Kwenye kumuaga Balozi Kijazi, Kikwete ametuma ujumbe mzito kwa vitendo

Tuache upotoshaji wa makusudi na kujenga fitna. Wote tunafahamu ni haki yake Mhe.Jakaya Kikwete kuvaa barakoa nk, kunakochagizwa na mazingira ya umri na afya yake !

Nalaani siasa chafu kwa jamii kwa kutumia matukio kama haya. Na kila anayeshadidia na kuanzisha upoteshaji kupitia misiba ,atanguliye mbele za haki upesi.
Duh Afya yake tena ? Sasa hapo nani analeta upotoshaji ?

Pia kumbuka anayevaa Barakoa sio kwamba anaogopa asiambukizwe au hawezi kuambizwa bali ni kwamba anajali kutokuwaambukiza wengine..., (Sio kwamba yeye anao la hasha ila huwezi kujua huenda ametoka kuupata siku chache na hajui, kama mimi na wewe ambavyo hatujui ukizingatia vipimo havipo wazi)

Kwahio mara nyingine anayevaa Barakoa jua kwamba anajali kupunguza maambukizi kwa watu wengine... Wote wakivaa itapunguza maambukizi ambayo watu wakiwa hawana chochote ni rahisi kuambukizana..

Anyway kuvaa kwake Barakoa kunaweza kutafsiriwa kwamba he cares na wengine waliokuwa wanaona aibu wataonekana wa ajabu wasiogope kuvaa

Hususan baada ya Kiongozi mkuu anavyoonekana akitoa pongezi kwa wale wasiovaa
 
Safu ya uongozi wa nchi imekaa mbele, kuna waziri mkuu, makamu wa raisi naibu Spika. Wote hawa hawajavaa barakoa na wala hawako umbali unaofikia mita mbili kutoka kwa kila moja. Hata hivyo raisi Mstaafu JK amepiga barakoa yake.

Je, tunapata meseji gani kama Watanzania?

Ni dhahiri kiongozi mstaafu anaonyesha mfano kuwa hizi nyakati siyo za kujiachiaachia.

Nawaonea huruma viongozi wengine ambao badala ya za kuambiwa na jiwe wachanganye na zao, wao wanajiexpose kwenye kwenye line ya hatari ya maambukizi.

Sisi kama Taifa tunapaswa kufuata mfano mwema kama wa JK

Hapa chini JK kapiga barakoa

View attachment 1706197

View attachment 1706196
Kimwete labda ana mafua na hakutaka kuwaambukiza wengine🤔! We vipi? Chikwete Chikwete! Mfyuuuuu!
 
At least inasaidia. Ndiyo maana wataalam wakashauri. Kwa taarifa yako barakoa zomeshauriwa kuvaliwa pale ambapo social distancing haiwezekani. Ndiyo maana tunahimiza serikali kufundisha njia za kujikinga. Sasa mtu kama wewe kama hili linakushinda kuelewa vipi wale ma-layman?

SERIKALI INATAKIWA IFUNDISHE KUWA WATU WAVAE BARAKOA NA PENYE MKUSANYIKO 'SOCIAL DISTANCING NI MUHIMU".
KWA MFANO HAPO KUNA UGUMU GANI KUPANGA VITI MBALI MBALI KWANI KUNA NAFASI!! HATA KWENYE MIKUTANO INAWEZA KUHIMIZWA KUWA WATU WAWE MBALI MBALI BADALA YA KUBANANA!!! CAN YOU BELIEVE YOU CAN HAVE A POLITICAL RALLY WHILE OBSERVING SOCIAL DISTANCING!!! SASA KWA VILE MMEAMANISHWA KUWA HAKUNA CORONA NDIO MANA MNAFANYA MAMBO BILA KUWA MAKINI NA MATOKEO YAKE MNAPOTEZA HAZINA YA WATU WENYE UZOEFU AMBAYO NI IMPOSSIBLE TO REPLACE!!
 
SERIKALI INATAKIWA IFUNDISHE KUWA WATU WAVAE BARAKOA NA PENYE MKUSANYIKO 'SOCIAL DISTANCING NI MUHIMU".
KWA MFANO HAPO KUNA UGUMU GANI KUPANGA VITI MBALI MBALI KWANI KUNA NAFASI!! HATA KWENYE MIKUTANO INAWEZA KUHIMIZWA KUWA WATU WAWE MBALI MBALI BADALA YA KUBANANA!!! CAN YOU BELIEVE YOU CAN HAVE A POLITICAL RALLY WHILE OBSERVING SOCIAL DISTANCING!!! SASA KWA VILE MMEAMANISHWA KUWA HAKUNA CORONA NDIO MANA MNAFANYA MAMBO BILA KUWA MAKINI NA MATOKEO YAKE MNAPOTEZA HAZINA YA WATU WENYE UZOEFU AMBAYO NI IMPOSSIBLE TO REPLACE!!
Uliyoondika ndiyo msimamo wangu. Bila kupepesa macho wala wasiwasi. Ila kwenye comment yako (pengine kwa kukuelewa vibaya) niliona kama umeponda uvaaji mask! Kumbe wewe umetaka pia kuwe na distance (kitu ambacho ni kizuri zaidi). Tupo kwenye meli moja!
 
Wanatuhadaa tu wakirudi kwenye gari wanajisanitizer wengine washajidunga astrazeneca
 
Pumbavu kabisa. Kuna watu wengi mna akili za kipumbavu kabisa. Hao virusi wako kwenye mate mate. Kama mtu anavaa barakoa, kama ana virusi hivyo, akikohoa, anakuwa amewalinda wengine. Kuna mtu alisema kuwa ni “Airborne”, kwahiyo hakuna haja ya kuvaa mask kwasababu eti hivyo vitambaa sijui havizuii! Upumbavu wenu usiwe msiba kwa Taifa.
Mbona unaonyesha udhaifu wako Kwa watu hadharani?,. Virusi vya corona havina ukubwa saize ya mbu au nzi kiasi cha kuzuliwa na hilo likitambaa ulilovaa puani na mdomoni,,usilishwe matango poli na wewe unajishangilia km zuzu,
 
Wasiovaa barakoa kwa kumsikiliza Jiwe hawana tofauti na askari wa Kinjekitie walioamini maji ya bwana mkubwa yanaweza kugeuza risasi kuwa maji!
 
Yeye hana haja ya kujipendekeza kwani hana wa kumtumbuia wala kutafuta cheo ni Rais Mstaafu hana mtu wa kumwondolea hicho cheo wala kujipendekeza kwa mtu.
Mtoto wa mjini anajua kujilinda. Anafata maelekezo ya wataalamu.

Ni sawa na kusema Mtoto wa mjini hali mzigo bila kinga
 
Hiyo ndio hoja wewe uliyoniona ya Nashik? Kuna mtu kazuiliwa kuvaa barakoa? Unashida mahari furani hapako vizuri wewe.
Usikatae kuna ujumbe mzito sana. Mkuu angeva na hao wasaidizi wake wangevaa. Hii ni migongano kinzani ndani ya mtu
Akivaa atakuwa amempinga mkuu japo atakuwa salama. Asipovaa atakuwa anamsapoti na atakuwa salama kwa kazi yake japo anahatarisha afya yake.
Ni sawa na binti anapata scolarship na hapo kampata mchumba achague kimoja.
Usifikiri wote wanaosujudu wanapenda...
 
Usikatae kuna ujumbe mzito sana. Mkuu angeva na hao wasaidizi wake wangevaa. Hii ni migongano kinzani ndani ya mtu
Akivaa atakuwa amempinga mkuu japo atakuwa salama. Asipovaa atakuwa anamsapoti na atakuwa salama kwa kazi yake japo anahatarisha afya yake.
Ni sawa na binti anapata scolarship na hapo kampata mchumba achague kimoja.
Usifikiri wote wanaosujudu wanapenda...
Halafu ndani ya korona viongozi wakuu wanatoa ujumbe gani kwa raia na dunia. Kikwete ametoa ujumbe gani. Nani sahihi. Upi ni ushujaa. Hii dini mpya ya kumtukuza binadamu itatupeleka wapi!
 
Mbona unaonyesha udhaifu wako Kwa watu hadharani?,. Virusi vya corona havina ukubwa saize ya mbu au nzi kiasi cha kuzuliwa na hilo likitambaa ulilovaa puani na mdomoni,,usilishwe matango poli na wewe unajishangilia km zuzu,
The viruses are in the moist. Ujinga wako usiwe msiba kwa Taifa.

Barakoa za kutengeneza nyumbani ziko Sawa tu vile vile.
 
Back
Top Bottom