Kwenye sekta ya Madini - huu ni uwekezaji au ni ukwapuaji?

Juaangavu

JF-Expert Member
Nov 3, 2009
935
132
Wachumi tusaidieni kutafakari hizi takwimu: Mnamo mwaka 1998 - uzalishaji wa madini Tanzania ulikuwa chini ya tani 1 na mchango wake ktk pata la taifa ulikuwa ni 2%; na mara baada ya kupokea wawekezaji wengi ktk sekta hii kufikia mwaka 2005 uzalishaji ulikuwa ni zaidi ya tani 50 na mchango wake ktk pato la taifa ni 3.5%. Wataalam wa mahesabu tusaidieni hapo kuna uwiano wowote; nany watalaam wa uchumi mtusaidie kuelewa sarakasi ya hizi namba.

Hivi haya madini yangeliendelea kubaki huko chini ili hali tunajipanga sisi wenyewe ili tuweze kuyachimba yangilioza au vipi.
Gonga hapa upate details:

Ministry of Energy and Minerals - Documents - Mineral Sector
 

Attachments

  • Mineral_Sector_Overview[1].pdf
    250.9 KB · Views: 597
Kwa mchango wa namna hii kwa pato la taifa, ndo maana Nyerere alitamani tuvune kwanza misitu ili hali tukijijengea uwezo kama taifa wa kuvuna rasilimali zilizoko chini ya ardhi.
 
Tunaibiwa sana!


Mi binafsi natamani kulia. Kwani tungetumia VETA ikasaidia vijana kufanya uchimbaji mdogo mdogo wakia na zana ambazo zimeboreshwa zaidi; na angalau tukaongeza uzalishaji toka hiyo tani moja angalu zikafika hata nne kwa mwaka.

Na pia serikali ikaboresha soko la ununuzi wa hayo madini; kwa kuwa hicho kipato kingelikuwa kinaingia kwenye mifuko ya watz wenzetu mchango wa haya madini ungekuwa zaidi ya hiyo 3.5% (kwa zaidi ta tani 50). Mungu na atusamehe; tumeamua kutupa rasilimali zetu wenyewe kama vile zina upupu
 
Hii yote inatokana na ubinafsi wa viongozi walioshikilia Dola, Kwa nini tusingekopa ili tuwekeze sisi wenyewe na kulipa taratibu, maana hata hayo makampuni yanayowekeza yanakopa mitaji, na Wataalam katika migodi yote ni sis vijana wakitanzania, sasa unashangaa wakina Ngeleja wanacheka cheka tu kwa kuwa wamo kwenye payroll za hawa wawekezaji wanyonyaji. na ndio maana wanajeuri ya hata kutunyanyasa, wanakuja kutoka kwao hawana pesa wanatajirikia hapa kwetu na wanatubagua katika ardhi yetu!, tembelea migodini uone wafanyakazi wanavyobaguliwa kwa rangi zao. ni hatari sana.

Wnapata kipato kikubwa sana hawa jamaa, na kwa kuwa serikali ipo mifukoni mwao haiwezi kuongea ukweli.
 
Unaambiwa huko Liganga tayari makaburu wameanza kukimbiza makaa ya mawe kupitia Mbamba Bay- malawi ,wananchi wanshangaa yanavyovunwa kwa haraka ,nchi ya mazuzu italiwa mpaka imalizwe
 
Hii yote inatokana na ubinafsi wa viongozi walioshikilia Dola, Kwa nini tusingekopa ili tuwekeze sisi wenyewe na kulipa taratibu, maana hata hayo makampuni yanayowekeza yanakopa mitaji, na Wataalam katika migodi yote ni sis vijana wakitanzania, sasa unashangaa wakina Ngeleja wanacheka cheka tu kwa kuwa wamo kwenye payroll za hawa wawekezaji wanyonyaji. na ndio maana wanajeuri ya hata kutunyanyasa, wanakuja kutoka kwao hawana pesa wanatajirikia hapa kwetu na wanatubagua katika ardhi yetu!, tembelea migodini uone wafanyakazi wanavyobaguliwa kwa rangi zao. ni hatari sana.

Wnapata kipato kikubwa sana hawa jamaa, na kwa kuwa serikali ipo mifukoni mwao haiwezi kuongea ukweli.


Hakika huo unaweza kuwa ni mzizi wa tatizo, sijui dhamira zao zimekufa au vipi!

Makanisa na misikitini wanahudhuria kwa wingi na wanatoa michango mikubwa mikubwa, lakini inapokuja kwenye masuala ya kulisaidia taifa kwa ujumla inakuwa kama vile ni misukule.
 
Unaambiwa huko Liganga tayari makaburu wameanza kukimbiza makaa ya mawe kupitia Mbamba Bay- malawi ,wananchi wanshangaa yanavyovunwa kwa haraka ,nchi ya mazuzu italiwa mpaka imalizwe

Ooh! Ina maana intelenjensia inaishia kwa watanzania peke yake. Wapo wapi wana usalama ili waweze kuzuia hii hali.
 
Ooh! Ina maana intelenjensia inaishia kwa watanzania peke yake. Wapo wapi wana usalama ili waweze kuzuia hii hali.

Hawawezi kuzuia, hivi hufahamu kwamba wakati Mali ikiwa inasafirishwa kutoka mgodini walinzi huwa ni FFU wetu! yaani Helicopter hutua chini ya ulinzi mkali wa FFU! jamaa (Wazungu hasa Makaburu) wanapakia mzigo na helicopter inaruka no ukaguzi no what! sasa shanga data wanapata wapi kwamba ton kazaa zimezalishwa na zimepelekwa nje!

Na hawa ndugu zetu FFU wapo tayari kukuchapa risasi ukikatiza tu hata kwa bahati mbaya wakati wa zoezi, na wakati katika nchi hii nafikiri hawa jamaa ndio wanalipwa kiduchu saaaana!

Inashangaza kuona mali amabayo ingelitumiwa vizuri ingeongeza hata kipato chao wanailinda wakati ikiibwa mchana kweupeee.
 
Hawawezi kuzuia, hivi hufahamu kwamba wakati Mali ikiwa inasafirishwa kutoka mgodini walinzi huwa ni FFU wetu! yaani Helicopter hutua chini ya ulinzi mkali wa FFU! jamaa (Wazungu hasa Makaburu) wanapakia mzigo na helicopter inaruka no ukaguzi no what! sasa shanga data wanapata wapi kwamba ton kazaa zimezalishwa na zimepelekwa nje! Na hawa ndugu zetu FFU wapo tayari kukuchapa risasi ukikatiza tu hata kwa bahati mbaya wakati wa zoezi, na wakati katika nchi hii nafikiri hawa jamaa ndio wanalipwa kiduchu saaaana! Inashangaza kuona mali amabayo ingelitumiwa vizuri ingeongeza hata kipato chao wanailinda wakati ikiibwa mchana kweupeee.

Duh! Sijui tufanyeje, kumbe ndo maana tunaambiwa na wana siasa wa upande wa pili kuwa tutabaki na maandaki pale reserves za madini yetu zitakapokwisha.

Afrika nakulilia afrika, afrika nakulilia afrika.
 
Hakika huo unaweza kuwa ni mzizi wa tatizo, sijui dhamira zao zimekufa au vipi! Makanisa na misikitini wanahudhuria kwa wingi na wanatoa michango mikubwa mikubwa, lakini inapokuja kwenye masuala ya kulisaidia taifa kwa ujumla inakuwa kama vile ni misukule.
mkuu uwe unaandika vitu vya uhakika. msikitini hakuna michango ya aina hiyo inayoingia labda huko kwenu makanisani. kwani wengi wa wanaoiba na jamii yenu (ambao wako kwenye system nyonyaji tangu unaoitwa uhuru) na hata hao ambao wanaiba na wangetoa michango labda huko misikitini huwa hawaendi zaidi ya kuishia bar na nyinyi. so please do re-read, usiandike tu kwasababu unataka kujifurahisha.
 
Duh! Sijui tufanyeje, kumbe ndo maana tunaambiwa na wana siasa wa upande wa pili kuwa tutabaki na maandaki pale reserves za madini yetu zitakapokwisha.
Afrika nakulilia afrika, afrika nakulilia afrika.

Kaka ililie Tanzania yako ambayo ndio uozo umezidi, angalau nchi nyingine za Africa zinaanza kujiondoa mtabaki Watanzania wenyewe.
 
Kaka ililie Tanzania yako ambayo ndio uozo umezidi, angalau nchi nyingine za Africa zinaanza kujiondoa mtabaki Watanzania wenyewe.

Nikilia mimi mwenyewe sijui kama hata machozi yangu yatawashitua hawa walo-amua kuifanya tz kuwa shamba la bibi. Kitu zaidi kinatakiwa kufanyika ktk taifa hili
 
Wachumi tusaidieni kutafakari hizi takwimu: Mnamo mwaka 1998 - uzalishaji wa madini Tanzania ulikuwa chini ya tani 1 na mchango wake ktk pata la taifa ulikuwa ni 2%; na mara baada ya kupokea wawekezaji wengi ktk sekta hii kufikia mwaka 2005 uzalishaji ulikuwa ni zaidi ya tani 50 na mchango wake ktk pato la taifa ni 3.5%. Wataalam wa mahesabu tusaidieni hapo kuna uwiano wowote; nany watalaam wa uchumi mtusaidie kuelewa sarakasi ya hizi namba.

Hivi haya madini yangeliendelea kubaki huko chini ili hali tunajipanga sisi wenyewe ili tuweze kuyachimba yangilioza au vipi.
Gonga hapa upate details:

Ministry of Energy and Minerals - Documents - Mineral Sector

Jua angavu umeongea kitu cha ukweli lakini kinauma, ningejua nisingefungua jf leo yaani siku imeharibika
 
Duh! Sijui tufanyeje, kumbe ndo maana tunaambiwa na wana siasa wa upande wa pili kuwa tutabaki na maandaki pale reserves za madini yetu zitakapokwisha.
Afrika nakulilia afrika, afrika nakulilia afrika.

mkuu usiwe kama pinda kulia do something! tuwaondoe haya MAFISADI TUU!
 
[/B][/COLOR]<br />
mkuu usiwe kama pinda kulia do something! tuwaondoe haya MAFISADI TUU!
<br />
<br />

Nimeacha kulia. Hivi Tahir square ya bongo ipo wapi tukajikusanye hapo mpaka kieleweke! Haiwezekana tukawa shamba la bibi kiasi hiki.
 
Back
Top Bottom