NetMaster
JF-Expert Member
- Sep 12, 2022
- 1,454
- 4,846
Alex kamshushia kipigo Israel Adesanya kwa pambano la tatu mfululizo, Katika pambano hili tuliamini kwamba Israel anaenda kulipiza kisasi lakini kilichotokea kapigwa K.O ya aibu sana, kapewa makonde ya kutosha mpaka ikabidi refa amalize pambano, Kwa kuhitimisha ni Kwamba Israel hamuwezi Alex!!
Hadi sasa kwenye UFC mbabe aliebaki ni Jon Jones pekee, kuna kipindi wengi tulipenda Israel apande daraja aende kupigana na Jon Jones lakini huko angetia aibu maradufu, kipigo hiki cha leo kimemsaidia aujue uhalisia mapema.
Ushauri wangu jamaa astaafu tu, kwa sasa akiendelea kufosi atajiharibia hasa ukizingatia kwamba uwezo wake wa kuhimili makonde ya mpinzani (endurance) umeshuka.
Drake kapigwa takribani bilioni 4 na nusu, alibeti Izy atashinda