Kyela : Mafuriko Makubwa yaharibu miundo mbinu , Kivuko Maarufu cha Kityeputyepu chasombwa , Daraja la Ipyana hati hati

Erythrocyte

JF-Expert Member
Nov 6, 2012
117,635
218,068
Mvua Kubwa inayonyesha Wilayani Kyela , huko Mkoani Mbeya imesababisha Mafuriko Makubwa ambayo yameleta maafa makubwa sana , Makazi ya watu karibu kila kijiji yamesambaratishwa vibaya huku Mashamba ya Mpunga yakifunikwa na maji kiasi cha kuharibu kabisa mpunga wenyewe , Hali ni mbaya sana .

Kivuko Maarufu na Muhimu sana kinachounganisha vijiji vya Lupembe , Ibungu na Mji wa Kyela kinachojulikana kama KITYEPUTYEPU kimesombwa na mafuriko hayo huku wananchi wasijue la kufanya .

FB_IMG_1651220910513.jpg


Kivuko hicho kinaunganisha Mji wa Kyela na baadhi ya vijiji na kinaanzia kwenye Taasisi ya Mango Tree , hili ni pigo lisilo na mbadala , Daraja la Ipyana nalo limepigwa na miti iliyong'olewa na Mafuriko na kupinda , huku watumiaji wa daraja hilo wakikumbwa na wasiwasi kama waendelee kutumia daraja hilo au la .

Kwa ujumla vijiji vingi vimepigwa na Mafuriko na kiukweli msaada wa haraka unahitajika , ukianzia kijiji changu cha Kajunjumele , Bujesi , ipyana , bujonde , Ndandalo , maeneo yote ya Kyela Mjini yanayotazamana na Hospitali ya Wilaya yote yamezama baada ya mto kiwira kutapika , zipo taarifa kwamba Mamba wameishaingia kwenye makazi ya watu .

Katumbasongwe , Kabanga na Isaki hali ni mbaya sana baada ya Mto Songwe kutapika , huko Mwaya , Tenende na Talatala hali haisemeki baada ya mto Mbaka nao kutapikia makazi ya watu na kusababisha Mafuriko ya Kutisha , kiasi cha kufunika barabara ya Nkuyu - Matema .

Bado hatujajua Juhudi zinazofanya na Serikali ya Wilaya hiyo ili kusaidia wananchi , Japo Gari la Mkuu wa Wilaya linaonekana kuzunguka huku na huko .

Mungu ibariki Kyela .
 
Huko Ni Malawi bhns poleni wanna Malawi hyo mvua Jana niliona utabiri wake kupitia aljazeera news kuwa kutakuwa na mvua kubwa Kati ya Zambia hvyo naona hyo mvua imekuja kudondokea kwenu uko ipinda
Kyela ni Tanzania
 
Mvua Kubwa inayonyesha Wilayani Kyela , huko Mkoani Mbeya imesababisha Mafuriko Makubwa ambayo yameleta maafa makubwa sana , Makazi ya watu karibu kila kijiji yamesambaratishwa vibaya huku Mashamba ya Mpunga yakifunikwa na maji kiasi cha kuharibu kabisa mpunga wenyewe , Hali ni mbaya sana .

Kivuko Maarufu na Muhimu sana kinachounganisha vijiji vya Lupembe , Ibungu na Mji wa Kyela kinachojulikana kama KITYEPUTYEPU kimesombwa na mafuriko hayo huku wananchi wasijue la kufanya .

View attachment 2204810

Kivuko hicho kinaunganisha Mji wa Kyela na baadhi ya vijiji na kinaanzia kwenye Taasisi ya Mango Tree , hili ni pigo lisilo na mbadala , Daraja la Ipyana nalo limepigwa na miti iliyong'olewa na Mafuriko na kupinda , huku watumiaji wa daraja hilo wakikumbwa na wasiwasi kama waendelee kutumia daraja hilo au la .

Kwa ujumla vijiji vingi vimepigwa na Mafuriko na kiukweli msaada wa haraka unahitajika , ukianzia kijiji changu cha Kajunjumele , Bujesi , ipyana , bujonde , Ndandalo , maeneo yote ya Kyela Mjini yanayotazamana na Hospitali ya Wilaya yote yamezama baada ya mto kiwira kutapika , zipo taarifa kwamba Mamba wameishaingia kwenye makazi ya watu .

Katumbasongwe , Kabanga na Isaki hali ni mbaya sana baada ya Mto Songwe kutapika , huko Mwaya , Tenende na Talatala hali haisemeki baada ya mto Mbaka nao kutapikia makazi ya watu na kusababisha Mafuriko ya Kutisha , kiasi cha kufunika barabara ya Nkuyu - Matema .

Bado hatujajua Juhudi zinazofanya na Serikali ya Wilaya hiyo ili kusaidia wananchi , Japo Gari la Mkuu wa Wilaya linaonekana kuzunguka huku na huko .

Mungu ibariki Kyela .
Hadi nyumba za kyela mjini zimefunikwa?
 
Hivi mvua kuna maeneo bado inanyesha?huku kwetu hakuna hata dalili na kumeanza kuwa na hali ya kibaridi flani,nahisi kipupwe cha mwezi wa sita ndio kinakaribishwa...
 
Poleni ndgu, ila hiyo wilaya sijui tatizo ni nini. Ni karibu kila mwaka mafuriko yanatokea .

Nadhani jiografia ya huko ni kitendawili, Rungwe mvua ni kila siku kwa miezi hii lakini hakunaga mafuriko wala mito kutapika. Na mvua ikiisha tu basi chap kwa haraka maji yanazama ardhini.
Ila huko hali ni tofauti kabisa.
 
Poleni ndgu, ila hiyo wilaya sijui tatizo ni nini. Ni karibu kila mwaka mafuriko yanatokea .

Nadhani jiografia ya huko ni kitendawili, Rungwe mvua ni kila siku kwa miezi hii lakini hakunaga mafuriko wala mito kutapika. Na mvua ikiisha tu basi chap kwa haraka maji yanazama ardhini.
Ila huko hali ni tofauti kabisa.
Hiyo mvua inayonyesha rungwe maji yake yanatiririkia Kyela
 
Back
Top Bottom