Kwenye uchaguzi ndani ya umoja wetu wa kufa na kuzikana vipo vituo vingi mawakala waligeuka wapiga kura wa mgombea mwenye nguvu

gimmy's

JF-Expert Member
Sep 22, 2011
3,283
3,271
Natamani hapa nilipo ningeletewa mashekhe,wachungaji,mapadre na waganga wakienyeji waniapishe ili nikisema uongo basi nguvu za kiroho za kokote baina yao zinihukumu.

Hapa mtaani kwetu tuna chama chetu cha kufa na kuzikana na huwa tunagawana madaraka kila baada ya miaka mitano.Kwenye uchaguzi wa mwaka jana kwenye huu umoja wetu wakuchagua viongozi wetu mgombea mmoja hakutenda haki.

Vipo vituo vingi mawakala badala ya kuwa wasimamizi walikuwa robed wakaanza kupiga kura kutwa nzima kwa mgombea mmoja huku wakiwa chini ya uangalizi madhubuti.

Kwenye umoja wetu sisi tumepiga sana hatua kwani Kila mwanachama anakadi maalumu yakupiga kura na kila kadi ina namba maalumu ikiitofautisha na zingine.

Mawakala walikuwa wanachukua makaratasi ya kura wanatizama kwenye register wanahamisha namba za kadi za mpigakura wanapiga tiki kwa yule mwenye mabavu.

Mwaka huu muitikio wa watu kupiga kura ulikuwa mdogo,vituoni kulikuwa tulivu kipindi kingi,hivyo hili zoezi likawa rahisi,

Ni kweli mgombea mwenye nguvu wanasema alishinda lakini zipo kura nyingi sana zilipigwa na wasimazi wa vituo badala ya wapiga kura.

Chaguzi za sarakasi zinaumiza sana tunaiomba serikali iwe inasimamia hivi vyama vyetu vya kufa na kuzikana ili hawa wenye nguvu wasishinde kimabavu.
 
Hayo yamefanyika sehemu nyingi kizuri zaid hata walosimamia uchaguzi nao wanayasema mtaani ko siri yao si siri tena CCM acheni dhihaka kwa Mungu mnaejifanya mnamshukuru majukwaani ili muonekane nyie n wema wakati ni simba kati ya kondoo
 
Kama kweli walipata ushindi mbona wapo kimya tangu jioni ya tarehe 28/ Mshindi wa kweli ni lazima nchi ingelipuka kwa kushangilia huo ushindi kwa sababu ushindi wa kweli unajionesha hata katika nyuso za walioshinda.
 
Kama kweli walipata ushindi mbona wapo kimya tangu jioni ya tarehe 28/ Mshindi wa kweli ni lazima nchi ingelipuka kwa kushangilia huo ushindi kwa sababu ushindi wa kweli unajionesha hata katika nyuso za walioshinda.
Watu waliozea ushindi huwa hawafurahii sana,hapa kazi tu.
 
Huwa inashangaza tukiwa kwenye chama chetu cha kufa na kuzikana yule mgombea mwenye nguvu anatuambia kwa unyenyekevu mkubwa tena huku wakati mwingine mbele ya viongozi wa dini,"Nendeni mkamtangurize Mungu mbere".

Viongozi wetu tendeni haki kwelikweli msifanye dhihaka kwa Mwenyezi Mungu.
 
3 Reactions
Reply
Back
Top Bottom