Kwenye msiba wa mwizi lazima vibaka wawepo

Imembe

Member
Nov 13, 2020
51
44
Habari wakuu,

Niende kwenye kisa moja kwa moja.

Hapa jirani yangu kuna kijana alikuwa ana jishughulisha na kazi ya wizi,sasa si mnajua siku za mwizi ni 40, sasa jana kaingia sehemu mbaya wakambananisha, akala kichapo heavy hadi kupelekea Kifo

Sasa tukiwa msibani mara kibaka kafanya jaribio la kuiba simu; wazee wakamshitukia, kala kichapo mixer kukatwa mikono

Nb: Wazazi tuwe makini na watoto wetu, maisha au shughuli zisitufanye kusahau majukumu ya malezi ya watoto wetu.
 
Vijana wanapenda maisha maraisi(kitonga)alafu asilimia kubwa jasa wa uswazi,wazazi pia wana wassuport.
wazazi wengi hawana tabia ya kuwashauri watoto wao hata wanaposikia kuwa kijana anabehave vibaya. Matokeo ni kuongezeka kwa vibaka mitaani.
 
Sisi twazika kesho mkuu,ila kwenye hii misiba ya wezi nimegundua hata ndugu awalii kwa uchungu,sijui kwa nini,wakati ni ajali kazini
Tafuta Mama mzazi wa huyo mwizi uone tena hulia kwa uchungu zaidi
 
Habari wakuu,

Niende kwenye kisa moja kwa moja.

Hapa jirani yangu kuna kijana alikuwa ana jishughulisha na kazi ya wizi,sasa si mnajua siku za mwizi ni 40, sasa jana kaingia sehemu mbaya wakambananisha, akala kichapo heavy hadi kupelekea Kifo

Sasa tukiwa msibani mara kibaka kafanya jaribio la kuiba simu; wazee wakamshitukia, kala kichapo mixer kukatwa mikono

Nb: Wazazi tuwe makini na watoto wetu, maisha au shughuli zisitufanye kusahau majukumu ya malezi ya watoto wetu.
Kulikuwa na haja gani ya kumdhulumu iyo nafsi ya huyo mwizi? Roho mbaya tu. Tanzania kila mtu ni mwizi kwenye nafasi yake. Hata wewe mleta mada ni mwizi vilevile kwenye nafasi yako. Mnafanya vibaya sana mkiwapiga na kuwatesa wezi wenzenu. Kuna sheria za nchi akamatwe apekekwe polisi na Sheria itafuata mkondo wake. Wote nyinyi ni maboriti.
 
Kulikuwa na haja gani ya kumdhulumu iyo nafsi ya huyo mwizi? Roho mbaya tu. Tanzania kila mtu ni mwizi kwenye nafasi yake. Hata wewe mleta mada ni mwizi vilevile kwenye nafasi yako. Mnafanya vibaya sana mkiwapiga na kuwatesa wezi wenzenu. Kuna sheria za nchi akamatwe apekekwe polisi na Sheria itafuata mkondo wake. Wote nyinyi ni maboriti.

Mkuu kwa upande wangu sija wahi kushiliki kulusha hata jiwe kumpiga mwizi,Ila jamaa ali kutwa na maswahibu sehemu nyingine kabisa,ila mkuu watu walio ibiwa huwa wana machungu sana.
 
Kulikuwa na haja gani ya kumdhulumu iyo nafsi ya huyo mwizi? Roho mbaya tu. Tanzania kila mtu ni mwizi kwenye nafasi yake. Hata wewe mleta mada ni mwizi vilevile kwenye nafasi yako. Mnafanya vibaya sana mkiwapiga na kuwatesa wezi wenzenu. Kuna sheria za nchi akamatwe apekekwe polisi na Sheria itafuata mkondo wake. Wote nyinyi ni maboriti.
usitufokeee,ndio ashauwawa sasa kwa wizi wake,kwahiyo unasemaje?
 
Maisha yamekuwa magumu MTU unakuwa bize mpaka mda wa kukagua familia huna unashangaa kijana kashahama kwenye mstari

Mzazi unakuja kugundua huku ushachelewa
Uswahilini vijana wanapomaliza shule wazazi wengi huwa hawana habari nao
Sasa hapo nguvu ya tamaa inaanza kumwingia taratiibu ukichanganya na hayo makundi mambo yanaanza kuharibika hapa
 
Chanzo cha mambo haya yote ni ubovu wa vyombo vya kusimamia sheria na kulinda usalama wa raia na mali zao. (Polisi na mahakama).

Hawa watu wangekuwa wanasimamia sheria bila kupinda pinda (rushwa) haya yasingetokea.

Kwanini?

Mwizi anaweza kukamatwa watu wakampeleka kituoni achukiliwe hata kisheria lakini huko ndugu zake wanajichanga wanaenda kituoni wanatoa hongo/rushwa jamaa mnashangaa amerudi kitaa anaendelea na tabia yake.

Inafika mahali anaona poa tu akikamatwa ndugu watamtoa au akienda sero siku 14 askari hawafuatilii kupeleka ushahidi mahakamani hakimu anatupia faili lake kapuni mtu anarudi mtaani.

Hapo ndio wanachi wanaamua tu kuchukua sheria mkononi maana wanaona wale waliopewa kazi wameshindwa na wao kila siku mali zao haziko salama. Wanaona ni bora kumkill tu.

Unfortunately pia kuna some cases hata mkitoa taarifa kuwa kuna mwizi amekamatwa kituoni response ya polisi ni very slow kiasi kwamba mpaka wafike eneo la tukio hata waliokuwa pale walishasahau tukio lenyewe.
 
2 Reactions
Reply
Back
Top Bottom