi haling'oki mawazoni mwa huyo mtu sasa basi kwa kuwa maneno hayo hujengeka mawazoni mwake kila kitu atakachokifanya akishindwa kufanikiwa tu atasingizia ni ile "Laana"

Na usiombe maneno hayo yalipokuwa yanatolewa kama kulikuwa na watu ndio kabisa watayasambaza hadi kila mtu atajua umelaaniwa, na kila mtu kama alitaka kufanya biashara na wewe atasitisha na ndipo nawe utakapoanza kuona kuwa ile laana inakuathili.

Kuhusu mtoa "laana" ni mtu yeyote anaweza kutoa "laana" sio lazima mzazi.
 
Pundit
Utawaambiaje wale wanao amini kuwa familia fulani "imelaaniwa" kwa sababu wana mtiririko wa matatizo fulani fulani? Je hali hii usababishwa na sio "laana", bali matokeo ya utukutu?

Je laana ndio huitwa "spell/curse" kwa kizungu?
Hiyo familia itakuwa na mkosi/nuksi na sio laana!
 
"Inaitwa LAANA JAMII", jamii inaweza kukulaani yakakupata kweli.
kwa mtazamo wangu....laana inatolewa na mtu yeyote yule....ila huyo mtu kama anakupenda kwa ukweli bila unafiki,yaani kama mama ako basi laana inakupata,ILA kama anakupenda kiunafki,basi laana inakuwa barakaa kwako
 
Back
Top Bottom