Kwenye medani za Sheria Nani mkali Kati ya Lissu na Kibatala?

Superbug

JF-Expert Member
Jan 31, 2018
12,405
30,908
WanaJF Naomba mnisaidie Kati ya hawa manguli kibatala na Lissu na mkali zaidi ambae hashindwi kesi kirahisi na ambae anaogopeka sana na mawakili na mahakimu.
 
Wana jf Naomba mnisaidie Kati ya hawa manguli kibatala na Lissu na mkali zaidi ambae hashindwi kesi kirahisi na ambae anaogopeka Sana na mawakili na mahakimu.
Wote wapo vizuri, Sasa hakimu atawaogopaje wanasheria wenzie boss,

Kibatala anaenda kuwa Bora zaidi,
 
Hili swali ungemuuliza hata viongozi wakuu wastaafu wala wasingepepesa macho. Anajulikana. Kibatala ni number mbili. Kisha akina mtobesya, fatma, mayalla etc
 
Wana jf Naomba mnisaidie Kati ya hawa manguli kibatala na Lissu na mkali zaidi ambae hashindwi kesi kirahisi na ambae anaogopeka Sana na mawakili na mahakimu.
Wote ni mawakili bora kabisa kuwahi kutokea Tanganyika.

Kibatala ni Junior kwa Lisu hata yeye mwenyewe ukimuuliza swali hili hawezi kupenda ulichouliza.

Ni ngumu kupata jibu la moja kwa moja kati ya Mesi na Christian Ronaldo nani zaidi.

Kuna wajinga walifikia hata hatuwa kutaka kumfananisha marehemu Magufuli na Hayati Baba wa Taifa.
 
Wana jf Naomba mnisaidie Kati ya hawa manguli kibatala na Lissu na mkali zaidi ambae hashindwi kesi kirahisi na ambae anaogopeka Sana na mawakili na mahakimu.
Niliwahi kumuuliza wakili msomi mmoja swali hili...Majibu yake ni kwamba kwa ujuzi wake wote ni wazuri ila kibatala yeye anamuona mzuri zaidi kwa sababu ameshinda kesi za prosecution kuliko lisu ambaye ameshinda kesi nyingi za defence hivyo yeye anaona kesi za prosecution ni ngumu zaidi hivyo anampendekeza kibatala.
 
Back
Top Bottom